LGE2024 Katibu mwenezi Arusha: Wao wanaokoteza wagombea, CCM ina demokrasia

LGE2024 Katibu mwenezi Arusha: Wao wanaokoteza wagombea, CCM ina demokrasia

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Arusha, Antony Maswi amewaasa wagombea wa nafasi ya uenyekiti wa vijiji/mitaa na vitongoji kuzingatia demokrasia na kutumia lugha za staha wakati wakiendelea na kampeni zao.

Soma: Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Amesema hayo Novemba 21, 2024 wakati wa uzinduzi wa kampeni katika mtaa wa Murieti kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu.

Ameongeza kuwa CCM ni chama kilichojipanga vizuri kuanzia zoezi la uandikishaji, uteuzi wa wagombea na mpaka sasa zoezi la kampeni linapoendelea na ameeleza kuwa huwezi ukawalinganisha CCM na vyama vingine ambavyo vinaokoteza okoteza wagombea.
 
Back
Top Bottom