Katibu Mkuu Utumishi pitia waraka wa utumishi wa umma na.2 wa mwaka 2018 kipengele na 3.2 (I) kinanyima haki watumishi

Katibu Mkuu Utumishi pitia waraka wa utumishi wa umma na.2 wa mwaka 2018 kipengele na 3.2 (I) kinanyima haki watumishi

Nazi embe

Senior Member
Joined
Sep 20, 2016
Posts
105
Reaction score
123
Majuzi niliomba kuona waraka huu hapa hapa jamvini kwa bahati nzuri mdau mmoja kanitumia PM hapa nimeona kipengele cha 3.2.(i) si rafiki kwani kinamnyima stahiki zake mtumishi endapo mwajiri hatukuwa na busara kipengele kinasema

(I)malipo ya uhamisho hasa katika maeneo ya mjini yafanyike baada ya mwajiri kujiridhisha pasipo shaka yoyote kuwa uhamisho wa mtumishi husika unamlazimu kuhama makazi hivyo katika kushughulikia uhamisho wa namna hii mwajiri azingatie mazingira halisi ya kila eneo.

Hapa neno mjini ni utata mjini wapi sasa kwenye magari mengi na nyumba za umeme, maduka makubwa makubwa, au senta ambapo watu wanakusanyikia

MY TAKE
Hichi kipengele ni tata kitaumiza watu wengi sana ushauri kifutwe au kitolewe ufafanuzi hilo neno mjini

Mfano unamwamisha mtumishi kutoka mbagala unampeleka goba uko arafu mwajiri anasema uhamisho wako sio wa malipo kwa sababu amejiridhisha upo mjini 😂😂😂😂 ona umbali huo maana si upon mjini hajathiri makazi yako anakutwanga na kifungu hicho si maumivuivu
 
I wish ningekuwa boss ningewanyoosha na hicho kifungu nikimtaka mkeo tu nakupeleka uko si mjini bwana hakuna malipo nakuhamisha tu
 
Mbona kipo clear, ukihamishwa kutoka wilaya ya ubungo kwenda kinondoni umehama wilaya Ila Kama unakaa Sinza huhitaji kuhama makazi. Maana yake unaweza kwenda kufanya kazi sehemu mpya pasipo kuhama makazi.
 
Mbona kipo clear, ukihamishwa kutoka wilaya ya ubungo kwenda kinondoni umehama wilaya Ila Kama unakaa Sinza huhitaji kuhama makazi. Maana yake unaweza kwenda kufanya kazi sehemu mpya pasipo kuhama makazi.

Ikiwa unahamishwa toka Bunju kwenda Mbagala je? Utakuwa unaishi Bunju na kwenda kutibu au kufundisha wanafunzi Mbagala?
 
Ikiwa unahamishwa toka Bunju kwenda Mbagala je? Utakuwa unaishi Bunju na kwenda kutibu au kufundisha wanafunzi Mbagala?
Ndio maana ukisoma hicho kipemgele kinasema Kama kitamlazimu mhamaji kuhamisha makazi.

Mfano Upo Bunju unahamia kerege pamoja unahama mkoa lakini mjini na address ya makazi haibadiliki

Ila unahama kerege unaenda chalinze lazima ulipwe. Ni hayo tu.
 
Back
Top Bottom