Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu amesema walimu ndio kada ya watumishi wa umma wanaolipwa mishahara mikubwa kuliko kada nyingine yoyote.
Naibu Katibu Mkuu amesisitiza kuwa walimu wanalipwa mishahara mikubwa sana nchi hii kuliko kada nyingine zote.
Naibu waziri ameyasema hayo kwenye kipindi cha televisheni cha chanel ten.
========
MOSES CHITAMA: Tumekuwa tukipata waajiri ambao ni wakurugenzi kwa mujibu wa sheria ilivyo, mkurugenzi analeta mashtaka kwamba mwalimu huyu amebainika na makosa haya. Tunaanzisha taratibu za kumchukulia hatua za kinidhamu.
Mwalimu anapewa barua ya shtaka ajieleze ambae anaundiwa kamati za uchunguzi kuchunguza shauri lake, Je ni kweli alifanya hayo makosa? Ni kweli alikuwa amelewa? Ni kweli alitukana? Ni kweli alipigana na mwalimu mwenzie eneo la kazi? Ni kweli mwalimu ni mtoro? Ni kweli mwalimu alikuwa anafanya mapenzi na mwanafunzi?
Ibainike, ithibitike pasipo shaka ni kweli mwalimu alikuwa anafanya mapenzi na mtoto wa shule, ikishabainika sasa hatua za kinidhamu zinachukuliwa. Mwalimu anaweza akafukuzwa kazi na kama alikuwa mtoro, mwalimu mwengine unakuta ametoroka mwaka mzima hayupo kumbe anafundisha private, huku anafundisha private huku anachukua mshahara wa serikali.
MWANDISHI: Kwanini huyu anatafuta kazi ya ziada, inawezekana kipato anachokipata mwalimu huyu ni kidogo?
MOSES CHITAMA: Kati ya walimu ambao wana maslahi mazuri, ambao wanapewa kipaumbele na serikali ni walimu. Mishahara yao mikubwa ya walimu, yaani ukimaliza degree yako unapata mshahara mkubwa kuliko mtumishi mwingine anaeanza, anaemaliza degree yake anaenda kwenye fani zingine. Mwalimu mshahara wake ni mkubwa, sitaki kukwambia hapa ni shilingi ngapi lakini huo ndio ukweli.
... 90% ya GDP ya Tanzania inachangiwa na 3% ya wenye kipato cha kati na matajiri. 97% ya wananchi mchango wao kwenye GDP ni 10%! Ndicho alichomaanisha huyo Mh. ama kwa kutokujua au kwa makusudi mazima - kama ilivyo ada dharau za CCM kwa wananchi baada ya chaguzi wakiwatimulia vumbi na ma-VX-V8 wanayonunuliwa kwa kodi za wanyonge.
Wapunguziwe mishahara maana wamezidi kujipendekeza kwa CCM.
Samahani mke wangu hawa walimu wenzio wamezidi, kama yule wa kule kwenye semina elekezi ya kusimamia mitihani(NECTA) aliyewaambia kwamba walimu mmeshinda uchuguzi.
... 90% ya GDP ya Tanzania inachangiwa na 3% ya wenye kipato cha kati na matajiri. 97% ya wananchi mchango wao kwenye GDP ni 10%! Ndicho alichomaanisha huyo Mh. ama kwa kutokujua au kwa makusudi mazima - kama ilivyo ada dharau za CCM kwa wananchi baada ya chaguzi wakiwatimulia vumbi na ma-VX-V8 wanayonunuliwa kwa kodi za wanyonge.
Mtasaidia sana kutoa tafsiri ya wakuu wetu. Sijui kwa vile wabovu wa lugha ya kiswahili au kulikoni?
Maana ni mpaka wapate msaada wa wanajf, vinginevyo hawaeleweki. Tutakuwa na wakalimani wangapi wa lugha ya kiswahili. Du, poleni sana, Msijali Ndungai atawabeba tu na kuwaelewa hata kama watanzania hawawelewi.