Katika Picha: Maandamano ya wanahabari Leo

Status
Not open for further replies.
Mzee Habib Nyundo aliyagusia yafuatayo:

Kwanza alidai wanahabari wameenda wakiwa wameziba midomo hivyo anaamini atakachoongea kitasikika japo itakuwa ni one way traffic.

Pili alisema Waziri hayupo yupo Bungeni Dodoma hivyo hawezi kujibu alichopelekewa haraka, hivyo atajibu baadaye.

Tatu alisema Jukwaa la Wahariri linalotambuliwa na serikali na lililosajiliwa lipo hivyo akawasihi wahariri kubadili jina kwani wao hawatambuliki! Kauli iliyoonekana kupokewa kwa hisia tofauti na kusababisha wengi kufungua midomo wakitaka kuongea lakini wakasita.

Tukatoka nje ya ofisi za Wizara na kikaendelea kifuatacho...
 
Oooohhhh!!! Zinaonekana wakuu, nadhani unatakiwa kusubiri kwa muda kiasi then unaziona....
Mh!!!Huyo Mkuchika aliyaona haya maandamano au aliona kwenye luninga tu??? any way good attempt ingawa mwanzo mgumu siku zote...
 
Hivi maandamano lazima yapokelewe ili yawe halali?
Nadhani maandamano yanapomkuta mtu aliyekusudiwa inakuwa ni nzuri zaidi kwani tunaamini kuwa ujumbe unamfikia moja kwa moja ingawa si lazima sana kuwa yapokelewe ndio kuwa halali. Uhalali wa maandamano nadhani ni mantiki ya wanaoandamana wanadhamiria kupeleka ujumbe gani ambao hautasababisha kero au uvunjifu wa utulivu/amani.
 
Asante kwa picha Maxence. Pongezi wanahabari kwa kushika bango. Mapambano yanaendelea....
 

Bwana Kibanda (anaonekana pichani) alionekana kushangazwa na serikali kulitambua Jukwaa la wahariri la miaka ya 70 ambalo ni wazi hakuna mhariri hata mmoja aliye katika vyombo vya sasa.

[Alimwakilisha Sakina Datoo ambaye yuko masomoni Ulaya]

Alisema kuwa kinachosisitizwa na Jukwaa la Wahariri si kwamba kilichoandikwa na MwanaHalisi ni sahihi ama si sahihi lakini akatoa dodoso kuwa kuna gazeti flani la leo limeandika habari ileile japo kwa namna tofauti.

Akaendelea kushangazwa na jinsi serikali inavyoamua kuchukua hatua kali dhidi ya vyombo vya habari ilhali walimu walipogoma (kitu ambacho serikali haikukiona halali) ilikwenda mahakamani, akauliza ni kwanini serikali haikwenda mahakamani kuiomba mahakama isitishe uchapishwaji wa gazeti hilo.

Aliendelea kuonesha kusikitishwa kwake na jinsi serikali inavyoonekana kuwa na ajenda ya siri kwani aliyeongelewa ni Ridhiwani naye hakutia neno na akashangaa serikali ilifungua kinywa kwa niaba ya Ridhiwani, ikachukua hatua kwa niaba ya Ridhiwani! Alisisitiza kuwa kilichoandikwa kuhusiana na njama za baadhi ya wanachama wa CCM kuwa na mbinu za chinichini kilikuwa ni kitendo cha kisiasa na katika siasa jambo hilo lipo!

Akatanabaisha kuwa Mhariri na Mkurugenzi wa MwanaHalisi bado wanaripoti makao makuu ya Wizara ya Mambo ya Ndani kila wiki kitendo ambacho amekilaani kuwa kina kitu nyuma yake.

Aliendelea kusema kuwa baadhi ya viongozi serikalini ni wamiliki wa vyombo vya habari ambavyo vimekuwa vikipindisha habari nyingi na haviguswi. Akavitahadharisha vyombo hivyo kuwa makini kwani vinaiangusha sana sekta ya habari

Naye Ayoub Ryoba alisisitiza kuwa Uhuru wa Habari Tanzania unaendelea kukandamizwa na akasisitiza kuwa wao kama MISA hawatavumilia kuona maslahi binafsi yanalindwa na maslahi ya taifa yanawekwa kando.


