Katiba ya Tanzania na Mipaka ya Uhuru wa Kujieleza

Katiba ya Tanzania na Mipaka ya Uhuru wa Kujieleza

Basi huko KKKT kumejaa vilaza usiombe. unajua qualification ya kuwapata maskofu haiko kwenye wingi wa akili ama upeo ? Kwa RC bishops ni mapadri hawa hawa wanaokesha na kushida wakimbembeleza misaada wakati miundo mbinu ya pesa wameikalia. Ni tamko moja tu la maaskofu lina ukweli na hakika nalo si hilo walilobandika hapo.
 
Habari wakuu,

Kumekuwa na wimbi la watu wachache wanaokuja na hoja dhaifu eti uhuru wa kujieleza umebanwa.

Kwanza naomba niweke wazi kuwa watanzania wanataka maendeleo hawataki uhuru wa kujieleza kwani ukiwa na njaa kujieleza hakusaidii kitu chochote.Hii ndo sababu ya Libya kumkumbuka Gaddafi.

Embu nijikite kwenye hoja ya msingi kuwa, je wanaotaka uhuru wa kujieleza wanaelewa maana yake?

Je wao wanakubali mawazo yasiyoridhisha matakwa yao?

Tumeshuhudia hata humu ndani wale magwiji wa kuzungumzia kuwa uhuru wa kujieleza umegandamizwa wakiwatukana na kuwakebehi na kuwapa majina mbali mbali kama wachumia tumbo, wataka vyeo, wanajipendekeza na matusi kadhaa wale wasioendana nao kimawazo instead ya kuheshimu mawazo yao kama ulivyo muhimili mkubwa unaounda uhuru wa kuongea.

Pia tumeshuhudia mitandaoni wale wanaohuburi uhuru wa kuongea ndio mabingwa wa kublock watu wanaopingana nao kimawazo.

Je uhuru wao wa kuongea ni kuongea yale yanaowafuraisha?

Nimekuwa muhanga mkubwa wa maneno ya kebehi na matusi kuwa natumika naomba niweke wazi kuwa mimi nashabikia kile nachokiona sahihi na sifanyi kwa ajili ya kupata kitu fulani na sijawahi kupata kitu chochote.
[emoji106][emoji106][emoji106][emoji106][emoji106][emoji106][emoji106]
 
Habari wakuu,

Kumekuwa na wimbi la watu wachache wanaokuja na hoja dhaifu eti uhuru wa kujieleza umebanwa.

Kwanza naomba niweke wazi kuwa watanzania wanataka maendeleo hawataki uhuru wa kujieleza kwani ukiwa na njaa kujieleza hakusaidii kitu chochote.Hii ndo sababu ya Libya kumkumbuka Gaddafi.

Embu nijikite kwenye hoja ya msingi kuwa, je wanaotaka uhuru wa kujieleza wanaelewa maana yake?

Je wao wanakubali mawazo yasiyoridhisha matakwa yao?

Tumeshuhudia hata humu ndani wale magwiji wa kuzungumzia kuwa uhuru wa kujieleza umegandamizwa wakiwatukana na kuwakebehi na kuwapa majina mbali mbali kama wachumia tumbo, wataka vyeo, wanajipendekeza na matusi kadhaa wale wasioendana nao kimawazo instead ya kuheshimu mawazo yao kama ulivyo muhimili mkubwa unaounda uhuru wa kuongea.

Pia tumeshuhudia mitandaoni wale wanaohuburi uhuru wa kuongea ndio mabingwa wa kublock watu wanaopingana nao kimawazo.

Je uhuru wao wa kuongea ni kuongea yale yanaowafuraisha?

Nimekuwa muhanga mkubwa wa maneno ya kebehi na matusi kuwa natumika naomba niweke wazi kuwa mimi nashabikia kile nachokiona sahihi na sifanyi kwa ajili ya kupata kitu fulani na sijawahi kupata kitu chochote.
Ndo tatizo lililopo humu jukwaani,ukiwa tofauti kimtizamo unatukanwa ile mbaya ,kosa kua tofauti na wanachokiwaza wao,sasa sijui wao ni malaika?
 
Habari wakuu,

Kumekuwa na wimbi la watu wachache wanaokuja na hoja dhaifu eti uhuru wa kujieleza umebanwa.

Kwanza naomba niweke wazi kuwa watanzania wanataka maendeleo hawataki uhuru wa kujieleza kwani ukiwa na njaa kujieleza hakusaidii kitu chochote.Hii ndo sababu ya Libya kumkumbuka Gaddafi.

