Katika hili Wakristo tumepotoka

Jokajeusi

JF-Expert Member
Joined
Jun 1, 2018
Posts
6,323
Reaction score
10,813
Habari wakuu!!

Mimi ni Mkristo. Tena si yule Mkristo wa kufuata miujiza au wa kufuata mkumbo. Ni mkristo ninayefuata misingi ya maandiko matakatifu kama yanavyosema bila kujali ni nini naamini au nani anaamini. maandiko matakatifu ndio msingi wa maisha ya binadamu wawapo hapa duniani. Kufuata maoni ya watu ni moja ya ukengeufu wa watu wengi hasa sisi Wakristo.

"YESU SIO MUNGU NA HAJAWAHI KUWA MUNGU, NA HATAWAHI KUWA MUNGU"

Wakristo wamejikuta wakivunja moja ya sheria za Mungu bila ya wao kujijua. Moja ya sheria za Mungu ni kutokuiabudu miungu mbinguni bila kujali inaishi wapi na inauwezo kiasi gani. Ngoja ninukuu:
Kutoka 20:
3 Usiwe na miungu mingine ila mimi.
4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.

Maandiko hayo yanatutaka tusiabudu miungu mingine. Wakristo tumejikuta tukiingia katika mtego bila kujijua. Wengi wanamhusisha Yesu na Mungu. Wengi wanamuabudu na kumtumikia iwe kwa kujua au la. Lakini ukweli ni kuwa wanavunja sheria hii kubwa ya Mungu. Sababu kubwa ya wao kumuita Yesu ni Mungu bado haipo dhahiri zaidi ya mahaba na imani iliyokosa akili na elimu ya dini. Yesu hawezi kuwa Mungu eti kwa sababu alikufa akafufuka, Alizaliwa bila mbegu ya baba, eti kisa alifufua wafua, kisa alitembea juu ya maji. Nasema hakuna kigezo kinachomfanya Yesu kuwa Mungu.

Yesu ni kiumbe kama walivyoviumbe wengine. Uwezo wake haumfanyi kuwa Mungu. Hata Musa kutenganisha bahari haikumfanya aitwe Mungu. Uwezo wa mtu, akili ya mtu na sifa zinginezo alizonazo mtu hazimfanyi kuwa Mungu. Bali zinamfanya awe mkuu kwa watu au viumbe husika.

Jukumu alilopewa Yesu ni kuitiisha Dunia kwa kurejesha utawala wa Mungu Duniani. Hata hivyo jukumu alilopewa Yesu kama kiumbe chenye heshima katika falme za kiroho ni kuiangusha mamlaka ya Shetani, kumkabili adui Mauti ambaye ndiye adui wa mwisho baada ya lucifa kuwekwa chini ya ulinzi. Na hilo ndilo jukumu la Yesu kuja kuukomboa ulimwengu kutoka katika maadui wawili yaani Shetani ambaye humtumikia Mauti. Hivyo ni kusema Mauti ndiye adui Mkuu ambaye shetani humtumikia.

Zingatia maneno niliyoyakoleza
Soma 1Wakorintho 15:
24 Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu.
25 Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.
26 Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.
27 Kwa kuwa, Alivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake. Lakini atakaposema, Vyote vimetiishwa, ni dhahiri ya kuwa yeye aliyemtiishia vitu vyote hayumo.
28 Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo Mwana mwenyewe naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote.

Ndugu zangu Wakristo tuache kuabudu Miungu bila kujijua. Yesu ni kama viumbe wengine. Tunachopaswa ni kumheshimu tuu kama viumbe wengine watakatifu. Hatupaswi kumtumikia Yesu wala kumuabudu isipokuwa Mungu pekee kama Amri za Mungu zisemavyo.

Kama kuna mwenye hoja tafadhali aje na maandiko sio maneno matupu tuu.

Nawasilisha
 
We ni mmoja wapo wa makondoo yanayojiita makristo huku yakiamini Adam alikuwa mzungu au mwarabu.
Mnaamini Yesu ni mzungu.
Mnadanganyika kuwa musa alikuwa mweupe.
Acha nikuambie huu ujinga ulioandika hapa ni afadhali na hao wanaoamini yesu ni Mungu kuliko wewe unayeamini si Mungu lakini ukaamini ni mweupe(mzungu)
 
1.0.Uyahudi na historia ya Mtu mweusi

1.2.Wayahudi weusi na Laana ya kongwa la chuma(Uthibitisho wa Kibiblia)

