NYAMKANG'ILI
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 223
- 112
CCM inataka serikali mbili ziendelee, wanakataa pendekezo la serikali 3. CCM wanatoa sababu nyingi ambazo siyo sababu hasa za kuwafanya CCM kukataa serikali3. SABABU zenyewe ZA CCM kukataa serikali3 ni hizi:
1) Muundo wa CCM, na kufanya kazi kwake, umetengenezwa kwa kuzingatia muundo wa serikali2
2) Iwapo kutakuwa na Serikali ya Tanganyika, itapaswa Rais wa Tanganyika ndiye awe mwenyekiti wa CCM taifa. Hii ni kwa sababu Tanganyika ndiko kuliko na watu wengi, raslimali nyingi, fedha nyingi, vyeo vingi vya kuwapatia makada wa chama. HILI KWA CCM ndo mtihani mkubwa, NANI AWE M/KITI kati ya Kiongozi wa TANGANYIKA na RAIS WA TZ?
3) Utulivu ndani ya CCM unategemea kitu kimoja tu: RASLIMALI na vyeo vya serikalini, katika serikali ya Jamhuri ya Muungano, ambavyo KWA MUUNDO wa sasa wa Muungano ni vya TZ, LAKINI ni vya Tanganyika katika mfumo wa serikali3. Kwa mfano, kada anapopiga kelele, anapozwa na ama uwaziri au ukuu WA MKOA, au ubalozi au u-DC, au ubunge wa kuteuliwa kama aliokuwa nao KINGUNGE kwa miaka yote, hajawahi kugombea jimboni, yeye ni mteuliwa. Na ukitofautiana nao, wanakufutia uteuzi; unarudi kijiweni, alafu baadaye unarudishwa kundini ukiwa umenyooka. Hili ndo lililotokea kwa SITTA. Hii kazi ya kujenga chama kwa kupitia mgongo wa raslimali za Tanganyika na vyeo vya Serikali anaifanya RAIS wa TZ ambaye NI M/KITI WA CCM TAIFA. Ukiiunda TANGANYIKA, BASI CCM itakuwa na mtihani mkubwa: nani awe m/kiti kati ya kiongozi wa Tanganyika mwenye mali na watu au RAIS WA TZ mwenye majeshi tu lakin asiye na mali wala watu wala vyeo vya kupooza makada?
4) Kambi za kugombea Urais wa TZ kupitia CCM. Hawa wakubwa watarudishaje pesa za 'marafiki' zao wanaowafadhili 'GIZANI' kwa ahadi za kupewa tenda, mikataba au vyeo? Hii ni kwa sababu Rais wa TZ ATAKUWA HANA vyeo wala raslimali za kuwapa makada ili watulie... HAWA WAMEJIPANGA KUKWAMISHA MCHAKATO MZIMA WA KATIBA.
Ukitazama hizi sababu (ambazo hazisemwi wala hazitasemwa hata siku moja na CCM) ndizo sababu za wao CCM kugomea serikali3. SERIKALI3 zitaimarisha sana Muungano, ila CCM itaparaganyika... na hapo ndipo wakubwa hawa wanaposema SERIKALI3 zitavunja muungano, badala ya kusema serikali3 zitaisambaratisha CCM...
1) Muundo wa CCM, na kufanya kazi kwake, umetengenezwa kwa kuzingatia muundo wa serikali2
2) Iwapo kutakuwa na Serikali ya Tanganyika, itapaswa Rais wa Tanganyika ndiye awe mwenyekiti wa CCM taifa. Hii ni kwa sababu Tanganyika ndiko kuliko na watu wengi, raslimali nyingi, fedha nyingi, vyeo vingi vya kuwapatia makada wa chama. HILI KWA CCM ndo mtihani mkubwa, NANI AWE M/KITI kati ya Kiongozi wa TANGANYIKA na RAIS WA TZ?
3) Utulivu ndani ya CCM unategemea kitu kimoja tu: RASLIMALI na vyeo vya serikalini, katika serikali ya Jamhuri ya Muungano, ambavyo KWA MUUNDO wa sasa wa Muungano ni vya TZ, LAKINI ni vya Tanganyika katika mfumo wa serikali3. Kwa mfano, kada anapopiga kelele, anapozwa na ama uwaziri au ukuu WA MKOA, au ubalozi au u-DC, au ubunge wa kuteuliwa kama aliokuwa nao KINGUNGE kwa miaka yote, hajawahi kugombea jimboni, yeye ni mteuliwa. Na ukitofautiana nao, wanakufutia uteuzi; unarudi kijiweni, alafu baadaye unarudishwa kundini ukiwa umenyooka. Hili ndo lililotokea kwa SITTA. Hii kazi ya kujenga chama kwa kupitia mgongo wa raslimali za Tanganyika na vyeo vya Serikali anaifanya RAIS wa TZ ambaye NI M/KITI WA CCM TAIFA. Ukiiunda TANGANYIKA, BASI CCM itakuwa na mtihani mkubwa: nani awe m/kiti kati ya kiongozi wa Tanganyika mwenye mali na watu au RAIS WA TZ mwenye majeshi tu lakin asiye na mali wala watu wala vyeo vya kupooza makada?
4) Kambi za kugombea Urais wa TZ kupitia CCM. Hawa wakubwa watarudishaje pesa za 'marafiki' zao wanaowafadhili 'GIZANI' kwa ahadi za kupewa tenda, mikataba au vyeo? Hii ni kwa sababu Rais wa TZ ATAKUWA HANA vyeo wala raslimali za kuwapa makada ili watulie... HAWA WAMEJIPANGA KUKWAMISHA MCHAKATO MZIMA WA KATIBA.
Ukitazama hizi sababu (ambazo hazisemwi wala hazitasemwa hata siku moja na CCM) ndizo sababu za wao CCM kugomea serikali3. SERIKALI3 zitaimarisha sana Muungano, ila CCM itaparaganyika... na hapo ndipo wakubwa hawa wanaposema SERIKALI3 zitavunja muungano, badala ya kusema serikali3 zitaisambaratisha CCM...