Katika vitu ambavyo hutakiwi kusahau katika maisha yako ni kutoa Zaka, uwe Mkristo, Mpagani au Muislam

Katika vitu ambavyo hutakiwi kusahau katika maisha yako ni kutoa Zaka, uwe Mkristo, Mpagani au Muislam

Mganguzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2022
Posts
1,604
Reaction score
3,715
Kama wewe unajua kwamba Mungu yupo! Hakikisha unatoa ZAKA. Fanya utani na masihara kwenye mambo yote lakini toa ZAKA! Babu yangu miaka Kumi iliyopita aliugua tb ambayo ilifanya apofuke macho! Hivyo akahudhuria kliniki na kuchoma sindano 120, lakini Bado hali yake haikubadilika ,naikumbuka siku Moja aliniita ni mwangalie mgongoni nikakuta anabanduka ngozi!

Akaniomba nianze kuitoa kwa kuibandua ,ilikuwa ni kazi ngumu ,unambundua ngozi mwili mzima na akiamka asubuhi ngozi unakuta ni kama jana hamkuibandua ,siku Moja yule babu alikata kauli ,watu wakakusanyika na kaburi likachimbwa ,alikuja askofu Mmoja hivi wa Moravian kutoka mission ya isoko Huko ileje mkoani songwe! Lakini kioja kilikuwa ni Kila wakiitoa maiti nje ili wakaizike inazinduka, anatikisa Mikono na kichwa ,wanaahirisha kuzika ,anaanza kupumua Tena kwa nguvu ,mnamrudisha ndani ,kaburi linafunikwa na mabati ,kesho mkiamka Tena mnakuta amekufa!

Kila wakijiandaa waanze ibada ya mazishi anazinduka,baada ya wiki Moja nakumbuka walikuja watumishi wengi kumuombea sana, siku ya saba alizinduka na kutamka maneno mazito kwamba nahitaji kutoa ZAKA, wakamwita askofu na mchungaji, wakaja kumsikiliza, walipoanza kumuuliza aliwajibu tena kwamba nataka kutoa ZAKA, bibi yetu akaruhusu atolewe ng'ombe kama zaka ya babu yetu, na akaomba akabidhiwe kamba ya Huyo ng'ombe kwa mkono wake akaikabidhi kwa askofu na wachungaji waliokuwepo ,walipoipokea na kuiombea na yeye akakata roho na hatimae akazikwa salama!

Hiki ni kisa kidogo lakini. Naamini sisi wengi hatuna elimu ya zaka ,mungu ndie akupae Kila kitu ,usione kama ni hasara kutoa zaka, hata kama Kuna watu watakubeza lakini toa ZAKA, kwa kadiri ya kipato chako ,hata kama hujawahi kuingia kanisani wewe agiza zaka Yako iende kanisani, au msikitini ama kwa mtumishi yeyote aliyekaribu Yako! Zaka inajitegemea na haihusiana na sadaka za kuwapa maskini na wahitaji Ile inaitwa ZAKA,
Kamwe usifanye mzaha kwenye kipengele cha zaka!

Uwe machinga, mpiga debe, mchoma chips, mama mboga ,mchimbaji ,mvuvi mkulima, mwanasiasa, shemasi, Mzee kanisa, doctor, msanii vyovyote ulivyo hakikisha unamtolea mungu zaka kila jumapili, kama huna muda wa kuhudhuria ibada nunua bahasha Yako ,Kila jumapili mwagize hata mtoto ataipeleka na itaombewa zaka Haina excuse, ni lazima.
 
Ndo umejua leo we jifanye mjanja na bia zako sinza
 
Kusaidia masikini wenye uhitaji na wagonjwa au kumpa mchungaji hela yangu kwa jina la zaka kipi kina thamani mkuu?

