Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Habari za asubuhi wakuu.
Siku ya jana, Mzee Wa Upako yaani Mchungaji Anthony Lusekelo alitengeneza headlines nchini kufuatia interview alyofanya na Jambo TV Online ambapo alizungumzia upepo wa kisiasa ulivyo nchini ikiwemo ishu za utekaji, ukosoaji unaendelea dhidi ya Rais Samia na mengineyo.
Lakini hii si mara ya kwanza kwa Mzee Wa Upako kutoa kauli ambazo zimeshtua na kutengeneza headlines Tanzania.
Tofauti na viongozi wengine wa kiimani ambao mara nyingi wamekuwa low profile kuzungumzia ongoing issues, Lusekelo amekuwa wa tofauti.
Here is how many times, mchungaji huyu ametengeneza headlines na kauli zake:
1. Nampenda Diamond, Ali Kiba Ana Kiburi
Mei 2018, Mzee Lusekelo aliingia kwenye headlines baada ya kusema kuwa anampenda Diamond zaidi kuliko Ali Kiba kwa sababu Diamond anaonekana kuwa Mnyenyekevu zaidi kuliko Ali Kiba
Pitia: Mzee wa Upako: Nampenda Diamond kwa sababu ni mnyenyekevu, simpendi Alikiba ni kiburi
2. Walionichafua Watakufa
Hii aliisema Desemba 2016 ambapo akiwa anaongea kwenye mahubiri yake ambapo alisema kuwa kila mwandishi wa habari aliyemuandika vibaya atakufa.
Soma Pia<<< Mzee wa Upako: Wote Walionichafua Watakufa Mwakani, Wasipokufa Nitaanza Kuuza Gongo
3. Unakujaje Kanisani Bila Sadaka?
Kwa wale wote ambao mnaenda kanisani bila kutoa sadaka, Lusekelo alitupa jiwe gizani July 2024 akiwa kwenye interview pale Wasafi FM kwa kuhoji wazi wazi kuwa Unakujaje Kanisani Bila Sadaka?
Swali likawa ni, je kama hauna sadaka hautakiwi kwenda kanisani?
4. Ishu Ya Tozo
Septemba 2022, Mchungaji Anthony Lusekelo alileta mjadala mkubwa mitandaoni baada ya kutetea tozo zilizoletwa na uongozi wa Rais Samia kwenye mitandao.
Katika kipindi ambacho Watanzania walikuwa wanalalamika kuhusu tozo, Lusekelo alijitokeza hadharani na kutetea tozo kwa kudokeza kuwa zilianza tangu kipindi cha torati.
Pitia<<< Mzee wa upako: Nchi itajengwa na wananchi wenyewe
5. Wagombea Urais Lazima Wawe Na Cheti Cha JKT
Mwaka 2022, Mzee Wa Upako aliishauri Tume Ya Uchaguzi yaani NEC kuweka kuhitimu JKT kama kigezo cha mwanasiasa kuruhusiwa kugombea Urais.
Pitia>>> Mzee wa Upako ataka wagombea Urais kuwa na cheti JKT
Hizi ni baadhi tu ya kauli za Mzee Wa Upako, kama unakumbuka nyingine tupia hapo chini.
Siku ya jana, Mzee Wa Upako yaani Mchungaji Anthony Lusekelo alitengeneza headlines nchini kufuatia interview alyofanya na Jambo TV Online ambapo alizungumzia upepo wa kisiasa ulivyo nchini ikiwemo ishu za utekaji, ukosoaji unaendelea dhidi ya Rais Samia na mengineyo.
Lakini hii si mara ya kwanza kwa Mzee Wa Upako kutoa kauli ambazo zimeshtua na kutengeneza headlines Tanzania.
Tofauti na viongozi wengine wa kiimani ambao mara nyingi wamekuwa low profile kuzungumzia ongoing issues, Lusekelo amekuwa wa tofauti.
Here is how many times, mchungaji huyu ametengeneza headlines na kauli zake:
1. Nampenda Diamond, Ali Kiba Ana Kiburi
Mei 2018, Mzee Lusekelo aliingia kwenye headlines baada ya kusema kuwa anampenda Diamond zaidi kuliko Ali Kiba kwa sababu Diamond anaonekana kuwa Mnyenyekevu zaidi kuliko Ali Kiba
Pitia: Mzee wa Upako: Nampenda Diamond kwa sababu ni mnyenyekevu, simpendi Alikiba ni kiburi
2. Walionichafua Watakufa
Hii aliisema Desemba 2016 ambapo akiwa anaongea kwenye mahubiri yake ambapo alisema kuwa kila mwandishi wa habari aliyemuandika vibaya atakufa.
Soma Pia<<< Mzee wa Upako: Wote Walionichafua Watakufa Mwakani, Wasipokufa Nitaanza Kuuza Gongo
3. Unakujaje Kanisani Bila Sadaka?
Kwa wale wote ambao mnaenda kanisani bila kutoa sadaka, Lusekelo alitupa jiwe gizani July 2024 akiwa kwenye interview pale Wasafi FM kwa kuhoji wazi wazi kuwa Unakujaje Kanisani Bila Sadaka?
Swali likawa ni, je kama hauna sadaka hautakiwi kwenda kanisani?
4. Ishu Ya Tozo
Septemba 2022, Mchungaji Anthony Lusekelo alileta mjadala mkubwa mitandaoni baada ya kutetea tozo zilizoletwa na uongozi wa Rais Samia kwenye mitandao.
Katika kipindi ambacho Watanzania walikuwa wanalalamika kuhusu tozo, Lusekelo alijitokeza hadharani na kutetea tozo kwa kudokeza kuwa zilianza tangu kipindi cha torati.
Pitia<<< Mzee wa upako: Nchi itajengwa na wananchi wenyewe
5. Wagombea Urais Lazima Wawe Na Cheti Cha JKT
Mwaka 2022, Mzee Wa Upako aliishauri Tume Ya Uchaguzi yaani NEC kuweka kuhitimu JKT kama kigezo cha mwanasiasa kuruhusiwa kugombea Urais.
Pitia>>> Mzee wa Upako ataka wagombea Urais kuwa na cheti JKT
Hizi ni baadhi tu ya kauli za Mzee Wa Upako, kama unakumbuka nyingine tupia hapo chini.