Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,761
- 216,011
Umoja wa Mataifa watoa wito kwa viongozi wa kisiasa na wafuasi wao kujiepusha na visa vya vurugu nchini Tanzania
Umoja wa Mataifa umetoa wito kwa Tanzania kuhakikisha uchaguzi mkuu wa Oktoba 28 unafanyika kwa njia ya amani.
Katika taarifa siku ya Jumatatu iliyotolewa kwa niaba ya Bw. Antonio Gutteres inasema mchakato shirikishi wa uchaguzi na ushiriki mpana wa vyama vya siasa na wagombea wao, haswa wanawake, unabaki muhimu kwa kulinda maendeleo yaliyofanywa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuimarisha utulivu, demokrasia na maendeleo endelevu.
Katibu mkuu wa Umoja huo pia ametoa wito kwa viongozi wa kisiasa na wafuasi wao kushiriki katika uchaguzi huo kwa amani na kujiepusha na visa vya vurugu.
Mamlaka pia imetakiwa kutoa mazingira salama ambayo yatawawezesha Watanzania kutekeleza haki yao ya kiraia na kisiasa.
Umoja wa Mataifa umetoa wito kwa Tanzania kuhakikisha uchaguzi mkuu wa Oktoba 28 unafanyika kwa njia ya amani.
Katika taarifa siku ya Jumatatu iliyotolewa kwa niaba ya Bw. Antonio Gutteres inasema mchakato shirikishi wa uchaguzi na ushiriki mpana wa vyama vya siasa na wagombea wao, haswa wanawake, unabaki muhimu kwa kulinda maendeleo yaliyofanywa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuimarisha utulivu, demokrasia na maendeleo endelevu.
Katibu mkuu wa Umoja huo pia ametoa wito kwa viongozi wa kisiasa na wafuasi wao kushiriki katika uchaguzi huo kwa amani na kujiepusha na visa vya vurugu.
Mamlaka pia imetakiwa kutoa mazingira salama ambayo yatawawezesha Watanzania kutekeleza haki yao ya kiraia na kisiasa.