Katika maisha unafiki ni muhimu sana!

Ryzen

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2012
Posts
7,301
Reaction score
8,706
Unajua bwana sisi tuliozaliwa vijijini tumeexperience maisha flani honest sana, yaani maisha yasiyo na unafiki wala makandokando, ila katika harakati za kusaka life huko Mijini, uki apply uhonest wa kijijini kwenu unafeli vibaya sana!

Kukaa mjini kumenifunza mengi, mtu kama ni mshikaji wako hata akifanya ujinga ilimradi yeye anapenda unamsifia tu, akilewa mpaka akazima ilimradi anapenda pombe na kulewa wewe unamsifia tu, ilimradi maisha yasonge.. Mkiambianana ukweli mnakosana, watu hawataki kuambiwa ukweli!

Na mengine mengi tu, Ama hakika Maisha bila Unafiki hayaendi!
 
Ni kweli af pia ukiona Hawa watu na wanakuchukia jua Kuna vitu unavifanya una misimamo mizuri..ila ukiona wanakucheka cheka na matabasam mengi jua huna viwango wanataka upotee.mtaani ukinunua TU gari utaanza kuchukiwa na maneno kibao juu yake
 
Ni kweli af pia ukiona Hawa watu na wanakuchukia jua Kuna vitu unavifanya una misimamo mizuri..ila ukiona wanakucheka cheka na matabasam mengi jua huna viwango wanataka upotee.mtaani ukinunua TU gari utaanza kuchukiwa na maneno kibao juu yake
Kabisa Mkali, nadhani nilichelewa kujua hii Principle!
 
Umeni kumbusha kuna series 1 hivi inaitwa fraternity ya ki-korea

Kuna scene moja mfamle Alikuwa anajifunza jinsi ya kutumia mshale na kulenga shabaha ....sasa kila alipo kuwa anarusha mshale ikawa anakosea ana miss target ...

Basi mpambe wake mmoja aka mwambia mfalme wangu una skills kubwa Sana Una kipaji mpaka cha kutumia mishale ..


Mfalme akamwambia ..hivi nyinyi watu keanini ni waongo hivi ..lina mtaamua kuwa mnaniambia ukweli ...Yaani unadiriki kumisifia sifa nzuri hata pale nina pokosea ..!!! Aka mwambia niwazi nitakuwa nimezungukwa na watu wanafiki wengi sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi kuna jamaa yangu nusura tukosane baada ya kumshauri gari aliyonae imechoka inamtia hasara ni bora arekebishe, Ila nikashtukia issue nikamwambia isee, kumbe gari yako nimeicheki kwenye mtandao ni gari ya dizaini yake ukiuza hii hupati tena kama hii, kwa sababu jamaa huwa tunakunywa kama tuna kiwanda chetu , huku tumekaa na Toto's, niliona nitakosa kampani yake. Mpaka sasa hivi akishauriwa hasara ya gari anawaambia " angalia aina ya hii gari kaingie mtandaoni, halafu leta jibu" tunaendelea kupiga maji huku tunapapasa Toto's. muda wa kuondoka baa likigoma Ku waka, namwambia , hii sehemu salama twende zetu tukashughulikie hawa viumbe gari tutaifuata kesho. Ila kweli hawakukosea kusema mpambe nuksi, na hiyo ni sababu hiyo tu, kuwa mnoko au mnafiki . ndicho binadamu idadi kubwa wanachopenda kukisikia ..[emoji41][emoji41][emoji41][emoji41]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna ukweli kiasi fulani.
 
Ahahahaha ni wachache sana wenye uelewa kama huyo Mfalme, wengi wao wapo kama Mheshimiwa hapa Nchini!
 
Absolutely, nivema ni vizuri kutokuwa Mnafiki, lakini wengi hawapendi kuwa Real, ili baadhi ya Michongo ifanikiwe ni Muhimu kuwa Mnafiki!
 
Mi napenda ukweli, sipendi kusifiwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Rafiki ni wachache kama wewe, Kuna rafiki yangu nilimkuta yuko na demu ambae ni Positive kitambo kirefu, asa demu ni mkali hasa utadhani kadownloadiwa.. Mwamba nikamstua asee kuwa mwana apo apafai.. Mchizi akanichukulia Snitch kuwa staki Apate Mtoto Mkali!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…