Katoro, Geita bado haijatendewa haki

Katoro, Geita bado haijatendewa haki

G-Mdadisi

Senior Member
Joined
Feb 15, 2018
Posts
165
Reaction score
100
KATORO, Geita. Kijiji pekee nchini kwasasa chenye hadhi ya kuitwa MJI lakini bado kinatambulika kama Kijiji sawa sawa na kijiji cha KASATO kule Biharamulo, ama Kiuyu Mbuyuni kule Micheweni, Pemba Zanzibar.

UKipata fursa ya kufika KATORO. Hapa kuna
BENKI karibu zote uzijuazo
MAJI ya kutosha
UMEME wa uhakika
MIUNDOMBINU ya Barabara bora hadi mitaani kuzidi hata meneo mengi yenye hadhi ya mji.

KATORO Ndilo lango la wafanyabiashara wa Nguo, urembo n.k (MACHINGA), pikipiki na bidhaa mbapimbali kutoka mikoa ya Kagera, Mwanza,Shinyanga, Simiyu, Dodoma, Tabora, Kigoma, Singida, hadi nchini UGANDA.

Cha kuvutia zaidi ni kwamba KATORO ni miongoni mwa maeneo salama, na yenye maisha rafiki kabisa kwa kila mtanzania kumudu kuishi kulingana na uwezo wa kipato chake. Hapa bidhaa ni bei ya kawaida sana ukilinganisha na maeneo mengine (kama wewe ni mtembeaji)

Licha ya ukubwa wa eneo hili kibiashara na kimaendeleo lakini bado #KATORO kiserikali inatambulika kwa hadhi ya KIJIJI ikiongozwa chini ya serikali ya KIJIJI na KATA.

Mpango wa kuzaliwa kwa mkoa mpya wa CHATO huenda ukaja kuzaa mabadiliko ya hadhi ya eneo hili la Katoro na kupata fursa ya kupanda hadhi kwani hapa ni moja ya maeneo ambayo bado mamlaka hazijayatendea haki kabisa na yana kila sababu ya kuitwa mji kutokana na kasi ya maendeleo iliyopo.

Kama hili la kuundwa kwa mkoa mpya wa #Chato litafanikiwa, sehemu ya kwanza na hazina kimkakati ni eneo hili kwani hapa ndipo pesa zinatengenezwa. Linahitaji kuangaliwa na kupewa hadhi yake.

Wasalaam
#GMdadisi

IMG-20210930-WA0004.jpg

 
Ila watu wa huko ni wabinafsi kupitiliza. Haijawahi kutokea Wilaya inapigiwa chapuo iwe Mkoa, kijiji kiwe mji, jimbo lijengewe airport, mbuga, mabenki, chuo, jengo la TRA, na bado kuomba Mkoa jirani uwachangie eneo daaah!

Halafu nikiwaza huyo mungu wenu alivyozima mchakato wa Moshi kuwa jijieti kisa watu wa huko ni wapinzani, ndiyo ninachoka
 
Ila watu wa huko ni wabinafsi kupitiliza. Haijawahi kutokea Wilaya inapigiwa chapuo iwe Mkoa, kijiji kiwe mji, jimbo lijengewe airport, mbuga, mabenki, chuo, jengo la TRA, na bado kuomba Mkoa jirani uwachangie eneo daaah!

Halafu nikiwaza huyo mungu wenu alivyozima mchakato wa Moshi kuwa jijieti kisa watu wa huko ni wapinzani, ndiyo ninachoka
Sasa kwanini uwe na jiji la moshi na arusha umbali wa saa 1?Nyie ndo wabinafsi
 
katoro hakuna huduma ya maji, katoro nzima na buseresere zinategemea chemchem za maji ya kabaherere kama chanzo kikuu.
na kuhusu barabara za mitaa ni bado n changamoto kubwa hasa kwa upande wa katoro ila upande buseresere Diwan wao (Gody) kafanya kweli kwenye barabara za mitaa.

yote katika yote Katoro ni kijiji kinachofunika Geita mjini.
 
Ila watu wa huko ni wabinafsi kupitiliza. Haijawahi kutokea Wilaya inapigiwa chapuo iwe Mkoa, kijiji kiwe mji, jimbo lijengewe airport, mbuga, mabenki, chuo, jengo la TRA, na bado kuomba Mkoa jirani uwachangie eneo daaah!

Halafu nikiwaza huyo mungu wenu alivyozima mchakato wa Moshi kuwa jijieti kisa watu wa huko ni wapinzani, ndiyo ninachoka
Moshi gani hiyo iwe jiji[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Napakubali sana katoro. Ardhi nzuri, samaki(fried,dried/smoked, fresh and tasty from fishermen) wa kutosha hapo busere sere na ccm pale, samaki wengi sana (availability) kuzidi hata Mwanza. Kuku, mbuzi na nyama ya ng'ombe huko vina ladha sana. Ndula za maana sokoni pale busere. Good weather.

