Pre GE2025 Kauli hii ya Rais Samia kuhusu nishati safi itavutia wanawake wengi kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu 2025

Pre GE2025 Kauli hii ya Rais Samia kuhusu nishati safi itavutia wanawake wengi kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Pamoja na siku za hivi karibuni kutoa boko sana kwenye hotuba zake lakini this time inaonekana kama Rais Samia ameanza kurudi kwenye mstari.

Kuna kauli ameitoa akiwa akiwa huko na Namtumbo, kauli ambayo bila shaka itachagiza wanawake wengi hasa wa vijijini kupiga kura kwenye uchaguzi ujao.

Wakati anazindua shule ya wasichana huko Namtumbo mkoani Ruvuma, Rais Samia amezungumzia kuhusu nishati safi ambapo amedokeza kuwa ana mpango wa kuwasaidia wanawake wengi kuacha kutumia kuni ili waanze kutumia nishati safi kama vile gesi n.k

Soma pia: Rais Samia Ameibeba Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia Kimataifa

Kwa wale ambao wameshaishi vijijini bila shaka watakuwa wanafahamu jinsi ambavyo matumizi ya kuni yanaathiri afya za wanawake na kauli hii ya Rais Samia ni kama imekuja kuwakomboa wanawake hao.

Rais Samia amesema:

Wanawake wa Afrika wanapata maradhi kwa sababu wanapikia kuni. Wanakufa na maradhi ya kupumua, wanapofua macho na hiyo ni kwa sababu kuni zinatoa gesi mbalimbali ambazo zinawapa madhara mama zetu, bibi zetu waliumia sana kwenye hilo. Sasa wakati umefika tubadilishe tutumie nishati safi za kupikia.
Kwa sababu mradi huu lengo lake ni kuwa ifikapo mwaka 2030, asilimia 80 ya watanzania wawe wanatumia nishati safi.


Kwenye hili, Rais ameupiga mwingi kwani wanawake wengi bila shaka watajitokeza kupiga kura ili waweze kujitoa kwenye matumizi ya kuni.

Nawasilisha
 
Pamoja na siku za hivi karibuni kutoa boko sana kwenye hotuba zake lakini this time inaonekana kama Rais Samia ameanza kurudi kwenye mstari.

Kuna kauli ameitoa akiwa akiwa huko na Namtumbo, kauli ambayo bila shaka itachagiza wanawake wengi hasa wa vijijini kupiga kura kwenye uchaguzi ujao.

Wakati anazindua shule ya wasichana huko Namtumbo mkoani Ruvuma, Rais Samia amezungumzia kuhusu nishati safi ambapo amedokeza kuwa ana mpango wa kuwasaidia wanawake wengi kuacha kutumia kuni ili waanze kutumia nishati safi kama vile gesi n.k

Kwa wale ambao wameshaishi vijijini bila shaka watakuwa wanafahamu jinsi ambavyo matumizi ya kuni yanaathiri afya za wanawake na kauli hii ya Rais Samia ni kama imekuja kuwakomboa wanawake hao.

Rais Samia amesema:




Kwenye hili, Rais ameupiga mwingi kwani wanawake wengi bila shaka watajitokeza kupiga kura ili waweze kujitoa kwenye matumizi ya kuni.

Nawasilisha
Wewe binafsi unaona kuna mazingira wezeshi na rafiki ya kiuchumi na kisera ambayo yatatoa nafasi kwa wanawake kutumia nishati safi ambayo ni Gesi asilia?

Kwanza hali ya kiuchumi ya Watanzania kumudu gharama za kununua gesi hasi gharama za kuanzia achilia mbali gharama za kuendeleza matumizi ikiwa ni pamoja na kufanya replacement? Au unavyoiona gesi mjini na matumizi yake ndivyo ilivyo katika maeneo mengine ya nchi ikiwemo vijijini?
 