Embu nijikite kwenye hoja ya msingi kuwa, je wanaotaka uhuru wa kujieleza wanaelewa maana yake?

Je wao wanakubali mawazo yasiyoridhisha matakwa yao?

Tumeshuhudia hata humu ndani wale magwiji wa kuzungumzia kuwa uhuru wa kujieleza umegandamizwa wakiwatukana na kuwakebehi na kuwapa majina mbali mbali kama wachumia tumbo, wataka vyeo, wanajipendekeza na matusi kadhaa wale wasioendana nao kimawazo instead ya kuheshimu mawazo yao kama ulivyo muhimili mkubwa unaounda uhuru wa kuongea.

Pia tumeshuhudia mitandaoni wale wanaohuburi uhuru wa kuongea ndio mabingwa wa kublock watu wanaopingana nao kimawazo.

Je uhuru wao wa kuongea ni kuongea yale yanaowafuraisha?

Nimekuwa muhanga mkubwa wa maneno ya kebehi na matusi kuwa natumika naomba niweke wazi kuwa mimi nashabikia kile nachokiona sahihi na sifanyi kwa ajili ya kupata kitu fulani na sijawahi kupata kitu chochote.
Hujui kabisa maana ya maendeleo rudi kidato cha tatu ukajifunze tena nini maana ya Social development.

Pili ina maana wewe una akili kuliko wale waliotunga katiba?
Watunga katiba waliweka uhuru wa kuongea kama haki ya msingi ya kila raia.

Tatu nani alikudanganya kuwa uhuru wa kuongea unazuia maendeleo?

Naomba unipe nadharia hata moja unayosema kuwa ukiwazuia watu wasiongee mawazo yao utafanya maendeleo yapatikane kwa haraka!!!!!!
 
Nachelea kusema kwamba kumekua na shutuma kuu zinazoelekezwa kwa Serikali ya Tanzania kwamba imezigandamiza haki za binadamu haswa haki ya Uhuru wa kujieleza na kutoa maoni.

Ni ukweli ulio wazi kwamba Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 katika Ibara ya 18 Ibara ndogo ya kwanza imetoa haki ya kila raia kuwa na uhuru wa kutoa maoni kwa maana ya kujieleza na kutoa nje mawazo kuhusu masuala mbalimbali na pia kupokea na kuto taarifa kutoka katika chombo chochote.

Hivyo basi sio kosa kisheria kwa raia yeyote kutoa maoni na mawazo kwa sababu tayari Katiba ambayo kimsingi ndio sheria mama imeshakikisha kwamba haki hiyo inapatikana kwa kila raia.

Nikiinukuu Ibara hiyo kama ilivyoandikwa inasema hivi;

"Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati."

Hapo mwanzo kabisa wa ibara hiyo ya 18 tunaona neno “BILA YA KUATHIRI SHERIA ZA NCHI” Sheria za nchi ni zipi? Sheria za nchi ni jumla ya ile miswada ambayo ilipitishwa na Bunge katika taratibu na kanuni zake za utungaji wa sheria kisha ikasianiwa na Rais wa Jamhuri wa Muungano na kuwa sheria kamili.

Sawa, Katiba imetoa haki ya kutoa maoni na kujieleza lakini pia Katiba hiyo hiyo imetoa masharti kwamba unapotaka kutekeleza haki yako hiyo basi inakupasa usivunje sheria nyingine za nchi.

Ibara ya 30 ya Katiba yetu imeweka Mipaka kwa haki na uhuru na hifadhi kwa haki na wajibu.

Katiba inasema;
"Haki na uhuru wa binadamu ambavyo misingi yake imeorodheshwa katika Katiba hii havitatumiwa na mtu mmoja kwa maana ambayo itasababisha kuingiliwa kati au kukatizwa kwa haki na uhuru wa watu wengine au maslahi ya umma"

Maana yake ni kwamba haki na uhuru wa mtu binafsi haupaswi kuwa chanzo cha kukosa haki na uhuru kwa watu wengine au umma kwa ujumla. Hivyo hakuna haki au uhuru usio na mipaka. Mipaka au ukomo wa haki na uhuru ni kwa kiwango haki na uhuru wako unavyoweza kuathiri au kuingilia haki na uhuru wa wengine.