Na Bro.Justine Kissay

Juma lililopita jahazi letu lilianza safari ya uthibitisho mkuu ya kwamba biashara ya utumwa ya Afrika Magharibi na ile ya Mashariki(Tanganyika na Zanzibar) ilihusisha wayahudi halisi wa kwenye Biblia ambao ni jamii ya watu weusi.Uthibitisho huo tuliupata kwenye kitabu cha kumbukumbu la torati sura ya 28 mstari wa 68 unaosema "BWANA atakurudisha tena Misri kwa Merikebu.Mstari huo unathibitisha dhahiri kwamba wale watumwa kutoka Afrika walikua ni wayahudi halisi kwa sababu katika kipindi chote cha historia ulimwenguni,ni watu weusi pekee ndio waliopelekwa utumwani kwa Merikebu tena wakitokea Afrika.Pamoja na ukweli huo uliozikwa kwa muda mrefu ya kwamba wayahudi halisi ni watu weusi,wapo ambao jambo hili halitapata kibali cha kupenya kwenye fikra zao,wakidhani kwamba huenda ikawa ni mapokeo mapya ama pengine ni hadithi tu ya kusadikika.Lakini hii ni kutokana na mbinu za utawala wa fikra(mind control ) zinazotumiwa na wazungu ule uzao wa Esau kupitia mifumo yao ya elimu waliyoiratibu,ambayo muda wote inaipa ukweli kisogo, huku ikiuacha uwongo ukitamalaki kwenye majoho na kofia za shahada.Naam tumekua mateka wa kudumu wa fikra kwa sababu hata historia yetu(watu weusi) imeandikwa na wahisani.Mwanaharakati nguli wa kutetea haki za watu weusi,Malcom X aliwahi kusema kwamba "Only fools would let their enermies educate their children"akiwa na maana kwamba ni wajinga pekee ndio wataruhusu maadui zao kufundisha watoto wao.Naam huo ndio ukweli wa mambo kwani tumeruhusu wahisani wamwage wino kwenye vitabu vya historia yetu na mbaya zaidi tumeendelea kushiriki kikombe chao cha udhalimu kwa kuendelea kutumia mitaala ya elimu yenye mkono wao..Naam tumejiandalia umauti wa historia yetu kwenye makalabrasha ya vitabu vya historia.Sasa Jahazi letu bado limetia nanga kwenye Kumbukumbu la torati sura 28 ili kuendelea kukomelea msumari wa uthibitisho ya kwamba biashara ya utumwa Afrika iliwahusu wayahudi halisi ambapo mstari wa 48 unasema "kwa hiyo utawatumikia adui zako atakaowaleta Bwana juu yako, kwa njaa, na kwa kiu, na kwa uchi, na kwa uhitaji wa vitu vyote; naye atakuvika kongwa la chuma shingoni mwako, hata atakapokwisha kukuangamiza.Mstari huu unamaanisha nini?Vyema...!Mstari huo ni muendelezo wa laana dhidi ya Wayahudi kwa sababu ya kuvunja agano la Mungu wao,na kuanza kuabudu miungu mingine.Hii ina maana kwamba pamoja na kupelekwa utumwani kwa Merikebu(kumbu.28:68) kama tulivyoona kwenye makala zilizopita,Biblia pia inasema kwamba adui yako (Mzungu na Mwarabu) atakuvika KONGWA LA CHUMA SHINGONI MWAKO.Tunakwenda sambamba?Kati ya wazungu na weusi ni nani haswa laana ya kupekekwa utumwani na Merikebu na pia kufungwa kongwa la chuma shingoni inayemhusu haswa?Ni mtu mweusi ama sivyo?jamani tunakwenda sambamba?Wandugu si kwamba eti najivunia utumwa huo wa wayahudi la hasha,hapa najaribu tu kuthibitisha Kibiblia kwamba wayahudi halisi ni watu weusi. Sasa wapo watakaohoji mbona jambo hili hatukuwahi kufundishwa shule ya Biblia (Bible school)ama shule ya Jumapili(Sunday school).Looh mbona kule Havard University nilipofuzu shahada ya Uzamivu (Phd) nako sikufundishwa?Mwandishi ameyatoa wapi haya? Wandugu,wino huu unaomwagika kwa masononeko kwenye ukurasa huu tabibu wa nyuma ya pazia kila jumapili ni matokeo chanya ya safari ndefu ya utafiti wa kuitafuta ile Kweli,kwa hiyo kua na amani kabisa kwani ninachokupatia hapa ni asali na maziwa halisi kutoka kwenye ile nchi ya ahadi na wala si bidhaa feki zitakazodhuru fikra zako.Pokea tu kwa shingo nyoofu kwani ninacholenga hapa ni kumtoa Mtu mweusi kwenye jela ya utumwa wa fikra, japo wapo ndugu zangu ambao hupenda kubeza na kukebehi kwa lengo la kunivunja moyo bila ya kua na hoja thabiti, nikwambie tu ndugu pinga uwezavyo, beza uwezavyo lakini ninakuhakikishia kamwe hutaweza kupata somo hili kwenye shahada yako unayosomea au uliyosomea iwe ni ya Falsafa ya Udaktari ama Thiolojia ama elimu yeyote ile, kwani mambo haya yamefichwa kwa makusudi maalumu ya kumtawala Mtu mweusi.
Mpendwa msomaji wazungu hawataki kamwe ufahamu ukweli huu kwasababu wameiba haki ya uzaliwa wa kwanza ya imani ya Uyahudi kutoka kwa mtu mweusi na kujivika wao kofia ya Uyahudi wakati wao ni Wazayuni.Kikubwa wanachohofia ni kwamba endapo tu wakikubali ukweli huo ni dhahiri watu wataanza kuhoji uhalali wa dini hizi kongwe walizotuletea na hapo ndipo jicho lao litakapokua matatani kwa sababu mboni itakua imetikiswa.Sasa kama ukiamua kua kwenye kilele cha utulivu wa fikra ni lazima tu utahoji upo wapi wema ama uzuri wa dini zilizopitia mikononi mwa watesi wetu yaani Wazungu na Waarabu.Upo wapi wema wa dini hizi zilizoenezwa kwa upanga mijeledi na bunduki?
Sasa kama tu zilivyo nguvu kuu mbili kinzani yaani Mungu na Shetani ama Nuru na Giza ndivyo ilivyo pia hata kwenye Israel na Uyahudi.Ninanachojaribu kumaanisha hapa ni kwamba kuna Israel ya Mungu na ya Shetani, halikadhalika kuna Wayahudi wa Mungu na Wayahudi wa Shetani. Kazi ya shetani siku zote ni kuharibu mbegu ya Mungu,Mfano tumbo lililomzaa Yakobo,ndilo lililomzaa muovu Esau,Ulipoota mzabibu wa ukweli na mzabibu wa uwongo ukamea, kwenye ngano safi yalikuwepo magugu,Habili alizaliwa na muovu Kaini.jamani tupo pamoja?
