#COVID19 Katika hili la Covid-19, nimejifunza sisi Watanzania ni wakushikiliwa akili

Waziri wa Afya na naibu wake waliita wanahabari wakawasihi watu wajikinge, wakaonyesha jinsi ya kunawa na kujifukiza, wakanywa dawa, watu wakamkejeli. Akawaonyesha yeye na mumewe wanavyojikinga, watu wakamkejeli mumewe kuwa kaolewa, wziri anapenda kiki. Waziri ni msaidizi wa raisi. Raisi hawezi kufanya na kusema kila kitu, ndo maana anawasaidizi. Hawa ndo watanzania. Wajuaji wasiojua kufikiri wenyewe.
 
Huku sio kuchemka bali kutokota!!!!
Mwaka jana Rais alisimamia mapambano dhidi ya Covid 19 na tulishinda.Kwanza alikiri kuwa ugonjwa upo,pili pakawa na mkakati wa serikali wa kuweka vituo vya matibabu na tatu palikuwa na kamati maalum ya kufuatilia.
Hakuna anayehitaji lockdown lakini kauli ya Rais ya kusema "ugonjwa upo na taratibu zifuatwe"inatosha kabisa kubadili upepo wa mapambano.
Kinachofanyika sasa ni kuwa hakuna anayekiri kuwa ugonjwa upo na hii inafanya hata jitihada za kujikinga kutopewa uzito unaostahili.
Kwani kuna kigugumizi gani mpaka tunaanza kuulizana kama kweli "tunamwamini Mungu"?
La mwisho Rais ajiamini kuwa anaaminiwa na watanzania wengi na aitumie hiyo fursa kuokoa maisha ya watu
 
Unaweza kufikiri una akili kumbe akili zenyewe huna. Ungejua kwa nini tuna viongozi labda ungebadili bandiko lako. Mungu atulinde sote.
 
Wajinga kama nyinyi ndio mnaofanya corona izidi kusambaa mitaani huku watu wanakufa lakini hakuna tahadhari yoyote watanzania kwa kiasi kikubwa hawana elimu
 
Jamii iliyo kimya unaweza ukawa kimya kwa kupenda mwenyewe ama kwa kunyamazishwa 'a silent society is a hindrance to business success'
 
Hizo akili zenyewe za kushikiwa mnazo ?
 
Nafikiri kuna mahali hujaelewa LOGIC ya wanao itaka serikali itamke kuwa COVID -19 ipo. Ukweli ni kwamba bila serikali kutamka na kuutangazia umma mbinu za kufuata ili kupambana na COVID-19 basi tutegemee maafa makubwa.

Juzi nilikuwa Morogoro mjini, ni watu wachache sana wanavaa barakoa. Maduka machache sana kuna maji tiririka na vitakasa mikono. Hakuna hata daladala moja ina sanitizer kwaajili ya abiria wake!! Sokoni hakuna tahadhari za kiafya ziliwekwa! Kwa ujumla watu hawa chukui tahadhari kabisa.

Logic inakuja hapa ; ukiingia kwenye daladala na usikute sanitizer huwezi kumuuliza konda kwanini hajaweka? Kwasababu serikali haijasisitiza kulazimisha kuweka huduma hizo. Kifupi bila serikali kuweka mkakati wa kisayansi na kufuatilia, ugonjwa huu utatuangamiza wengi.
Maombi sawa lakini Mungu anawapenda watu wanao tumia akili. Serikali ikiweka mkakati ina kuwa ni rahisi kwetu kuhoji kwanini hujaweka sanitizer? Kwanini umejaza abiria kupita uwezo? Kwanini hujaweka maji tiririka na vitakasa mikono dukani kwako? Kazi inakuwa nyepesi.
 
Huna lolote sabato watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa haya ni maneno ya M/Mungu baba mwenye nyumba ukifeli familia inaangamia
 
unataka muongozo gani.

huoni gwajima anavyohangaika kuelekeza watu namna ya kuzima dalili za covid!!!

suala la wewe kuvaa barakoa halihutaji uje uambiwe na profesa, au mkurugenzi. ni la kwako binafsi.
Covid ni zaidi ya barakoa, serikari kuamuru hata kwenye usafiri watu wakae level seat kama ilivyokuwa mwaka jana na kuruhusu magari mengine kuingia mjini. Hili haliwezi kukamilika bila kusimamiwa ipasavyo. Maana hata wenye magari ya wanatafuta pesa.

Kwenye mahospitali mwaka jana kuliamriwa kuwe na sehemu maalumu za isolation na serikali ilikuwa ikipita kwenye vituo husika kutoa support lkn kwa sasa wagonjwa wenye hii changamoto wanalazwa mawodini na wagonjwa wengine matokeo yake mtu amelazwa kwa malaria anakuja kupata covid kwa uzembe tu wa mtu mmoja kuficha mambo.


Bila kauli ya viongozi ndio zinaweza kufanya jamii iwe salama ikiwa hata kupunguza idadi ya maambukizi.
 
Unachobisha nini mkuu, Mwenyekiti amesema Corona ilishashindwa na haipo. Mpaka sasa hajatoa tamko lolote kama kiongozi mkuu wa nchi. Viongozi wote wa serikali hakuna anayevaa barakoa, unataka tusimlaumu kwa nini?
 
Hivi kuna mtanzania ambaye kapoteza ndg zake kabisa atakuja na visentensi vya kupinga umhimu wa serikali kuwa wazi juu ya covid 19, ikiwa ni pamoja na kuja na mikakati mahususi ya kupambana na hili janga?
 
umesahau kuweka namba ya simu mkuu kwajili ya uteuzi
 
The good thing about these lies is that internet never forgets the TRUTH.

 
Jamaa ni muongo wa kupitiliza. Sasa anataka kutudanganya eti siku ina masaa 48! πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

 


Alishasema ipo, lakini hakutumia lugha sahihi kwa wananchi wengi kuelewa.

Ni hivi jina la kisayansi ni SARS-CoV-2.

Inamaanisha Severe Acute Respiratory Syndrome. Kifupi ni Changamoto kubwa za kupumua zinazosabishwa na kirusi cha korona cha pili.

WHO wakasema wananchi/ Dunia hawataelewa kwa hiyo tufupishe tuuite. Covid -19, au Corona Virus. That's what happened.
 
Mgonjwa wa Covd 19 akipelekwa hospital wanamkataa... Wagonjwa wa Covd 19 wanahudumiwa majumbani...
Na wanao kufa kwa Covd 19 wanazikwa pasipo kuzingatia tahadhari...

Hali Ni mbaya na inatisha.

Hapahapa wanajuaje ni mgonjwa wa Covid?
 
Good message.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…