Katika hili wanawake wanakosea

Katika hili wanawake wanakosea

Hili sio suala dogo la kukurupuka,Inategemea na kipato cha mtu kikoje,kama wewe mwenyewe haujitoshelezi utawezaje kumhudumia mjamzito na akishajifungua na mwanae?Makubaliano yalikuwa ni kufanya kazi.
Na huo mshahara mdogo wa 15 elfu pia inategemea na kipato cha mtu,kuna wengine ni mabaamedi wanalipwa hela ndogo kwa mwezi.

Ndiyo maana nasema tuchukulie mazingira ya tanzania na nchi nyingine maskini ili tuhusishe utu. Hata hao ma-baa medi kama uliyo sema kuna sehemu wanalipwa vyema na wanaishi ki-vyao lakini kuna sehemu zingine wana mshahara mzuri na wanapewa vyumba vya kulala, hii inatokana na roho nzuri ya mwenye biashara.

Wito wa mtoa mada hii kwa jamii ni kwamba akina mama/baba tuwe na moyo wa utu na huruma ktk kuishi na watumishi wetu wa ndani na wanapo kosea tuwashauri/tuwaadhibu kama ndugu zetu/watoto wetu au wadogo zetu.
 
Hii mada ni muhimu sana kwa wanao elewa matatizo yanayo wapata watoto wetu wengi katika jamii yetu. Wito wangu tu kwa akina mama kwenye familia zetu tuwalee hawa watumishi wetu wa ndani kama watoto/wadogo zetu na wanapo kosea basi waadhibiwe kama watoto/ndugu zetu na siyo kuwa fukuza au kuwapiga kama wezi.

Huwezi kumuita mtu mfanyakazi wakati unamlipa shs 10,000 au 15,000 kwa mwezi!!! Hawa ni ndugu zetu!!

Nakushukuru sana sana Magezi, umenisaidia kufafanua jambo hili, maana mimi nilikuwa sieleweki, Mungu na akubariki
 
Wito wa mtoa mada hii kwa jamii ni kwamba akina mama/baba tuwe na moyo wa utu na huruma ktk kuishi na watumishi wetu wa ndani na wanapo kosea tuwashauri/tuwaadhibu kama ndugu zetu/watoto wetu au wadogo zetu.
Kweli Magezi umenisaidia sana, mada hii inaeleweka isipokuwa kuna watu wanajifanya hawaelewi maana ninayopinga ndiyo wanayowafanyia hawa mabinti, Mungu atawalaani wote,
 
hivi kwa mfano ukimuuliza mimba katoa wapi akakwambia ni ya mmeo utafanya nini hapo??
swala la mshahara nalo ni issue 15,000.00 ni ndogo sana kwa maisha ya sasa sijui huwa tunafikilia nn kuwapa mshahara mdogo namna hii?

Wanakula na kulala kwa mwenye nyumba hawalipi kodi yeyote (umeme maji nk) nafikiri inawatosha
 
hivi kwa mfano ukimuuliza mimba katoa wapi akakwambia ni ya mmeo utafanya nini hapo??
swala la mshahara nalo ni issue 15,000.00 ni ndogo sana kwa maisha ya sasa sijui huwa tunafikilia nn kuwapa mshahara mdogo namna hii?
Kama ni ya mmeo, cha kufanya ni kuwaeleza wazazi wake kuwa amekuwa mke mwenzio na sio mfanyakazi tena, mmeo kama atakubali mwambie ampangishie chumba

Hiyo mishahara midogo ndiyo inayosababisha wapewe mimba na wauza mchicha magengeni au wapiga debe,

Msichana anayelipwa kuanzia 30,000/= kwa mwezi hawezi kupata mimba kienyeji hivyo.
 
Hebu leteni case studies za kweli, kisha tuzifanyie analysis.... hii nadharia haitaisaidia hii thread!
 
Hebu leteni case studies za kweli, kisha tuzifanyie analysis.... hii nadharia haitaisaidia hii thread!
Waulize waliosapoti mada hii, watakwambia kuwa yanatokea, kama unaishi uswahilini yanatokea sana, case za kweli utazipata ukitembelea uswahilini, lakini huko masaki na o`bay hauwezi kuelewa kinachozungumzwa hapa.
 
Hebu leteni case studies za kweli, kisha tuzifanyie analysis.... hii nadharia haitaisaidia hii thread!

Mkuu hii siyo nadhalia.....tunaishi mtaani tunayaona na wengine hapa tunaishi na hawa mabinti na wametueleza mengi kuhusu manyanyaso wanayo pata.

Cha msingi ni kwamba let's try to treat them equally as our children or young sisters then we will see the change.
 
Unakwenda kijijini unakuta familia masikini sana, hawana hata uwezo wa kupata mlo mmoja kutwa, kuwaonea huruma unachukua binti yao hadi kwako mjini akufanyie kazi za ndani, apate pesa awasaidie wazazi wake

Binti akiwa kwako anapata ujauzito, bila kujali ameupata wapi, wewe unamludisha kwao,

-Je! huu ni uungwana?
-Hauoni kuwa unaiongezea familia umasikini na mzigo wa kulea mimba na hatimaye mjukuu?
-hakuna njia nyingine ya kumsaidia huyu binti zaidi ya kumrudisha kwao?
-Je ukikuta mimba hiyo ni ya mwanao wa kiume? na wakati huo umeisha mrudisha kwao!

Asante Mkuu, kweli wanakosea
 
Masaki hata mimi pia sijamwelewa jamaa kabisa yaani alikuwa nalenga nini? Kaitaba please hebu tufafanulie ili tuelewe zaidi.

