Katibu CDM Ngorongoro ashikiliwa polisi kwa kujifanya Katibu mkuu maliasili na utalii

Katibu CDM Ngorongoro ashikiliwa polisi kwa kujifanya Katibu mkuu maliasili na utalii

Hiyo ni gharama ya mapambano dhidi ya CHAMA CHA UKOO..angalia asiandikiwe ya mauaji.
 
inatia mashaka yaaani mfanyakazi wa ngazi ya juu wanyama pori hafahamu sauti au namba ya waziri wake au katibu wa wizara acheni masihara
 
Hivi na CHADEMA nao wanaita viongozi wao wa Kata "KATIBU KATA"? Now wonder mwandishi na sub editor wa gazeti makini ya la SAUTI HURU kusema kuwa Mnyika ni KATIBU WA ITIKADI NA UENEZI WA CHADEMA!

Too Low
 
Habari hii imetoka kwenye magazeti pinzani wa chadema - utata wa kwanza.
Tofauti kati ya CCM na CHADEMA siyo kwamba Chadema ni Malaika hivyo kila kitu ni kizuri sana kama mbinguni, hapana. Ila tofauti ni Chadema wanawachukulia hatua wahusika kwa mujibu wa sheria pale inapothibitika na ccm ukijiuzulu basi. Hata kama umeiba mabilioni ya umma.
 
Bado haiingii akilini Katibu Kata wa Chadema kujifanya Katibu Mkuu wa Wizara? Tena kwa Mhifadhi mkuu wa Ngorongoro? something wrong somewhere.
 
Ni kweli kuna issue ya kama hii,na leo asubuhi tumefika kituo cha polisi na Denis ametakiwa kurudi Jumatatu.
Hili swala lina utata,hasa mazingira yake,na jitihada za huyu Kamanda wetu Denis Katibu Kata wa Enduleni,amepambana sana na mafisadi,wanaamini kuwa ana documents za siri,wanamlazimisha kuwa aseme nani anamtolea hizo docs
Haki na ukweli vitashinda
Aluta continua
 
Mbinu zingine za kubebesha watu uovu hazina hata miguu na kichwa,huyo veronica hajui numba za mabos wake??hainamantiki yoyote nu upuuzi mtupu.ngoja tuone mwisho wake!
 
Hapa kuna mchezo mchafu hata ukiangalia kwenye gazeti utajua hii habari ina ushabiki.

Cdm si chama cha malaika, kama itathibitika yeye kuhusika lazima hatua stahiki zita chukuliwa!

Lakini bado nina mashaka na hili swala!
 
Chama cha matapeli wezi na wanyang'anyi kadri cku zinavyoenda ukweli unajionyesha mtashangaa wenyewe mnaoshabikia upuuzI wao
 
Wanabodi
Katibu kata wa CHADEMA kata ya Enduleni Ngorongoro ameshikiliwa kituo kikuu cha polisi Arusha, baada ya mtego aliowekewa kumnasa, Katibu huyu Denis Paulo alijifanya kuwa ni Katibu mkuu wa wizara ya utalii, kisha kumpigia Mhifadhi utalii wa NCAA Bi Veronica na kumtaka atoe Mil I6, ili kumsaidia kwenye tume iliyoundwa na waziri kuchunguza ubadhirifu mkubwa kwenye mamlaka hiyo.

Baada ya mahojiano na polisi Katibu huyo amekana kujua chochote, nilikutana na Nanyaro ambaye ni mmoja wa viongozi wa CHADEMA mkoa wa Arusha, na akakiri kumwekea dhamana polisi, ni kweli huyu ni katibu wa chama kata ya enduleni, nimemdhamini kwa masharti kuwa aripoti kituoni kesho asubuhi, mazingira ya kukamatwa kwake yanatia mashaka sana,

Ukumbuke kuwa Katibu huyu alifanikisha kuhamisha zaidi ya wanachama 2800 wa CCM wakahamia CHADEMA, mapema mwaka huu, kesho nitakuwa kwenye nafasi nzuri ya kulizungumzia baada vingozi wenzangu, alisema Nanyaro

Ina maana huko serikalini hela inatoka kwa kumpigia tu mtu simu ya mkwara?!!
 