Sasa Israel ya kileo ya kina Benjamini Netanyahu imezaliwa ndani ya ardhi ya Palestina mwaka 1948 kwa kutumia mamlaka ya Uingereza(Balfour Declaration ) na Umoja wa Mataifa UN.(tutaona kwa kina huko mbele)
Mwisho wa Israel kama Taifa la Mungu ambao ni watu weusi ulikoma pale majeshi ya Warumi chini ya Generali Vespasian na mwanaye Titus,yalipoivamia Yerusalemu mwaka 70 A.D ambapo wayahudi wa kabila la Yuda(Ufalme wa Kusini) walikimbilia Afrika Magharibi(Negroland) kwa ajili ya kukwepa machafuko na kisha baadae kupelekwa utumwani kwa Merikebu ikiwa ni muendelezo wa laana ya kuvunja maagano ya Mungu wao.
jambo hili limethibitishwa kwenye Luka 21:20-24 pale Yahusha (Yesu) alipowaambia wayahudi wakimbilie milimani (Afrika ) kukwepa majeshi ya Warumi kumbuka hiyo ilikua ni mwaka 70 A.D ambapo mstari wa 24 unasema"Wataanguka kwa ukali wa upanga, nao watatekwa nyara na kuchukuliwa katika mataifa yote; na Yerusalemu utakanyagwa na Mataifa, hata majira ya Mataifa yatakapotimia.Umeelewa hapo? kwamba wakati wayahudi halisi wakiwa utumwani Yerusalemu itakanyagwa na mataifa hata majira ya mataifa yatakapotimia.kwahiyo wale waliopo israeli leo hii ni watu wa mataifa waliojivika kofia ya uyahudi lakini sio.Sikia Mungu anachosema juu ya israel ya shetani.
Ufunuo 2:9 "Naijua dhiki yako na umaskini wako, (lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni Wayahudi, nao sio, bali ni sinagogi la Shetani.jamani tunakwenda pamoja? Kwamba Israel ya kileo ni sinagogi la shetani.Wapendwa wayahudi halisi wa Mungu bado wapo utumwani na watarejea mara baada ya majira ya Mataifa yatakapotimia.sasa ni lini na ni namna gani majira ya mataifa yatatimia tutaona huko mbele kwa kina.Labda niwatoe tu hofu wapendwa wasomaji wa safu hii ni kwamba, jambo hili nimelifanyia utafiti kwa miaka takribani kumi kwa kutumia rejea mbalimbali za Wanazuoni manguli wa Kibiblia, Kiakiolojia, Kianthropolojia, Kibailojia na pia Kihistoria bila kusahau tafiti za wabobezi wa mambo ya kale wa Misri (Egyptologists)Kwahiyo huu ni utafiti uliokamilika katika "angle" zote tena ulioshiba hoja za uzania wa hali ya juu yaani "heavy weight".Aidha nimeamua nikuletee mtiririko huu ili upate kitu tofauti kidogo tofauti na kusoma vitu vile vile visivyokua na msingi wowote ule katika maisha yako.Asikwambie mtu ndugu yangu hakuna jambo zuri kama kuitambua historia yako kwani bila ufahamu wa historia yako ya nyuma, chanzo chake, na utamaduni wake unakua kama mti usiokua na mizizi ( Marcus Garvey — 'A people without the knowledge of their past history, origin and culture is like a tree without roots.'Marcus Garvey alikua ni mwanaharakati wa kusiasa na kada kindakindaki wa harakati za ukombozi wa mtu mwrusi.
Tuendelee kidogo....Sasa chanzo kikuu cha mgogoro wa Israel na Palestina ni uvamizi wa wayahudi feki(sinagogi la shetani) katika ardhi ya Wapalestina.Hivi umekwishawahi kujiuliza, Israeli ya Mungu inaweza kua na hatia ya damu ya Wazee,Wanawake,Vijana,Wamama na watoto wasio na hatia huko palestina, Syria,na Mashariki ya kati yote?.Ifikie mahala tutumie utashi.Na huwezi kupata utashi timilifu kama usipoweka dini pembeni kwa muda kwani zimetufunga mengi hata yale yanayohitaji utashi mdogo tu wa kufikiri.Sasa sisemi kwamba dini ni mbaya hapana nasema si vibaya kuhoji zilipotoka na zililetwa na nani na kwa misingi gani na zina rangi gani.Kuna haja gani sisi watu weusi kuchukiana kwa misingi ya dini tena zilizoletwa na wageni ilihali sisi tu watoto wa Baba mmoja?Je umeanza kumuona mbwa mwitu(Israeli feki) akimtafuna mwanakondoo(israeli halisi)? Naam hao ndio Wazayuni wanaoitawala dunia kupitia Marekani wanaojaribu kutengeneza serikali moja ya dunia kupitia mpango wa New World Order. Kwa hayo machache tuliruhusu jahazi letu litie nanga kwa siku ya leo kwa kuiangalia Matendo 13:1 inayomzungumzia simoni wa Antokia aliyefahamika kwa jina la Nigeri yaani NEGRO.Neno "Nigeri" lilitumika kuwatambua wayahudi likimaanisha mweusi.Mbali na Negro jina lingine lililokua likitumika kuwatambulisha wayahudi ni Hebrews yaani Wahebrania ama HEEBOES.Ndio maana walipofika Afrika Magharibi ardhi yao ilifahamika kama NEGROLAND kwa wayahudi wa Ufalme wa Yuda na East African Negroland kwa wayahudi wa Ufalme wa Kaskazini waliofika kwenye Pwani ya Swahili na Zanj.Majina yote hayo kwa pamoja yalitumika katika masoko ya utumwa ambapo wayahudi hao walipokua wakiuzwa huko Marekani.Jina hilo "Negro" ama "Niger" halikufia kwenye masoko ya utumwa tu ,kwani mpaka leo hii wayahudi walioasi akina Jay Z na Beyonce walioamua kumtumikia lucifer kupitia muziki bado wanaitwa Niger/Negro,na salamu yao maarufu ni what's up Niger.?umeona namna jina la Nigeri lilivyosafiri toka Antokia, Afrika Magharibi mpaka Marekani?Wapendwa hiki ni kipande kidogo tu cha barafu kutoka kwenye mlima wa theluji.Ukitaka kujua habari hii kwa undani kabisa tafadhali jipatie nakala ya kitabu cha Uyahudi na historia ya Mtu mweusi. itaendelea tena kesho....

