Katuni pendwa ya watoto ya Scooby-Doo yamtambulisha mmoja wa wahusika kama msagaji

Katuni pendwa ya watoto ya Scooby-Doo yamtambulisha mmoja wa wahusika kama msagaji

Cannabis

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
11,557
Reaction score
33,535
images - 2022-10-06T030000.960.jpeg

Katuni maarufu ya Scooby-Doo ambayo imekuwa ikionyeshwa katika chaneli mbali mbali kama Cartoon Network, imemtambulisha mmoja wapo wa wahusika kama msagaji (lesbian).

Mhusika huyo anayeitwa Velma ameonyeshwa katika toleo jipya la katuni hiyo kama mwanamke anayevutiwa kimapenzi na mwanamke mwingine.

Hali hiyo imepelekea mgongano wa mawazo katika mitandao ya kijamii nchini Marekani, ambapo baadhi ya watu wamesema hakukuwa na ulazima wa kuweka maudhui hayo katika katuni ya watoto.

Kutokana na maamuzi hayo mtandao wa Google umeonekana kuunga mkono maamuzi hayo ambapo wameweka rangi nyingi za upinde wa mvua pale mtu anavyotafuta neno "Velma" katika mtandao huo kama inavyoonekana kwenye picha.

Hali hii inazidi kuonyesha uhitaji wa ongezeko la umakini wa wazazi kuhusiana na maudhui ambayo watoto hujifunza kutoka kwenye katuni ambazo zimekuwa zikitazamwa kwa miaka mingi hapa nchini Tanzania.

IMG_20221006_024829.jpg
 
Inabidi wazazi mdownload katuni za zamani 1970s kama kina Tom and Jerry, mpaka miaka ya 2000 ndio muwawekee watoto kwa sababu hizo agenda zilikuwa hazijapenyezwa kwenye mainstream media zao.

kuanzia 2010s kwenda juu hapo risk ni kubwa sana lazima utakuta kuna viashiria fulani tu !
 
Mnakuza mambo tu.
Kwani watu wazima usagaji wamejifundishia kwenye katuni?
Kama mtu msagaji atabaki kuwa msagaji tu hakuna haja ya kufundishwa wala nini.
Kuna mmoja alisema ushoga Afrika umeletwa na Wazungu, nikamuuliza huko kwa Wazungu ushoga umepelekwa na nani hakunipa jibu
 
Inabidi wazazi mdownload katuni za zamani 1970s kama kina Tom and Jerry, mpaka miaka ya 2000 ndio muwawekee watoto kwa sababu hizo agenda zilikuwa hazijapenyezwa kwenye mainstream media zao.

kuanzia 2010s kwenda juu hapo risk ni kubwa sana lazima utakuta kuna viashiria fulani tu !
Sahihi kabisa kwa 100%.
 
Tutengeneze katuni zetu,zenye maudhui ya jamii yetu.
sio tu kuwa nakubaliana nawe lakini pia nafikiri sasa ni waktai mahususi wa wizara husika, uandaanda mtaala kwa watengeneza kattuni wa Tanzania iliwaweze kutengeneza katuni za kuongeza maarifa ya watoto, kwenye nyanja za sanaa,siasa, sayansi, uchumi na kuwaburudisha. Hii itasaidika kujenga kizazi chenye fikra ya Kitanzania kuuelekea ulimwengu.
 
Wazazi inabidi kuwa makini watoto wanatazama nini. Ni vizuri kutafuta background info kuhusu wahusika kabla ya kuruhusu watoto kutazama

..... mimi binafsi siku nilipojua mhusika mkuu wa vichekesho vya bingbang theory (Sheldon) ni shoga na ameolewa niliudhika na nikaacha kabisa kutazama vile vichekesho. Bora nimtazama charlie happer ambaye ni kitombi na mtumia madawa
 
cartoon nzuri na sijui kama zipo sahivi..
tom and jerry
pink panther
dexter the laboratory
ed, edd, eddy (sijui nimepatia kuandika)
the power puff girls
😂😂😂

bila kimsahau john bravo
 
Mnakuza mambo tu.
Kwani watu wazima usagaji wamejifundishia kwenye katuni?
Kama mtu msagaji atabaki kuwa msagaji tu hakuna haja ya kufundishwa wala nini.
Kuna mmoja alisema ushoga Afrika umeletwa na Wazungu, nikamuuliza huko kwa Wazungu ushoga umepelekwa na nani hakunipa jibu
Okay Mr. Rainbow tumekupata

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mashoga na wasagaji hawabadiliki, kutokuonesha vipindi hivyo bado wanapelekana kwa mpalange kama kawaida😡
 
Marekani ni taifa linalofuata misingi ya kikrsto kama zlvyo nchi za jumuia ya ulaya.
Ushoga kwao sio dhambi.
 
Marekani ni taifa linalofuata misingi ya kikrsto kama zlvyo nchi za jumuia ya ulaya.
Ushoga kwao sio dhambi
 
Taratibu rainbow,,hivi nchi Zp znaruhusu ushoga na mashoga kuolewa???
Taja walau nchi mbili basi,then tutajua wapi asili ya ushoga
 
Mnakuza mambo tu.
Kwani watu wazima usagaji wamejifundishia kwenye katuni?
Kama mtu msagaji atabaki kuwa msagaji tu hakuna haja ya kufundishwa wala nini.
Kuna mmoja alisema ushoga Afrika umeletwa na Wazungu, nikamuuliza huko kwa Wazungu ushoga umepelekwa na nani hakunipa jibu
yaani sisi wafrika tuna shida weeee!!utafikiria sisi tuko peponi,maujinga yetu hatuyaoni,mfano haya mauaji ya kikatili tunayofanyiana kila siku,hatuyaoni kwakuwa ni silaha zetu ndio zinatumika,ila ingekuwa ni bunduki ungesikia ohooo,ni wazungu!!!kama kwenye jamii yako maudhui hayo hayafai acha kuyaangalia tu,siku moja nilisia eti wanamuomba rais aingilie kati,chaneli hizo zifungwe!!!waafrika tumezidi unafiki sana
 
Inabidi wazazi mdownload katuni za zamani 1970s kama kina Tom and Jerry, mpaka miaka ya 2000 ndio muwawekee watoto kwa sababu hizo agenda zilikuwa hazijapenyezwa kwenye mainstream media zao.

kuanzia 2010s kwenda juu hapo risk ni kubwa sana lazima utakuta kuna viashiria fulani tu !
Huko kote watakuja unafikir hiyo Scooby niya juzi kwa kifupi hawa jamaa wamedhamiri na wako tayari kwa gharama yoyote ajenda yao itimizwe
 
Back
Top Bottom