Ryoba leo 28 Oct '08

Mkurugenzi wa Chama cha waandishi wanawake Tanzania (TAMWA) alionesha kutofurahishwa na kitendo cha serikali kulifungia gazeti la MwanaHalisi. Akasema ukikifungia chombo chochote cha habari ni kuwa unakuwa unawafunga wananchi midomo. Akasisitiza kuwa mwanzo wa kufungia gazeti moja ndio mwanzo wa kufungia vyombo vingine vya habari binafsi. Akasisitiza Serikali ilifungulie gazeti hilo mara moja.


Mkurugenzi TAMWA

Mimi ni mjumbe tu
 
Nafurahia kusema kwamba ile "ndoa" kati ya viongozi wetu na baadhi ya waandishi wetu sasa imeanza kupungua kimapenzi na muda si mrefu mhimili huu wa nne utajitegemeza wenyewe.
Ndoa hii itadumu unless waandishi wanawezeshwa ipasavyo na vyombo vyetu vinakuwa na uwezo wa kusimama vyenyewe bila kuitegemea serikali.

Nilibahatika kuhudhuria UN GA siku za nyuma hakukuwa na chombo chochote cha habari toka Tanzania.

JK alipoingia angalau niliona vyombo vya serikali. TVT, RTD na Daily News.

Baadaye na vya binafsi kama ITV, Channel Ten na Star pia hudhuria nikajifariji kuwa media yetu si mchezo. Baadaye nikagundua anayewalipia ni serikali. Just imagine wewe ni mwandishi umefadhiliwa kuripoti JK kwenye GA. Unalipiwa return ticket ya Dar/NY/Dar. Unalazwa Intercontinental hapo New York. Utathubuti kuripoti ndivyo sivyo?.
Ndoa bado ipo, Mkuchika amechemka tuu na hapo ni penye uzia tuu, atakapochomeka rupia, watu watageukana.
 
Asante kwa picha Maxence. Pongezi wanahabari kwa kushika bango. Mapambano yanaendelea....
Asante mkuu.

Katika waliohudhuria sikumwona mhariri wa RAI wala Mtanzania.

Labda walikuwa na udhuru.
 
Tatizo serikali/mkuchika hajui nini maana ya MWANAHALISI na nani ni nani humo.....Salva acheni kumuumiza mkubwa wenu kwa shinkizo la mzigo wa kisiasa aliojibebesha (MAFISADI MAARUFU)....

Nataka kuaamini UAMUZI wa Mkuchika ni mwanzo wa mpango wa UDIKTETA wanao utaka MAFISADI ambao wamekuwa wakimtaka JK akubaliane nao muda mrefu.

Nina wasiwasi kuwa MKUCHIKA kafanya hayo akipigia mahesabu siasa za KIMAKUNDI ndani ya CCM na kumchinganisha JK na waandishi ambao hadi sasa wamejaribu sana kumlinda na UVUNDO WA UFUSADI.

Nina wasiwasi uamuzi wa MKUCHIKA ni moja ya hatua za mwanzo za kumuundoa JK mwaka 2010 kwa kuchochea chuki ya moja kwa moja kati ya waandishi na JK ili ikifika 2010 waseme kuwa hauziki na mzigo kwa CCM halafu wamtafute kanyaboya atakayeweza KUAMINIKA kwa maslahi ya CHAMA na MFUMO FISADI....

Tanzanianjema
 
Max asante kwa taarifa hii na picha. Hivi wahariri wa new habari co-operation walikuwepo?
 
Mkuu,

You nailed it!
 
Max asante kwa taarifa hii na picha. Hivi wahariri wa new habari co-operation walikuwepo?
Hapana mkuu Nziku,

Hili lilihojiwa na wengi, mpaka kwa kutania nikaulizwa "Wewe ndiye Manyerere?"
 
Kundi lingine jipya katika maandamano!Media must know that they have a very strong revolutionary power coz they have the power to create a plotical leader or destroy him!
 
Saed Kubenea naye alikuwepo kama anavyoonekana pichani...
 
Message sent! Tuhabarisheni basi after arriving wizarani, walipokelewa vipi, na/au barua walimkabidhi nani? Tupe mkuu kilichojiri!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…