#COVID19 Katika hili la Covid-19, nimejifunza sisi Watanzania ni wakushikiliwa akili

Typing error sio shida shida ni pale viongozi wa juu wakikanusha hakuna korona tz na hidi wengine wakidiriki kupita hospitalini na kutuambia wamekuta watu wenye mimba tu sasa sijui mzee kijazi alikuwa wapi wakati wanapita
Labda waliona kitambi, kwa wenge walilo nalo wakafikiri ni mimba
 
Watu wapo bize kutafuta taarifa za wafu wapost maana naona imekuwa sifa sasa kuwa wa kwanza kupost kifo cha kigogo. Corons ipo tuchukue tahadhari sio hadi tutangaziwe na JPM

lakin ye ni kiongozi wa nchi why is he living in denial ? whats wrong with admitting that corona is there and people should take precautions ?
 
Hao wanaolalamika ni siasa tu na ndio hao hata mwaka jana walikuwa wanasema kwamba Tz watu hufa kimya kimya kwa corona na maneno mengine mengi tu ila uchaguzi ulipokaribia wakaacha kuongea hayo mambo wakajielekeza na kampeni ambazo hazikuwa na tahadhari zozote,hakuna huku uraiani ambaye anasubiri serikali imwambie achukue tahadhari na ndio maana pamoja na kwamba serikali haijasema wazi kuwa kuna corona ila kuna watu wengi tu wanachukua tahadhari na wengine hawachukui tahadhari kwa uamuzi wao na si kwa sababu wanasubiri serikali iseme.
 
Watu wapo bize kutafuta taarifa za wafu wapost maana naona imekuwa sifa sasa kuwa wa kwanza kupost kifo cha kigogo. Corons ipo tuchukue tahadhari sio hadi tutangaziwe na JPM
Mkuu swali dogo tu, je wadau wanaposema serikali itangaze huwa wew unaelewa nini au malengo yao huwa ni nini?
 
Kwa kweli tunaitaji katiba mpya isiyo mpa raisi madaraka ya kupitiliza kama ilivyo sasa, yaani raisi anatamka hakuna corona wakati ipo, chanjo zisije wakati tatizo lipo, hapana kiwepo kifungu cha kumshugulikia pale anapo kengeuka!!
 
We need coordinated efforts za kujikinga ili kupata matokeo yaliyo kusudiwa, inahitaji mamlaka kumfanya kila mtu azingatie taratibu zitakazo wekwa.

Mgonjwa wa Covd 19 akipelekwa hospital wanamkataa... Wagonjwa wa Covd 19 wanahudumiwa majumbani...
Na wanao kufa kwa Covd 19 wanazikwa pasipo kuzingatia tahadhari...

Hali Ni mbaya na inatisha.
 
Unaijua vizuri kazi na wajibu wa Rais katika ku address majanga ya kitaifa? Unajua umuhimu wa mwananchi kupewa taarifa zilizo sahihi kutoka katika mamlaka sahihi?
Hata hivyo sabato ili iwe njema Ni lazima tujifunze kuwajali na kuwathamini wengine.
 
Ni kweli tunapaswa kujiongeza kama wananchi ila haiondoi ulazima wa rais na wateule wake kutoa muongozo kwa taifa. Ni jukumu lao 100%
unataka muongozo gani.

huoni gwajima anavyohangaika kuelekeza watu namna ya kuzima dalili za covid!!!

suala la wewe kuvaa barakoa halihutaji uje uambiwe na profesa, au mkurugenzi. ni la kwako binafsi.
 
Mi nawashangaa watu San..! Kam mnajidanganya kuvaa barakoa ndo unajikinga Basi US watu wasingekufa kama kuku kwa mazingira ya nchi yetu kuvaa barakoa haisadii peke yake...!
Walewale, sijui nani huwa anawazaa viumbe kama nyie
 
Nilipoona tu kichwa cha habari kina maneno wakushikiriwa akiri, moja kwa moja nikajua kilichoko ndani kwenye bandiko ni uchafu.
sababu tu sio ujumbe wa kukashifu.

mna tabu sana nyinyi nyumbu.
 
Pengine usichokijua ni kikubwa zaidi ya ulichoandika. Nobody is interested in your lame duck president but rather a public concern for government lack of leadership to the effect.

Wewe hukusikia Mambosasa anatangaza kwenda kuwachunguza na kisha kuwafungulia mashitaka Agakhan Hospital? Eti Kwa sababu wanatoza gharama kubwa Kwa wagonjwa wa COVID 19? Kama COVID 19 ni janga la kimataifa/kitaifa polisi tena ngazi ya mkoa, inawezaje kutoa amri ya aina hiyo? Maana yake ni kuwa hakuna government leadership to the effect. Na hiyo ndio hoja ya Watanzania. Nevertheless you can still love your lame duck president.
 
Unataka muongozo gani.

Huoni gwajima anavyohangaika kuelekeza watu namna ya kuzima dalili za covid!!!

Suala la wewe kuvaa barakoa halihutaji uje uambiwe na profesa, au mkurugenzi. ni la kwako binafsi.
Ndio maana ya kuwa na kiongozi katika jamii si kwamba watu hawajui nini cha kufanya ila kiongozi anachofanya ni kuleta muunganiko wa maamuzi yanayohusu jamii husika.
 
Ndio maana ya kua na kiongozi katika jamii si kwamba watu hawajui nini cha kufanya ila kiongozi anachofanya ni kuleta muunganiko wa maamuzi yanayohusu jamii husika.
alichobakiza rais ni kutangaza lockdown,ili watu waanze makelele anawaua kwa njaa.

kila kitu keshasema kamaliza.
 
Hizo ndiyo akili za kushikiwa
Ukiwa unajisaidia chooni wakati jamii inayokuzunguka inakunya hovyo mahali popote tambuwa kuwa na wewe utakula/ kunywa/kugusana na mavi ya wenzio bila kuangalia kuwa wewe unatumia choo. Unatakiwa uwajibikaji wa pamoja. Mamlaka ziwalazimishe watu kufanya wasiyotaka kuyafanya ndiyo maana ya tamko la serekali.
 
wewe nae sio muelewa, sio kwamba hatujui kama corona ipo, tunataka Raisi aaibike kwa kuonyesha udhaifu wa kutangaza hali ya hatari. Raisi amekua kinara wa kuwatoa watu hofu, sisi tunataka awatie watu hofu, ndo tunachotaka. Sio kwamba hatujui Covid haipo.
 
Umeandika pumba tupu,halafu unamalizia na "sabato".
Au wewe ni mtoto wa jiwe?
 
Bongo akili zetu kama panzi
 
Hivi unadhani mamilioni ya Watanzania wanajua kinachoendelea?
Tunaojua kuwa corona inakoronoa Watanzania tuko wachache.
Siku moja Rais akikili kwa kinywa chake kuwa mdudu yupo nao viongozi na wanahabari watawafungua akili watanganyika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…