Katika ajali Ile dereva alijua soon kifo kinatuvaa

Katika ajali Ile dereva alijua soon kifo kinatuvaa

Buffet

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2018
Posts
639
Reaction score
1,571
Tarehe 16 September 2016 nilisafiri na Basi la Newforce toka Dar to Songea, Safari ilikuwa nzuri sana toka tunaondoka Ubungo, nakumbuka nilikaa seat no A2, A1 alikaa rafiki yangu ambaye alikufa dakika chache baada ya ajali kutokea

Basi hili halikuwa na tatizo lolote maana toka Dsm halikupoteza hata dakika likifanyiwa matengenezo njiani, Sasa mida ya saa mbili tukiwa sehemu ya Kifanya Njombe gari lilimzidi dereva kutokana na kona halafu mteremko, kwa kuwa tulikaa siti ya mbele kabisa dereva alisikika akimwambia conductor wake Cassian huu msala, sitaweza kulirudisha Tena, wakati huo Basi linayumba mwendo mkali na watu wanapiga kelele, kumbuka haya yote ni ndani ya dakika moja tu kishindo kikubwa kikasikika na abiria wote tukajikuta badala ya kukaa tukajikuta tumelala kiubavu ndani ya Basi, wengine wanalia, wengine wamekufa, wengine damu zinawavujia bila kujua zinatoka kwny jeraha la nani

Ajali naifananisha na ambushi, huwezi ukajiandaa kuikabili, rafiki yangu alikufa miongoni mwa 19 waliokufa, ila bado nakumbuka na kumpenda minza wangu kipenzi

RIP minza
 
Unahisi dereva alikua na sifa zipi hapo kati hizi

 
Picha
2059248889.jpg
788921479.jpg
 
Ilitokea Kifanya sehemu gani!?
Au ndio hii ajali iliyotokea Mlima Lukumburu!?
 
B
We jamaa yaonesha hujawahi move on tokea hilo swala litokee.

Maisha yetu ni dakika yoyote yanatoweka
Bro,Kuna mm inawezekana hili Jambo nimeshindwa kabisa kulizoea,kulisahau and then kumove on,tokea siku hiyo niliamin Allah kaniumbia dunia yangu tu,hiyo ajali haikuishia kunijeruh physically tu, ilijeruhi had sehem ya mustakabali wangu,ilichukua maisha ya alokuwa mke wangu mtarajiwa
 
Labda utuambie wewe uliweza vipi kutoka salama ingali mpenzi wako alifariki dunia pale pale,je ulifunga mkanda yeye hakufunga? au Mungu tu.?
 
Labda utuambie wewe uliweza vipi kutoka salama ingali mpenzi wako alifariki dunia pale pale,je ulifunga mkanda yeye hakufunga? au Mungu tu.?

Labda utuambie wewe uliweza vipi kutoka salama ingali mpenzi wako alifariki dunia pale pale,je ulifunga mkanda yeye hakufunga? au Mungu tu.?
Hujawah kusikia ajali imetokea halaf wakafariki baadhi na wengine wakatoka bila hata jeraha au m hubuko??pata ajali nawewe halaf ikitoka salama utakuwa na jibu kamili la umetokaje salama na wenzio wamekufa
 
Hujawah kusikia ajali imetokea halaf wakafariki baadhi na wengine wakatoka bila hata jeraha au m hubuko??pata ajali nawewe halaf ikitoka salama utakuwa na jibu kamili la umetokaje salama na wenzio wamekufa
Jibu swali
Au bado umevurugwa na ajali
 
Back
Top Bottom