Habari picha
Myahudi akiwa amefungwa kongwa la chuma shingoni na maadui zake(kumbu 28:48

Mwandishi wa Kitabu ni Mtaalamu wa kilimo, Mtafiti wa historia, Mwanaharakati wa haki za mtu mweusi, na mchambuzi wa siasa za kitaifa na kimataifa.
Simu 0769732635(Piga simu upate utaratibu wa kitabu)
Email justinekissay@gmail.com.

N.B. Kitabu hiki ni sehemu ya kwanza ya safari ya ukombozi wa fikra za mtu mweusi ambapo kitakupa mwangaza wa yale yote uliyofichwa tangu kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu huu.
 
Yesu si Mungu hata yeye mwenyewe anajijua kuwa yeye sio Mungu...ova"
 
Kwani maneno Mungu na Miungu yana maana gani mleta mada?
 
Yesu si Mungu hata yeye mwenyewe anajijua kuwa yeye sio Mungu...ova"
Sio Mungu na sio mzungu na sio mwarabu na ukristo ni uongo wa kaka mkubwa uislam ni uongo wa mdogo wake.
Wote wazungu na waarabu ni uzao wa malaika waasi(yaani watoto shetani alizaa na binadamu yaani binti za watu weusi)
 
Angekuwa kweli Mungu duniani kungekuwa na imani moja tu yaani ukristu usiogawanyika . Huu utitiri wa madhehebu ni ishara tosha kuwa sio Mungu ila tu mtume wa kawaida
 


JE, YESU YU MWANA WA MUNGU ?


Kuna matatizo mengine mengi ya Wakristo kuhusu kumwelewa Yesu asili yake na uhusiano wake na Mungu.

Tukichunguza na kuchambua imani ya Kikristo kinachojitokeza ni kwamba kuna Mwana wa Mungu ambaye anazo sifa za mtu mkamilifu na pia zile za mungu mkamilifu.