Kanuni kuu ya kufahamu juu ya dhana ya haki na uhuru wako ni ile kanuni ya kimaandiko inayosema ‘mpende jirani yako kama nafsi yako mwenyewe’ hii inaonesha kwamba kwa kiwango kile ambacho ungependa haki zako na uhuru wako uheshimiwe na kulindwa basi hakikisha nawe unafanya kwa kiasi hicho kwa jirani yako. Jirani yako ni mtu yeyote ambaye anaathirika kwa njia moja ama nyingine kutokana na kauli zako au matendo yako. Kama usingependa utu wako udhalilike, kwa matusi kebehi na fedheha basi jitahidi pia uulinde utu huo wa mwenzako.

Katiba inaendelea pia kuainisha juu ya mipaka ya haki na uhuru kwa kusababisha sheria kutungwa ili kulinda haki za watu wengine na maslahi mapana ya umma kwa ujumla, sawa na Ibara ya 30 (2) inasema;
"Ifahamike kwamba masharti yaliyomo katika Sehemu hii ya Katiba hii, yanayofafanua misingi ya haki, uhuru na wajibu wa binadamu, hayaharamishi sheria yoyote iliyotungwa wala kuzuia sheria yoyote kutungwa au jambo lolote halali kufanywa kwa mujibu wa sheria hiyo ."

Hapa maana yake ni kwamba mamlaka pamoja na kuzitambua na kuziheshimu haki na uhuru wa kila raia, zinaweza kutunga sheria kwa ajili ya kulinda na kutetea haki za watu wengine na makundi mengine ikiwepo serikali na mambo yote ya maslahi ya umma.

Mfano Sheria ya Kanuni ya adhabu,Sura ya 16 kifungu cha 89 kifungu kidogo cha kwanza kimeweka adhabu ya kifungo cha miezi 6 kwa mtu yeyote atakayetumia lugha ya matusi dhidi ya mtu mwingine.

Hivyo mtu kabla hujaamua kutekeleza haki yako yoyote lazima uifahamu mipaka yake na namna ambavyo sheria zinalinda watu wengine na mamlaka za nchi dhidi ya kuharibiwa sifa au udhalilishaji.

Eneo la mipaka ya haki na uhuru limekuwa na changamoto kubwa sana katika kufikia mwafaka, kwani wapo wanaoamini kuwa haki hizi za kibinadamu hazina mipaka lakini wapo wanaamini kuwa haki zina mipaka. Katiba imeweka wazi kuwa katika kutekeleza haki yako hakikisha upo ndani ya mipaka husika.

Hakikisha kwenye uhuru wako wa kujieleza au imani yako au faragha kwa namna yoyote hauingilii haki na uhuru wa watu wengine, shughuli za umma, mamlaka za nchi, hadhi za watu ikiwa ni viongozi au raia wa kawaida.

Ni rai yangu kwa wananchi wenzangu kuwa na taadhari katika maneno na vitendo tunavyofanya kwa kudhani kuwa tuna haki tu ya kufanya chochote, sheria zipo na mamlaka za kutekeleza sheria zipo, tuepuke kuwa na matumizi mabaya hasa ya mitandao kutuma na kupokea jumbe ambazo zinaweza kuingilia haki na uhuru wa watu wengine na mamlaka mbali mbali katika nchi yetu.

Hakuna Haki na Uhuru usio na mipaka, jua mipaka yako uepuke madhara kwa wengine na juu yako. Kumbuka kutokujua sheria si utetezi iwapo utatenda kosa lolote.

Tekeleza haki zako za kikatiba lakini zingatia usivuke mpaka wala kuvunja sheria nyingine za nchi .Usipofanya hivyo nyundo ya sheria itakugonga na hautakua na mtetezi wa kukusaidia pindi utakapofungwa gerezani.
 
Ndio maana wanapiga kelele za katiba mpya
 
FISIEMU.jpg
 
Kwa mfano kwenye maongezi yako yote ukasema DICTETA uchwara utakua umekosea kisheria mpaka ukajikuta kizimbani?
 
Unataka kusema nini
Kuwa muwazi
Kwa hivi wanaotaka katiba mpya ni mazuzu wewe ndio mwenye kuilewa zaidi
Endelea.....
 
Ni sheria ipi iliyotungwa na Bunge kwamba mikutano ya kisiasa mpaka 2020? Na kwamba baadhi ya vyama na viongozi hawafungwi na sheria hiyo? HAKI na USAWA ni maneno mafupi sana brother lakini yaliyoshikilia mustakabali wa taifa isipokuwa kwa walevi. Ni punguani pekee asiyeona double standards za waziwazi zilizopo.
 
