The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Serikali imeanza kujenga shule ya Sekondari Ruhuhu wilayani Ludewa mkoani Njombe ili kupunguza adha ya watoto kusafiri umbali wa takribani Km 15 Hadi Manda Sekondari na Km 30 Hadi Mchuchuma kupata elimu.
Kwa hatua za awali Tayari madarasa mawili yapo mwishoni kukamilika na Mbunge wa Jimbo la Ludewa Joseph Kamonga anasema mwezi Machi Mwaka huu Wanatarajia wanafunzi waanze kusoma.
Katika Sherehe za miaka 48 za kuzaliwa kwa Chama Cha mapinduzi CCM mkoa wa Njombe Mkuu wa shule ya Sekondari Ruhuhu Mwalimu Enocy Dominick amesema mazingira hatarishi ya watoto wa kike kutembea umbali mrefu kwenda Manda Sekondari na wamefikia zaidi ya Asilimia 80 katika utekelezaji wake.
Sesilia Ngatunga na Charles Mbuluma ni wakazi wa Ruhuhu ambao wanasema watoto wao Wengi Wamekuwa wakikwama kuhitimu masomo kutokana na changamoto mbalimbali zikiwemo za kupata ujauzito na kukosa baadhi ya Vipindi wakati mito inapojaa maji wakati wa masika lakini sasa wataepukana na janga Hilo.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Njombe Deo Sanga na Halima Mamuya Mlezi wa CCM mkoa wa Njombe na mjumbe wa Kamati kuu ya CCM Taifa wamesema serikali itakwenda kukamilisha ujenzi wa shule ya Sekondari Ruhuhu ili watoto wapate Elimu kwa ukaribu na urahisi.
Kwa hatua za awali Tayari madarasa mawili yapo mwishoni kukamilika na Mbunge wa Jimbo la Ludewa Joseph Kamonga anasema mwezi Machi Mwaka huu Wanatarajia wanafunzi waanze kusoma.
Katika Sherehe za miaka 48 za kuzaliwa kwa Chama Cha mapinduzi CCM mkoa wa Njombe Mkuu wa shule ya Sekondari Ruhuhu Mwalimu Enocy Dominick amesema mazingira hatarishi ya watoto wa kike kutembea umbali mrefu kwenda Manda Sekondari na wamefikia zaidi ya Asilimia 80 katika utekelezaji wake.
Sesilia Ngatunga na Charles Mbuluma ni wakazi wa Ruhuhu ambao wanasema watoto wao Wengi Wamekuwa wakikwama kuhitimu masomo kutokana na changamoto mbalimbali zikiwemo za kupata ujauzito na kukosa baadhi ya Vipindi wakati mito inapojaa maji wakati wa masika lakini sasa wataepukana na janga Hilo.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Njombe Deo Sanga na Halima Mamuya Mlezi wa CCM mkoa wa Njombe na mjumbe wa Kamati kuu ya CCM Taifa wamesema serikali itakwenda kukamilisha ujenzi wa shule ya Sekondari Ruhuhu ili watoto wapate Elimu kwa ukaribu na urahisi.