Hata hivyo kumbuka ya kwamba sawa na imani ya Kikristo 'Baba' si sawa hasa na 'Mwana'.

Mungu Baba yu Mungu mkamilifu lakini si mtu mkamilifu, ambapo 'Mwana' ni mtu mkamilifu na papo hapo ni mungu mkamilifu
pia.

Ndiyo kusema kwamba hawa wawili ni dhati mbili tofauti walio na sifa mbalimbali.

Ieleweke ya kwamba sifa hizo haziwezi kubadilishwa. Ziko sifa katika baadhi ya vitu ambazo zaweza kubadilishwa.

Kwa mfano, maji yaweza kugeuka kuwa theluji na pia mvuke pasipo kubadilika kitu chenyewe ama asili yake. Lakini tofauti zilizopo katika sifa za Mungu na Kristo, ambapo sifa kadha zinaongezwa kwa mmoja wao, haziwezi kupatanishwa asilani.

Haiwezekani kwa mmoja wao kupata mabadiliko hayo na asipambanuliwe na mwenzake.

Ni tatizo kubwa kabisa ya kwamba Yesu Kristo alikuwa mungu mkamilifu na mtu mkamilifu.

Kama alikuwa na sifa za aina hizo mbili kwa pamoja, bila shaka yeye alikuwa tofauti na Baba ambaye hakuwa mtu kamili wala mtu asiye kamili.

Huo uhusiano ulikuwa wa aina gani?

Je, 'Mwana' alikuwa mkubwa kuliko Baba?

Kama sifa yake hiyo ya ziada haimfanyi 'Mwana' kuwa mkubwa kuliko Baba, hapo bila shaka sifa hiyo ina dosari. Kwa maana
hii 'Mungu Mwana' mwenye kasoro si tu ni kinyume cha madai ya Ukristo bali pia ni kinyume kabisa na Mungu jinsi anavyofahamiwa na watu wote ulimwenguni. Basi mtu anawezaje kuelewa itikadi ya ajabu inayojipinga yenyewe, ambayo inatutaka tuamini kwamba 'Mmoja katika Watatu' na 'Watatu katika Mmoja' ni sawa tu pasipo tofauti yoyote iwayo?

Hiyo inaweza kutokea tu iwapo msingi wa imani hauwekwi juu ya hakika bali unawekwa juu ya mawazo ya kuzushwa.

Isitoshe, kuna tatizo jingine tena linalopaswa kutatuliwa, nalo ni hili: Kama Yesu alikuwa 'Mwana wa Mungu' kwa sababu ya
kuzaliwa kutoka katika tumbo la Mariamu, basi cheo chake kilikuwa kipi hapo kabla?

Na kama yeye alikuwa 'Mwana' siku zote hata bila ya kuzaliwa na Mariamu, ilikuwa haja gani basi, kwamba azaliwe kwa sura ya binadamu?

Na kama ilikuwa lazima, hapo sifa ya kuwa Mwana haikuwa ya milele; bali ilipatikana kama sifa ya nyongeza baada ya yeye kuzaliwa na ikatoweka alipotengana na mwili na kurejea mbinguni.

Hivyo kuna matatizo mengi yazukayo kutokana na itikadi inayokanushwa na akili na busara. Nawaalikeni kukubali jambo lililo na heshima tena la hakika, la kuzaliwa kwa Yesu aliyeumbwa na Mungu kwa kutumia kanuni fulani za asili zilizofichika machoni mwa watu.

Yesu alikuwa mwana wa Mungu kimithali aliyekuwa mpenzi maalum wa Mungu, lakini hata hivyo alikuwa mwanadamu kwa
vyovyote.

Cheo cha kuwa 'Mwana' alipachikwa miaka mia tatu takriban baadaye ili kuendeleza hekaya yake jambo ambalo litajadiliwa baadaye.

Hali ya uhusiano wa ndoa baina ya Mungu Baba na Mariamu ni swala ambalo mtu anachukia kulijadili waziwazi. Hata hivyo
katika jitihada za kuelewa ile kazi ya kati aliyoifanya Mariamu baina 'Baba' na 'Mwana', hilo linakuwa ni uovu usioepukika.
 
Sijaelewa maana Mambo ya Dini umeyafnya kuwa siasa.
 
Sijaelewa maana Mambo ya Dini umeyafnya kuwa siasa.

anza na hii

DHAMBI NA KAFARA

Ningebainisha kwanza ya kwamba Wakristo wote hawaamini neno kwa neno yatakayofuata hapa chini.

Hata baadhi ya viongozi wa Kanisa wamekwenda upande na kuachana na msimamo mgumu wa fundisho la imani la Kanisa.

Hata hivyo falsafa ya 'Dhambi na kafara' ni kanuni ya msingi ya imani ya Kikristo inayokubalika kwa jumla.