Nani anamfahamu Mwl. Raphael na kwaya zake Katoro primary school enzi hizo?! The guy is a legend.

Katoro is sure a very rapid grown and still growing place. I ever been to Katoro, Chato and Geita urban but Katoro is phenomenal. Katoro is my favourite place next to Mwanza town
 
Haya tumewasikia na sisi huku peramiho tunaomba serikali iwe wilaya inayojitegemea maana tuna kila kitu Zaid ya wilaya nyingne hapa Tanzania





Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Sasa kwanini uwe na jiji la moshi na arusha umbali wa saa 1?Nyie ndo wabinafsi
Arusha ni Makao Makuu ya Mkoa wa Arusha kwa hiyo kuwa na jiji kisheria ni sawa.

Moshi ni Makao Makuu ya Kilimanjaro kwa hiyo kuwa jiji kisheria ni sawa.

Sass ninyi mnataka kijiji kiwe mji wakati kisheria, Kata moja au zaidi ndiyo hupanda hadhi kuwa mji mdogo, na siyo kijiji wala kitongoji.

Eti jimbo la chato nalo liwe Mkoa?dah yaani kwa maneno mengine mnataka tarafa iwe Mkoa, na baada ya kukosa vigezo mmeomba Mkoa jirani wa Mwanza uwagawie Jimbo la Buchosa(ambalo ninyi mnaliita Wilaya, Buchosa ipo ndani ya Wilaya ya Sengerema) ili mpate kigezo cha kuunda kimkoa kisicho na vigezo.
 
Ila watu wa huko ni wabinafsi kupitiliza. Haijawahi kutokea Wilaya inapigiwa chapuo iwe Mkoa, kijiji kiwe mji, jimbo lijengewe airport, mbuga, mabenki, chuo, jengo la TRA, na bado kuomba Mkoa jirani uwachangie eneo daaah!

Halafu nikiwaza huyo mungu wenu alivyozima mchakato wa Moshi kuwa jijieti kisa watu wa huko ni wapinzani, ndiyo ninachoka
wakati munajipelekea barabara za rami na umeme kila kijiji huko kwenu kuna mtu alihoji?
 
Ni mji pekee pia ndani yake kuna miji miwili ndani ya wilaya mbili tofauti. Ndani Katoro, kuna Katoro ambayo iko wilaya Geita na vilevile ndani ya Katoro kuna buseresere ambayo iko wilaya ya Chato. Waanze kwanza kutatua hili, hakuna haja ya kuwa na miji miwili tofauti ndani ya mji mmoja.
KATORO, Geita. Kijiji pekee nchini kwasasa chenye hadhi ya kuitwa MJI lakini bado kinatambulika kama Kijiji sawa sawa na kijiji cha KASATO kule Biharamulo, ama Kiuyu Mbuyuni kule Micheweni, Pemba Zanzibar.

UKipata fursa ya kufika KATORO. Hapa kuna
BENKI karibu zote uzijuazo
MAJI ya kutosha
UMEME wa uhakika
MIUNDOMBINU ya Barabara bora hadi mitaani kuzidi hata meneo mengi yenye hadhi ya mji.

KATORO Ndilo lango la wafanyabiashara wa Nguo, urembo n.k (MACHINGA), pikipiki na bidhaa mbapimbali kutoka mikoa ya Kagera, Mwanza,Shinyanga, Simiyu, Dodoma, Tabora, Kigoma, Singida, hadi nchini UGANDA.

Cha kuvutia zaidi ni kwamba KATORO ni miongoni mwa maeneo salama, na yenye maisha rafiki kabisa kwa kila mtanzania kumudu kuishi kulingana na uwezo wa kipato chake. Hapa bidhaa ni bei ya kawaida sana ukilinganisha na maeneo mengine (kama wewe ni mtembeaji)

Licha ya ukubwa wa eneo hili kibiashara na kimaendeleo lakini bado #KATORO kiserikali inatambulika kwa hadhi ya KIJIJI ikiongozwa chini ya serikali ya KIJIJI na KATA.

Mpango wa kuzaliwa kwa mkoa mpya wa CHATO huenda ukaja kuzaa mabadiliko ya hadhi ya eneo hili la Katoro na kupata fursa ya kupanda hadhi kwani hapa ni moja ya maeneo ambayo bado mamlaka hazijayatendea haki kabisa na yana kila sababu ya kuitwa mji kutokana na kasi ya maendeleo iliyopo.

Kama hili la kuundwa kwa mkoa mpya wa #Chato litafanikiwa, sehemu ya kwanza na hazina kimkakati ni eneo hili kwani hapa ndipo pesa zinatengenezwa. Linahitaji kuangaliwa na kupewa hadhi yake.

Wasalaam
#GMdadisi

 
Back
Top Bottom