Unaweza kumsaidia mtoto yatima ada ya shule au pesa ya matibabu akatibiwa akapona au unaweza kupeleka kanisani hiyo pesa kwenye bahasha kwa jina la zaka alafu jioni mchungaji akaenda kaunta kuagiza kvant au akachukulia demu hiyo hela kipi cha kupitishia zaka hapo mkuu
 
Kama wewe unajua kwamba mungu yupo! Hakikisha unatoa ZAKA! Fanya utani na masihara kwenye mambo yote lakini toa ZAKA! Babu yangu miaka Kumi iliyopita aliugua tb ambayo ilifanya apofuke macho! Hivyo akahudhuria kliniki na k
Mmmh!
Hii nakataa kimtindo. Umechanganya vitu vingi, tofauti tofauti kwenye kapu moja)
Kutoa sadaka yoyote kunahitaji vitu vikuu vitano:

1. Unamwamini yule unayemtolea hiyo sadaka. Ni Mungu yupi unayemtolea hiyo sadaka? (Sadaka ni ibada kwa 100%)

2. Unajua maana ya hiyo sadaka unayotaka kuitoa. (Umeambiwa nini kuhusu hiyo sadaka ukitoa na je umeamini hicho?)

3. Unatoa sadaka halali au haramu (Umeipata vipi hiyo sadaka? Je ni mapato halali au haramu?)

4. Moyo wako hapo kabla umeandaliwa vipi kuhusu Mungu anayetaka kumtolea . (Sadaka ya Mungu wa Kweli inaanzia moyoni. Toba, Toba, Toba, Toba.....)

5. Unatoa wapi au kwa nani? (Kuna sadaka inatakiwa kwenda kwa mjane na yatima halafu wewe umekwenda kumpa pastor wako ili kuongeza suti nyingine, hapo usitegemee kupata baraka)
 
Kusaidia masikini wenye uhitaji na wagonjwa au kumpa mchungaji hela yangu kwa jina la zaka kipi kina thamani mkuu?

Unaweza kumsaidia mtoto yatima ada ya shule au pesa ya matibabu akatibiwa akapona au unaweza kupeleka kanisani hiyo pesa kwenye bahasha kwa jina la zaka alafu jioni mchungaji akaenda kaunta kuagiza kvant au akachukulia demu hiyo hela kipi cha kupitishia zaka hapo mkuu
Ubishi wakati mwingine hauna faida mkuu...toa kanisani au msikitini, mengine achana nayo
 
Tusichanganye baina ya ZAKA na SADAKA. Ninavyofahamu ni kwamba:-

ZAKA ni sehemu ya KUMI au 10% ya mapato yako. Mfano kama umepata shilingi 1000/= ZAKA unayotakiwa kutoa ni shilingi 100/=

Kwa upande wa sadaka ni kiasi chochote cha pesa au mali ambacho moyo wako umeamua kutoa kwa Mungu. Sadaka haina kiwango maalumu. Lakini kumbuka: usitoe Sadaka kilema au Sadaka dhaifu. Chochote upandacho ndicho utavuna. Ukitoa kwa ukarimu utavuna kwa ukarimu. Ukipanda haba (uchoyo), utavuna kadiri ulivyopanda. Mfano wa kupanda haba ni huu: una kipato cha shilingi 1,000,000/ kwa mwezi halafu ukienda ibadani unatoa shilingi 500/=

Naishia hapo kwa leo. Muwe na jioni njema.
 