Sehemu ya kwanza ya maana ya Dhambi na Kafara ni kwamba Mungu ni mwadilifu na anafanya uadilifu wa dhati. Yeye
hasamehe dhambi pasipo kuadhibu; kwani kusamehe tu dhambi hivi hivi kungekuwa kinyume cha uadilifu halisi.

Sifa hiyo ya Mungu inasababisha kafara ilivyoaminiwa na Wakristo kuwa jambo la lazima.

Sehemu ya pili ni kwamba mtu ni mwenye dhambi kwa sababu Adamu na Hawa walitenda dhambi. Matokeo yake ni kwamba
wazao wao wakaanza kurithi dhambi, kana kwamba hiyo dhambi ikaingizwa katika vijine (genes) vyao na tangu hapo watoto wote
wa Adamu huzaliwa wakiwa wenye dhambi.

Sehemu ya tatu ya itikadi hiyo ni kwamba mwenye dhambi hawezi kutoa kafara ya dhambi ya mwingine: mtu asiye na dhambi pekee ndiye anayeweza kutoa kafara ya dhambi za wengine.

Juu ya msingi huu, inakuwa wazi sawa na ufahamu wa Kikristo, ya kwamba Nabii yeyote wa Mungu hata akiwa mwema namna gani ama akiwa karibu sana na ukamilifu hawezi kumtakasa mtu nakumwondolea dhambi na matokeo yake. Akiwa mwana wa Adamu, asingeweza kuepukana na dhambi aliyorithi alipozaliwa.


Huo ndiyo muhtasari wa muradi wa imani nzima ya kafara.
 
Sijaelewa maana Mambo ya Dini umeyafnya kuwa siasa.


KAFARA KWA MWANADAMU:

Ili kutatua tatizo lisiloweza kutatulika kidhahiri, Mungu akawaza mpango wa akili sana.

Haijulikani kwamba yeye alishauriana na mwana ama hapana; ama wote wawili wakawaza mpango huu wakati mmoja; au uliwazwa na mwana peke yake lakini ikakubaliwa na Mungu Baba.

Maelezo ya mpango huu yalifafanuliwa katika zama za Yesu kama ifuatavyo. Miaka elfu mbili iliyopita 'Mwana wa Mungu' aliyeshirikiana na Mungu katika umilele barabara, alipata kuzaliwa tumboni mwa mama wa kibinadamu.

Akiwa 'Mwana wa Mungu' yeye akajikusanyia ndani yake sifa kamilifu za kibinadamu na pia za Mungu Baba.

Tena tunaambiwa ya kwamba mama mmoja mwema na mtawa, jina lake Mariamu, akachaguliwa kuwa mzazi wa 'Mwana wa
Mungu'

Mama huyo akashika mimba ya Yesu kwa kushirikiana na Mungu. Ndiyo kusema kwamba Yesu akiwa mwana halisi wa Mungu akazaliwa pasipo kuwa na dhambi, hata hivyo akachukua sifa na sura ya binadamu.

Hivyo akajitolea kwa hiari yake kubeba mzigo wote wa madhambi ya wale watu watakaomwamini na
kumkubali kuwa mwokozi wao.

Kwa njia ya mpango huo wa akili, inadaiwa, Mungu akaepa kuhatarisha sifa yake ya uadilifu halisi.

Kumbukeni ya kwamba sawa na mpango huu pia mtu hatasamehewa dhambi pasipo kuadhibiwa. Bado Mungu ataweza
kumwadhibu mwenye dhambi bila ya kuepa sifa yake ya uadilifu.

Tofauti yenyewe ni kwamba sasa Yesu ataadhibiwa, siyo wale wana na mabinti wa Adamu waliotenda dhambi. Hiyo ni fidia ya Yesu itakayosababisha kuwaondolea dhambi watoto wa Adamu.

Mantiki hiyo hata ikionekana ya ajabu na ya kutatanisha , lakini ndivyo ilivyokubaliwa hasa kwamba ilitendeka.

Yesu akajitolea mweyewe na akaadhibiwa kwa ajili ya dhambi ambazo hakuzitenda kabisa
 
Sijaelewa maana Mambo ya Dini umeyafnya kuwa siasa.


DHAMBI YA ADAMU NA HAWA:

Hebu tuchunguze upya kisa cha Adamu tangu mwanzo. Sehemu yoyote ya itikadi hiyo hapo juu haiwezi kukubaliwa na dhamiri
ya mtu na mantiki.

Kwanza, tunaambiwa ya kwamba kwa kuwa Adamu na Hawa walitenda dhambi, basi wazao wao wakachafuliwa kwa kudumu na dhambi waliyorithi wakati wa kuzaliwa.

Lakini kinyume chake, sayansi ya tabia zirithishwazo inabainisha ya kwamba mawazo na matendo ya mtu, yakiwa mazuri ama mabaya , hata mtu akiwa nayo kwa kudumu maisha mazima, hayawezi kuhamishwa katika mfumo wa tabia za kurithishwa katika kuzaana.