Kuna Watu walikamatwa sababu ya kuvaa T-shirts Zimeandikwa Njaa,Ukuta..nk
Walivunja Sheria gani?
Wengine Walienda kujitolea Damu kwa Ajili ya Lissu..Walivunja Sheria Gani..?
Kwenye Swala la Kujieleza mf: Askofu Kakobe alivunja Sheria gani?
Hii Awamu Kubalini tu Haki za Binadamu zinavunjwa ..Na Mnaofaidika na huu utawala endeleeni Kushabikia..
 
  • Thanks
Reactions: exo
Wanabodi,

Mvutano kati ya wanasiasa ni jambo la kawaida sana nchini Tanzania. Vurugu za hapa na pale huwa zinatokea sana na kwa bahati mbaya, wana siasa wa vyama vya upinzani wamefanywa mfano mbaya kwa kutiwa nguvuni na vyombo vya usalama mara kadha. Katika vipindi vingine wana siasa hawa wa vyama vya upinzani walifikishwa mahakamani baada ya vyombo vya usalama kuweza kufungua mashtaka dhidi yao. Kesi za uchochezi au kukamatwa kwa kufanya mikutano ya hadhara na hata mikutano ya ndani ya chama ni jambo la kawaida sana. Wana siasa hawa wameisha jaribu kuwa elewesha wananchi kuhusu haki zao kikatiba zinazo waruhusu kufanya shughuli zao lakini vyombo vya usalama havija wahi kuwasikiliza wala kuacha kuingilia shughuli zao.

Swali muhimu la kujiuliza ni kwamba, je haki ya kujieleza ina mipaka ipi Tanzania?. Je ni kweli kwamba katiba ya Tanzania hairuhusu shughuli za kisiasa nje ya kipindi cha uchaguzi?. Je maandamano ya amani na mikutano ya mitandaoni inapotosha umma au kuleta sinto fahamu nchini?.

Ikifikia hatua ambayo vyombo vya usalama vinaweza kumuweka yeyote mahabusu, kufungia vyombo vya habari au mahakama kuweza kusikiliza mashtaka ya yeyote, je katiba yetu ikoje kuhusu mambo kama hayo?. Ikitokea kwamba umekamatwa, je lazima vyombo vya usalama viwe na ushahidi wa kiasi fulani kuweza kuendelea kukushikilia?

Mwisho kabisa, nina amini kwamba nchi ambayo ni ya kidemokrasia lazima iwaruhusu wananchi kujieleza kwa uhuru. Vile vile uhuru huu unaweza kutumiwa vizuri au vibaya na ndio maana lazima mipaka iwepo. Je uhuru wa kujieleza Tanzania una mipaka ipi?.
 
Mkuu licha ya uwepo wa mipaka katika uhuru wa kujieleza hapa nchini.

Je! Katika mipaka hiyo moja ya chanzo chake ndiyo iwe inatokana na katazo ambalo linatolewa kupitia tamko la Rais lenye kukinzana na katiba, sheria na kanuni za nchi yetu?

Je! Mipaka hiyo pia iwe inatokana na hisia za viongozi wa vyombo vya dola wenye kujipendekeza kwa chama tawala hasa waliopo katika Jeshi la Polisi, wenye kutafuta visingizio kila kukicha kuwa wamepokea amri kutoka juu kuhalalisha dhuluma ili kuzuia haki zilizoainishwa kikatiba na kisheria?
 




Huo ndio uhuru wa kupata habari mnaoutaka, iwe hiyo story imerushwa karibu na vyombo vyote vya online media.

Huu upuuzi mbona atukusikia zama za Magufuli, same thing wanasiasa na magazeti wana tabia za kutungia vyama vingine, viongozi wao na serikali mambo ya uongo mtupu.

Uwezi kuachwa unalisha jamii ujinga na uachwe.

Yaani kuna mashahidi kabisa kuna mama kajingua ‘hedgehog’ huko bariadi.

Nashangaa Dr Abbas yupo kimya mpaka kwenye ili sakata.

Isitoshe maandamano na mikutano ya siasa, as nothing na uhuru wa kujieleza soma katiba vizuri kuna vipengele maelezo yake on rules of engagement ya ivyo vitu.
 
Back
Top Bottom