Tusichanganye baina ya ZAKA na SADAKA. Ninavyofahamu ni kwamba:-

ZAKA ni sehemu ya KUMI au 10% ya mapato yako. Mfano kama umepata shilingi 1000/= ZAKA unayotakiwa kutoa ni shilingi 100/=

Kwa upande wa sadaka ni kiasi chochote cha pesa au mali ambacho moyo wako umeamua kutoa kwa Mungu. Sadaka haina kiwango maalumu. Lakini kumbuka: usitoe Sadaka kilema au Sadaka dhaifu. Chochote upandacho ndicho utakuwa. Ukitoa kwa ukarimu utakuwa kwa ukarimu. Ukipanda haba (uchoyo), utavuna kadiri ulivyopanda. Mfano wa kupanda haba ni huu: una kipato cha shilingi 1,000,000/ kwa mwezi halafu ukienda ibadani unatoa shilingi 500/=

Naishia hapo kwa leo. Muwe na jioni njema.
Zaka inatakiwa itolewe wapi?
Je ni lazima itolewe kanisani tuu?
Je nikiwa nachukua 10% yangu naipeleka direct kwa wahitaji ni kosa?
 
Kama wewe unajua kwamba mungu yupo! Hakikisha unatoa ZAKA! Fanya utani na masihara kwenye mambo yote lakini toa ZAKA! Babu yangu miaka Kumi iliyopita aliugua tb ambayo ilifanya apofuke macho! Hivyo akahudhuria kliniki na kuchoma sindano 120 ,lakini Bado hali yake haikubadilika ,naikumbuka siku Moja aliniita ni mwangalie mgongoni nikakuta
NAKAZIA
 
Kama wewe unajua kwamba mungu yupo! Hakikisha unatoa ZAKA! Fanya utani na masihara kwenye mambo yote lakini toa ZAKA! Babu yangu miaka Kumi iliyopita aliugua tb ambayo ilifanya apofuke macho! Hivyo akahudhuria kliniki na kuchoma sindano 120 ,lakini Bado hali yake haikubadilika ,naikumbuka siku Moja aliniita ni mwangalie mgongoni nikakuta an
Umeandika VYEMA sana mwanzoni katikati ila mwisho sasa unatuambia jumapili wakati wengine tunasali jumamosi, Wengine Ijumaa,Si ungemalizia tu kama ulivyoanza kwamba yeyote Kwa Imani yake atoe Zaka,Nakubaliana na wewe 100% kuwa Zaka ni jambo la muhimu sana kiimani na tulifanye liwe la kwanza kwani ni utii kwetu Kwa MUNGU wetu
 
ZAKA NI MUHIMU..Hayo mengne eti alikuwa anakufa anafufuka hayo maongo kandanganye watoto.zaka hailazimishwi bali inatolewa kwa moyo wa utii na upendo kwa mungu wako.
 
Kama wewe unajua kwamba mungu yupo! Hakikisha unatoa ZAKA! Fanya utani na masihara kwenye mambo yote lakini toa ZAKA! Babu yangu miaka Kumi iliyopita aliugua tb ambayo ilifanya apofuke macho! Hivyo akahudhuria kliniki na kuchoma sindano 120 ,lakini Bado hali yake haikubadilika ,naikumbuka siku Moja aliniita ni mwangalie mgongoni nikakuta
Hakuna mahali popote Mungu amekuagiza wewe mtanzania usiye wa kabila la Israel utoe zaka.

HAKUNA
 
ka Yako iende kanisani ,au msikitini ama kwa mtumishi yeyote aliyekaribu Yako! Zaka inajitegemea na haihusiana na sadaka za kuwapa maskini na wahitaji Ile inaitwa ZAKA,
Wagalatia hamna akili,zaka wenzenu wanawapa masikini,nyie mnawapa hao wachungaji matapeli
 
Kusaidia masikini wenye uhitaji na wagonjwa au kumpa mchungaji hela yangu kwa jina la zaka kipi kina thamani mkuu?

Unaweza kumsaidia mtoto yatima ada ya shule au pesa ya matibabu akatibiwa akapona au unaweza kupeleka kanisani hiyo pesa kwenye bahasha kwa jina la zaka alafu jioni mchungaji akaenda kaunta kuagiza kvant au akachukulia demu hiyo hela kipi cha kupitishia zaka hapo mkuu
Kuwapa masikini ni bora zaidi
 
Back
Top Bottom