Muda wa maisha ya mtu ni mdogo sana kwa kuleta mabadiliko hayo makubwa.

Hata maovu ama mema ya taifa, kizazi baada ya kizazi, hayawezi kuingizwa katika wazao yakiwa ni mienendo ya kurithiwa.

Labda mamilioni ya miaka inahitajika kuingiza sifa mpya katika vijine (genes) vya mtu.

Hata kama mtu angekubali kutukia jambo hilo la ajabu la kutatanisha kwa kapanua mawazo yake ya kipuuzi yasiyokubalika
akilini, basi na angekubali kilicho dhidi yake pia kwa kutumia mantiki kama hiyo.

Hiyo itamaanisha ya kwamba kama mtu mwenye dhambi akitubu na akatakasika mwishoni mwa siku, basi hiyo nayo ingerekodiwa katika mfumo wa sifa zile zinazorithishwa na kufutilia mbali kabisa athari ya dhambi ile ya zamani.

Kisayansi hiyo haiwezi kutendeka, lakini kwa yakini kuna mantiki zaidi katika picha hiyo inayoonesha pande mbili kwa
usawa kuliko kufikiria kwamba maelekeo kwa dhambi tu yanaandikwa katika utaratibu wa sifa za kurithishwa lakini
maelekeo ya mema hayaandikwi.
 
Sijaelewa maana Mambo ya Dini umeyafnya kuwa siasa.

Pili, kwa kujaribu kutatua tatizo la Adamu kwa kutoa shauri ya kuwa dhambi inahamishwa kwa vizazi vijavyo ambavyo vinairithi
tangu kuzaliwa, msingi wenyewe unabomolewa ambao juu yake imani ya 'Dhambi na kafara' imejengwa.

Kama Mungu ndiye mwadilifu halisi, basi upo wapi uadilifu katika kuwahukumu wazao wote wa Adamu na Hawa kwa dhambi yao waliyotenda mara mmoja tu na kisha wakatubu pia?

Kwa vyovyote, hiyo ilikuwa dhambi ambayo waliadhibiwa vikali kwa sababu yake na wakafukuziliwa mbali katika Pepo kwa
fedheha kubwa .

Ni aina gani ya uadilifu ya kwamba baada ya kuwaadhibu Adamu na Hawa sana sana kupita kiasi kwa sababu ya dhambi yao, bado hamaki ya kujilipiza kisasi haijapoa na akawahukumu wanadamu wote wapate fedheha ya kuzaliwa tayari wamerithi dhambi?

Nafasi gani wanayo wazao wa Adamu kuikwepa dhambi?

Kama wazazi wanafanya kosa, kwa nini watoto wao wasiokosea wasumbuke daima kwa sababu ya kosa la wazazi wao?

Kama ni hivyo, basi batilifu iliyoje maana ya uadilifu anayojidaia Mungu na kuifurahia ikiwa Yeye anawaadhibu watu
waliopangiwa kutenda dhambi hata wakichukia dhambi namna gani?

Dhambi ikafanywa sehemu ya maana sana ya maumbile yao. Hamna kabisa sasa nafasi kwa mtoto wa Adamu kubaki
katika hali ya kutokuwa na dhambi. Kama dhambi ndiyo jinai basi ni jinai ya Mwumbaji siyo ya viumbe.

Basi, uadilifu gani ungetaka kuwaadhibu wasiokosea kwa jinai za wengine?
Tangazo la Kurani Tukufu ni tofauti kabisa na ufahamu wa Kikristo wa dhambi na matokeo yake. Kurani Tukufu inatangaza:

Hakuna mbebaji atakayebeba mzigo wa mwingine. (35: 19)
Mungu haikalifishi nafsi yoyote zaidi ya uwezo wake. (2:287)

Tangazo hilo la Kurani kwa kulinganisha na imani ya Kikristo kuhusu Dhambi na Kafara ndiyo taratibu halisi ya kuituliza roho.

Sasa tugeukie maelezo ya Biblia kuhusu yaliyotendeka hasa wakati Adamu na Hawa walipotenda dhambi, na matokeo
yaliyofuata nyuma ya wao kuadhibiwa.

Sawa na mafunzo ya Mwanzo, Mungu alikubali nusu-nusu udhuru wao na wakapewa adhabu ya kudumu milele inavyoelezwa hapa chini:

Wanadamu walikuwapo muda mrefu sana kabla hawajazaliwa Adamu na Hawa. Wanasayansi wa magharibi wenyewe
waligundua mabaki ya watu wengi waliokuwepo ardhini katika zama za kale sana na wakawapa majina mbali mbali ya
kupambanua. Neanderthal - mtu pengine ndiye anayejulikana zaidi miongoni mwa hao.

Wa-Neanderthal waliishi zaidi katika Yoropa,Mashariki ya Karibu na Asia ya Kati, baina miaka 100,000 na 35, 000 mpaka sasa. Maiti ya mtu mkamilifu imenguduliwa ambaye mtu huyo aliishi ardhini miaka 29,000 kabla Adamu na Hawa hawajaanza safari yao fupi huko Peponi.