Wewe binafsi unaona kuna mazingira wezeshi na rafiki ya kiuchumi na kisera ambayo yatatoa nafasi kwa wanawake kutumia nishati safi ambayo ni Gesi asilia?

Kwanza hali ya kiuchumi ya Watanzania kumudu gharama za kununua gesi hasi gharama za kuanzia achilia mbali gharama za kuendeleza matumizi ikiwa ni pamoja na kufanya replacement? Au unavyoiona gesi mjini na matumizi yake ndivyo ilivyo katika maeneo mengine ya nchi ikiwemo vijijini?

Mkuu mpango kama umesoma vizuri, unaenda mpaka 2030, we can make that assesment tukifika 2030.

Its unfair to ask those questions at this time when we are 6 years behind the deadline.

The fact that ameongelea inaonesha she cares and something is about to be done.

Mpe benefit of doubt
 
Mkuu mpango kama umesoma vizuri, unaenda mpaka 2030, we can make that assesment tukifika 2030.

Its unfair to ask those questions at this time when we are 6 years behind the deadline.

The fact that ameongelea inaonesha she cares and something is about to be done.

Mpe benefit of doubt
Huo mpango unakwenda kupunguza bei ya gas ya mtungi mdogo kufikia 8000?
 
Sorry naomba bei ya mtungi ukiwa tupu wa ⛽? (Kampuni yyte) MDOGO
Pia naomba bei ya mtungi ukiwa na ⛽ ndani?(Kampuni yyte) MKUBWA

Vuta picha ya vipato vya wanavijiji vya Tanganyika.
All the best
 
Mkuu mpango kama umesoma vizuri, unaenda mpaka 2030, we can make that assesment tukifika 2030.

Its unfair to ask those questions at this time when we are 6 years behind the deadline.

The fact that ameongelea inaonesha she cares and something is about to be done.

Mpe benefit of doubt
Siku zote wanasiasa wamekua ahadi ambazo ni impractical kwa ajili ya kukidhi matakwa yao kuchaguliwa tena na sio kuboresha maisha ya watu (quality of life improvement) kwa kutunga na kusimamia utekelezaji wa sera wezeshi na rafiki zinalonga kufikia uboreshaji huo wa maisha.

Nitakupa mifano hai na naamini wanaolewa mambo wataungana na mimi kwa kiasi kikubwa. walipokua kwenye kampeni ya kujenga JNHEPP walisema kwamba Tanzania itajitosheleza kwa umeme kwa kiasi kikubwa na hata ziada kuuzwa nje ili kufidia pamoja na mambo mengine gharama za ujenzi wa mradi ule sambamba na kushuka kwa bei ya umeme kwa maana ya gharama za uunganishaji na unit. Malengo hasa hapa iliku ni kuhakikisha upatikanaji (availability) uhakika (reliability) kufikika kwa maana ya kila mtu kupata (accesibility) na kuhimilika in terms of cost (rafordability). Ni dhahiri kwamba January na Maharagande walipoingia ofisini tulishhudia mabadiliko makubwa ikiwemo gharama za uunganishwaji wa umeme, pamoja na ongezeko la kodi ya jengo mpaka 1500 Kwa nyumba za kawaida kila mtu anunuapo umeme. Kumbe mtu wa kijijini akiwa na buku hawezi kupata umeme acha maswala ya gharama za kuunganishwa. Sasa kiuhalisia hii inakatisha tamaa matumizi ya umeme kama huduma bali imekua ni anasa. Sote tuanjua umuhimu wa HEP katika upatikanaji wa nishati safi ya kupikia.
Hakuna Jitihada zozote zinazofanyika ili kuondoa ugumu huo mpaka sasa isipokua wanapropaganda wamenata na beat kwa kulinganisha tanzania na nchi nyingine. Watu wakilinganisha na nchi nyingine katika mambo mazuri wanakua wakali
hali kadhalika bei ya gesi ya kutumia majumbani imezidi kupaa kila uchwao sasa hivi mtungi mdogo unauzwa kwa wastani wa tsh 50-60 elfu kwa mtu anayeanza na nusu yake kwa ghrama za re-filling. Ukipiga mahesabu ni dhahiri kwamba no affordability aspects inayofikiriwa na serikali kwa nia ya kumsaidia mwananchi au huyo mama kuhusu swala la nishati safi.
Badala ya kulipia goli la mama ingetengenezwa mechanism kusubsdize bei ya h=gesi ya kutumia majumbani ikihusisha pia adhabu kubwa ya faini kwa wachoma mkaa na fedha hizo zielekezwe kwenye mfuko wa nishati safi na watu wangehama by default sababu ya affordability.
Shida ni kwamba wenye biashara ya gesi ni wanasiasa na marafiki zao hivyo wanahamasisha biashara zao kwa mwamvuli wa nishati safi na sio political will ya kutatua changamoto husika practically.
adios
 