Jamani huyu anamaanisha nyie akina mama mna roho mbaya binti wa watu amepata mimba nyumbani kwako hata roho ya huruma kumsaidia hakuna ndo kwanza unamsepesha haraka haraka hata kama ni mimba ya mmeo.
 
Ninacho maanisha ni hiki, ebu tafakari mtoto katoka familia masikini, anakuja kwako kujikwamua na umasikini, bahati mbaya anapata ujauzito, badala ya kumbana kumtaja aliyempa huo ujauzito, badala yake hakina mama wanacho fanya ni kumpa kipigo kama mwizi, kisha kumrudisha kwao,

Sasa angalia, kwao ni masikini halafu anarudi kwao na mzigo, wewe unafikri wazazi watakuonaje,

Njia nzuri ni kumuozesha tu, na mimba wasiitoe anaweza kupata matatizo ukafungwa

namaanisha hilo.

niulize tena


mimba ya bahati mbaya? hiyo atakuwa amejitafutia matatizo mwenyewe!...kwanini actumie kinga?....kumuoza ni rahic pale ambapo aliempa mimba akamkubali akimkataa utafanyaje na huna ushaidi kwamba mimba ni ya huyo anaetajwa?....wawe makini watokapo kjjn.
 
Nafikiri hili suala inabidi tuliweke ktk mazingira ya kitanzania yaani tunawachukua hawa watoto wa kike kama wafanyakazi wa ndani lakini kiukweli huwezi kusema ni wafanyakazi per say. Wengi wao unakuta wadogo au hata kama wakubwa mambo mengi hawajui so ni kama kuwasaidia.

Kwa hiyo kwa uungwana unaweza kumsaidia kwamba ajifungue huyo mtoto lakini wazazi wake wataarifiwe kuhusu hali ilivyo na pia lazima amtaje aliye mpa uja uzito, ili mambo ya kisheria yafuate baada ya kujifungua.

Akisha jifungua kama utaona bado anafaa kuendelea kufanya kazi mimi sioni tatizo kwa nini asiendelee kuwepo mpaka yeye aseme anataka kuacha kukaa kwangu. Haya ni mawazo yangu na nafikiri ndivyo inapaswa kuwa.


na hicho kipindi akiwa mzazi nani anisaidie kazi za ndani na mie ni mfanyakazi na nina mtoto mdogo? malezi mchezo....kama wanajiona wadogo kwanini wanafanya mambo ya kikubwa, ndio maana niligoma na ma h/g,nilikuwa na mmoja na nilimtoa kjjn haswa, nilikaa nae chini na kumuelewesha maisha jinc alivyo awe makini na hiki na kile, alivyooanza kupendeza na tabia ilibadilika na aliempa ujauzito alimkana, nilifanya kumrudisha kwao na asante na pesa kidogo afanye shughuli binafc hapo kjjn.......
 
Ukikuta mimba ni ya mmeo hapo uamue kumuadhibu mmeo na siyo huyo binti kwni ni wewe ulimleta na amedanganywa na mumeo.

Ndiyo maana nikasema tushukulie mazingira ya kitanzania ambapo tunafanya mambo kiudugu lakini tukisema kazi kama kazi hakuna mtu wa kawaida atakaye chukua mtoto wa mtu eti ni mtumishi wa ndani.

Kuhusu mshahara hii inatokana na kwamba chakula wanapata ktk familia, matibabu, kulala, n.k. Lakini tukifanya kama nchi za wenzetu kwa mab ni ajira rasmi mshahara utapanda lakini inabidi huyu mtumishi ajitegemee kwa chakula, matibabu, maji, umeme (kama upo), malazi n.k. kwa hiyo hakuna mtoto wa maskini atakaye weza hayo.


sasa undugu upi wakati malezi ya wanangu yananipa presha?
 
Unakwenda kijijini unakuta familia masikini sana, hawana hata uwezo wa kupata mlo mmoja kutwa, kuwaonea huruma unachukua binti yao hadi kwako mjini akufanyie kazi za ndani, apate pesa awasaidie wazazi wake

Binti akiwa kwako anapata ujauzito, bila kujali ameupata wapi, wewe unamludisha kwao,

-Je! huu ni uungwana?
-Hauoni kuwa unaiongezea familia umasikini na mzigo wa kulea mimba na hatimaye mjukuu?
-hakuna njia nyingine ya kumsaidia huyu binti zaidi ya kumrudisha kwao?
-Je ukikuta mimba hiyo ni ya mwanao wa kiume? na wakati huo umeisha mrudisha kwao!
Well said Mkuu hapa jambo lipo lazima tulingalie kwa upanaa wake sana!
 
Kama ni ya mmeo, cha kufanya ni kuwaeleza wazazi wake kuwa amekuwa mke mwenzio na sio mfanyakazi tena, mmeo kama atakubali mwambie ampangishie chumba

Hiyo mishahara midogo ndiyo inayosababisha wapewe mimba na wauza mchicha magengeni au wapiga debe,

Msichana anayelipwa kuanzia 30,000/= kwa mwezi hawezi kupata mimba kienyeji hivyo.


mbona mie nilikuwa nampa 35 na alipata? na hapo ni nje ya kila kitu, malazi juu yangu,hata vitu vya kidada nilikuwa namnunulia pale ninapoweza....
 
hapo ndo ukweli utaujua lakini ukimfukuza haraka hutaujua ukweli na hata kama ni mumeo ndo kampa mimba mtumishi wa ndani sheria lazima imbane, tumeyaona kwa Mahita.
Mahita kalipa?! si bado mtoto anateseka,
 
Back
Top Bottom