Katika zama hizo wanadamu kimaumbile walikuwa kama sisi na waliishi katika Yoropa, Afrika na Asia, na baadaye mnamo zama za Theluji (Ice Age) walienea hadi Marekani pia. Vilevile huko Australia historia thabiti ya utamaduni wa Waaborijini (Aborigines) inaonesha ulianza miaka 40,000 iliyopita kutoka leo. Waaborijini ni watu wa asili ya Australia.


Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa uchungu utazaa watoto, na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala. Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nilikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako; michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni; kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo kwa hiyo ulitwaliwa kwa maana u mavumbi wewe nawe mavumbini utarudi (Mwanzo 3:16-19)

Kwa kulinganisha na zama za hivi majuzi, mifupa yote ya mwili ikiwa pamoja, ya mwanamke, imepatikana huko Hedar katika Ethiopia ambayo mifupa hiyo ni ya tangu miaka milioni 2.9. Sasa kwa kulingana na matukio ya historia yalivyoelezwa katika Biblia, Adamu na Hawa waliishi karibu miaka 6,000 tu tangu leo.

Mtu aweza kuangalia nyuma kwa mshangao taarifa ya historia ya wanadamu, ama Homo Sapiens wanavyoitwa katika istilahi
ya Kisayansi
 
Sijaelewa maana Mambo ya Dini umeyafnya kuwa siasa.


KAFARA ILILETA BADILIKO GANI?

Kuhusu matokeo ya Yesu Kristo kusulibishwa tumekwisha hakikisha ya kwamba imani katika Yesu haikupunguza adhabu ya dhambi kwa namna yoyote iliyotolewa na Mungu kwa Adamu na Hawa na wazao wao.

Wanawake wote bado wanazaa kwa uchungu na wanaume bado wanachuma riziki yao kwa jasho la uso wao.

Twaweza kuliangalia jambo hilo kwa jiha nyingine, kwa kulinganisha ulimwengu wa Kikristo na ulimwengu wa wasiokuwa Wakristo kuanzia zama za Yesu Kristo.

Katika kipindi chochote cha historia waumini wa Kikristo hawawezi kuonesha badiliko lolote maalum kwa wanawake wao kwamba wanazaa bila uchungu, wala kwa wanaume wao kwamba wanachuma riziki .

Kuhusu maelekeo ya kutenda dhambi twashuhudia ya kwamba hayo hayakufutika kabisa baina ya waumini wa Kristo kwa athari ya kafara ya Yesu. Aidha, mtu anashangaa kweli kwa nini imani katika Mungu imehesabiwa kuwa hafifu kuliko imani katika
'Mwanawe'.

Hiyo inahusika hasa na zama kabla haijatobolewa siri hii kubwa ya kwamba Mungu anaye Mwana. Naam, walikuwapo watu zamani waliokuwa na imani katika Mungu na Umoja wake.

Vilevile watu wengi wasiohesabika walizaliwa tangu wakati wa Yesu katika dini mbalimbali na nchi mbalimbali hapa ardhini waliomwamini Mungu na Umoja wake.

Mbona imani katika Mungu haikuathiri dhambi za wanadamu na adhabu zao?

Tena kwa nini Mungu Baba hakudhihirisha wema wake na kusumbuka kwa ajili ya wenye dhambi ambao wema huo
ukaoneshwa na 'Mwana' aliyekuwa na daraja dogo kuliko Baba?

Kwa yakini 'Mwana' anaonekana anayo khulka bora zaidi (Mungu apishe mbali) kuliko Baba asiye mstaarabu sana. Je, Uungu
unakua na bado unaendelea kukua ili kufikia ukamilifu wake, mtu aweza kuuliza?
 
afafhali wqtu kama nyie mlikuwepo humu jf, na ifahamike kuwa Mungu ni Mmoja ilayupo katika nafsi tatu, Mungu Baba ambaye ndiye Muumbaji , Mungu Mwana ambaye ndiyeMwokozi ambaye ni yesu na Mungu Roho mtakatifu.
 
Sio Mungu na sio mzungu na sio mwarabu na ukristo ni uongo wa kaka mkubwa uislam ni uongo wa mdogo wake.
Wote wazungu na waarabu ni uzao wa malaika waasi(yaani watoto shetani alizaa na binadamu yaani binti za watu weusi)
sio kweli ova na hakuna malaika waasi ova kasome upya ujue nature ya malaika na jinsi walikuwa na utiifu mbele ya muumba wao utajua mengi kuliko kusoma kitabu kimoja kila siku bora uwe unalala tu. ova
 
MUNGU ALIENIUMBA MIMI HAKUZAA WALA HAKUZALIWA WALA HANA MSAIDIZI KAZI ZAKE ANAFANYA MWENYEWE KWA MAPENZI YAKE simple as water
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…