Katibu Mkuu wa Baraza la Vijana CHADEMA Dua Lyamzito amesema uwepo wa Chama cha Mapinduzi madarakani unaendelea kuwafanya wantanzania kuwa maskini hali yakuwa wao(CCM) wanakua na maisha mazuri.
Akizungumza akiwa Kibanga, Muleba mkoani Kagera Dua amesema “kwetu Karambi nikienda miaka mitano nikirudi napakuta vilevile unadhani hii ni kwa sababu ya Mungu, Mungu ndiye anaamua mtu mmoja anaweza akala chakula akatupa na mwingine akakosa vile vile? kuna watu wanaitwa CCM wako ofisini wamesababisha sisi tule au tufe njaa”
Dua ameongeza kuwa ni maamuzi ya wananchi kuendelea kuiamini CCM na waendelee kuishi maisha magumu ya kushindwa hata kupata mlo au kuitoa madarakani ili waweze kumudu maisha yao na hata kukidhi mahitaji yao ya msingi kama chakula.
Unashangaa kupakuta vilevile kwani wewe umefanya nini kupaendeleza? Mie nakaa Mwanza, lakini nyumbani Kiziba nimejenga na mdogo wangu nimemwekea ka biashara. Wewe hujafanya chochote halafu unalalamika eti hapajabadilika! PUMBAVU!!
Unashangaa kupakuta vilevile kwani wewe umefanya nini kupaendeleza? Mie nakaa Mwanza, lakini nyumbani Kiziba nimejenga na mdogo wangu nimemwekea ka biashara. Wewe hujafanya chochote halafu unalalamika eti hapajabadilika! PUMBAVU!!