Kwamba % kadhaa wanawake wanakufa Kwa kupikia Kuni?

Hawana point nyingine tofauti na hii?
Mama yangu saivi ana miaka81 anaendesha Hadi baiskeli tumempelekea mtugi mdogo wa kupikia tangu tupeleke huu ni mwaka3 amebadirisha mara4 tu kwanza anasema ugali hauivi vzr mara nyingi wake zetu walienda ndo huenda kutumia.


Bibi kizaa baba alikuwa na miaka 97

Kizaa mama yeye alikufa na miaka 79 hatujamkuta.

Leo hii mnapikia gesi na umeme mnakufa na miaka mingapi?
 
Wewe binafsi unaona kuna mazingira wezeshi na rafiki ya kiuchumi na kisera ambayo yatatoa nafasi kwa wanawake kutumia nishati safi ambayo ni Gesi asilia?

Kwanza hali ya kiuchumi ya Watanzania kumudu gharama za kununua gesi hasi gharama za kuanzia achilia mbali gharama za kuendeleza matumizi ikiwa ni pamoja na kufanya replacement? Au unavyoiona gesi mjini na matumizi yake ndivyo ilivyo katika maeneo mengine ya nchi ikiwemo vijijini?
Tanzania hakuna uchaguzi bali kuna maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura. Sasa sijui ni wanawake gani unawaongelea.
 
Pamoja na siku za hivi karibuni kutoa boko sana kwenye hotuba zake lakini this time inaonekana kama Rais Samia ameanza kurudi kwenye mstari.

Kuna kauli ameitoa akiwa akiwa huko na Namtumbo, kauli ambayo bila shaka itachagiza wanawake wengi hasa wa vijijini kupiga kura kwenye uchaguzi ujao.

Wakati anazindua shule ya wasichana huko Namtumbo mkoani Ruvuma, Rais Samia amezungumzia kuhusu nishati safi ambapo amedokeza kuwa ana mpango wa kuwasaidia wanawake wengi kuacha kutumia kuni ili waanze kutumia nishati safi kama vile gesi n.k

Soma pia: Rais Samia Ameibeba Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia Kimataifa

Kwa wale ambao wameshaishi vijijini bila shaka watakuwa wanafahamu jinsi ambavyo matumizi ya kuni yanaathiri afya za wanawake na kauli hii ya Rais Samia ni kama imekuja kuwakomboa wanawake hao.

Rais Samia amesema:




Kwenye hili, Rais ameupiga mwingi kwani wanawake wengi bila shaka watajitokeza kupiga kura ili waweze kujitoa kwenye matumizi ya kuni.

Nawasilisha

..suluhisho ni bei ya mtungi wa gesi kuwa rahisi kuliko gunia la mkaa, au mzigo wa kuni?

..pia kama Stieglers imeanza kuzalisha umeme, bei inapaswa kupungua kwa sababu ni umeme unaozalishwa kwa maji.
 
Back
Top Bottom