Wanabodi
Katibu kata wa CHADEMA kata ya Enduleni Ngorongoro ameshikiliwa kituo kikuu cha polisi Arusha, baada ya mtego aliowekewa kumnasa, Katibu huyu Denis Paulo alijifanya kuwa ni Katibu mkuu wa wizara ya utalii, kisha kumpigia Mhifadhi utalii wa NCAA Bi Veronica na kumtaka atoe Mil I6, ili kumsaidia kwenye tume iliyoundwa na waziri kuchunguza ubadhirifu mkubwa kwenye mamlaka hiyo.

Baada ya mahojiano na polisi Katibu huyo amekana kujua chochote, nilikutana na Nanyaro ambaye ni mmoja wa viongozi wa CHADEMA mkoa wa Arusha, na akakiri kumwekea dhamana polisi, ni kweli huyu ni katibu wa chama kata ya enduleni, nimemdhamini kwa masharti kuwa aripoti kituoni kesho asubuhi, mazingira ya kukamatwa kwake yanatia mashaka sana,

Ukumbuke kuwa Katibu huyu alifanikisha kuhamisha zaidi ya wanachama 2800 wa CCM wakahamia CHADEMA, mapema mwaka huu, kesho nitakuwa kwenye nafasi nzuri ya kulizungumzia baada vingozi wenzangu, alisema Nanyaro
[/QUOTE mpalu loading......
 
[h=2][/h] Ijumaa, Agosti 31, 2012 06:27 Na Eliya Mbonea, Arusha

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimekumbwa na tuhuma nzito baada ya kiongozi wake mmoja kukamatwa kwa kosa la utapeli wa Sh milioni 16.

Kiongozi huyo ambaye ni Katibu wa Kata ya Endulen wilayani Ngorongoro, Denia Paul (33), anadaiwa kuwatapeli wafanyakazi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCCA) kiasi hicho cha fedha, kwa kujifanya kuwa yeye ni Katibu wa Wizara ya Maliasili na Utalii.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini wake mjini hapa jana, Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Arusha, Lebaratus Sabas, alisema kuwa, mtuhumiwa huyo alikamatwa Agosti 27, mwaka huu.

“Kabla ya kukamatwa, Paul aliwapigia simu wafanyakazi wa NCCA, akijitambulisha kuwa yeye ni Mwenyekiti wa Tume iliyoundwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki.

“Alidai anaitwa David Kagasheki, Katibu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, ambaye amejumuishwa kwenye tume hii ambayo ina kazi ya kuchunguza tuhuma mbalimbali za wizara hii.

“Aliwaambia wafanyakazi wa NCCA, kuwa atakuwapo Ngorongoro hadi Agosti 29, mwaka huu na siku ambayo ingefuata angekuwa Ngorongoro kwa ajili ya uchunguzi.

“Inadaiwa katika mazungumzo hayo, alimwambia mfanyakazi mmoja aandae Sh milioni 10, wakati mwingine aliambiwa aandae Sh milioni 6, ili mambo yao yawe safi,” alisema Kamanda Sabas.

Baada ya Jeshi la Polisi kupata taarifa hizo, liliweka mtego na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa akiwa eneo walilokubaliana kukutana.

Kwa upande wake, Katibu wa CHADEMA, Mkoa wa Arusha, Amani Golugwa, akizungumzia tukio hilo, alikiri kiongozi huyo kukamatwa.

“Kweli kiongozi wetu amekamatwa, tunafanya utaratibu wa kumpata wakili atakayetusaidia na kujua ukweli wa tukio hili, ila ninachoweza kusema kwa kifupi ni kwamba taratibu zote zimekamilika,” alisema Golugwa.

Alisema anasikitishwa na taarifa ya polisi kwani namba ya simu ya kiongozi huyo, inayodaiwa kutumika si ya kweli.

“Paul alifika Mjini Arusha kwa ajili ya kulipia ada za shule za watoto wake, ndipo akapokea simu ya mtu asiyemfahamu ambaye alimtaka wakutane Hoteli ya Kibo Palace na kwa kuwa alitambua hana kosa, alilazimika kwenda.

“Alipofika pale, aliona watu wakimuuliza wewe ndiye fulani?, wakampatia begi kushika, baada ya kukataa akajikuta akikamatwa kwa nguvu na kunyang’anywa simu zake na baada ya kunyang’anywa simu zake, aliwekewa laini ya simu ambayo imesajiliwa kwa jina la David Kagasheki,” alisema Golugwa.

[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]
 
Hizo ni mbinu za magamba100%.lakini ninaamini ukweli utashinda.
Kwani huyo katibu wa maliasili na utalii anaitwa kagasheki???? Kazi kwelikweli.
 
Back
Top Bottom