Elections 2010 Kauli mbiu mpya ya JK 2010


Mkuu hapo haujaweka Mishahara na posho za Mawaziri 60 ambao si watendaji bali wanasiasa. Miradi ya kipuuzi kama vitambulisho, yaani unatumia mabilioni kwenye issue kipuuzi tu.

Kama tungeamua hasa kwa dhati kuwa makini na matumizi basi nchi kama TZ ilitakiwa kuwa na mawaziri wasiozidi 15 tu. wengine wote ni redundant!
 
Ifuatayo ni hotuba ambayo Rais Kikwete ameitoa leo Dodoma akitangaza nia yake ya kugomea tena Urais.

Je, Kikwete amewafanyia nini Watanzania kwenye kipindi cha miaka mitano iliyopita 2000-2010 ili kustahili apewe miaka mitano mingine? Naomba maoni yenu wana JF...



 
Hivi kuna mategemeo yoyote ya Chadema kuweka mgombea wa Urais na kumshinda Jakaya?Au ndiyo yale yale ya Vuvuzela?
 
Na wabongo wataimba hiyo tu, huruma!

Je ana maana kuwa madudu yote tuliyoyashuhudia toka aingie madarakani yataongezeka kwa ari zaidi nguvu zaidi na kasi zaidi - yaani tutegemee ufisadi zaidi, wizi zaidi, usanii zaidi na uzembe kama kazi au?

Yaani ari zaidi kwa safari kama za Vasco Dagama, matumizi kama ya mlevi vile na utawala usiojali sheria, wenye ubia na mafisadi na upendeleo kwa washikaji hadi 2015 ?

Mbona hapo tutakuwa tumeliwa au ndio tunajitafuna wenyewe kama mapunguani ? Talk of the dumb, the blind and the stupid, that's what we are for sure.
 
What Speed?

There is zero sense of urgency with anything the government does.

MORE CORRUPTION, MORE INCOMPETENCE, MORE LAZINESS
 
Ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi kwenye lipi?

Aliahidi kuipitia upya mikataba ya kuchimba dhahabu ambyo ilikuwa inalalamikiwa na Watanzania kwamba haina maslahi kwa Tanzania. Baada ya miaka mitano ya kuwepo madarakani bado tunaambulia 3% ya mapato yote yanayotokana na dhahabu yetu na wachukuaji kuendelea kufaidi 97%. Pamoja na kuongezeka kwa kiasi kikubwa kwa bei ya dhahabu katika soko la dunia ongezeko hilo halina manufaa yoyote kwa Watanzania wanaofaidi na Wachukuaji na shareholders wao.

Alipoingia madarakani wagonjwa wengi na hata waja wazito walikuwa ama wanashare vitanda au kulala chini na baada ya miaka mitano hakuna ahueni yoyote katika hali hii.

Alipoingia madarakani hospitali zetu nyingi zilikuwa hazina madawa au vitendea kazi muhimu nah ii kusababisha waheshimiwa wengi kukimbilia nje kwa ajili ya matibabu yao. Baada ya kuwepo madarakani kwa miaka mitano hali hii bado iko vile vile hakuna ahueni yoyote.

Alipoingia kulikuwa na manung'uniko mengi toka kwa Wafanyakazi wa sekta mbali mbali nchini kuhusu kuhusiana na mishahara midogo ambayo haiendani na hali halisi ya gharama za maisha hadi hii leo hakuna lolote lililofanywa la kuongeza mishahara ili ilingane na gharama halisi za maisha na kama mtakumbuka hivi karibuni kulikuwa na tishio la mgomo wa Wafanyakazi kote nchini. Kwa maneno mengine hili nalo pamoja na kuwepo madarakani miaka mitano halijafanyiwa kazi.

Alipoingia madarakani Wanafunzi wengi katika shule za msingi na sekondari katika mikoa yote nchini walikuwa wanakaa chini na na wengi hawana hata madarasa na hivyo kusomea chini ya miti. Halii hii baada ya kuwepo madarakani kwa miaka mitano haijapatiwa ufumbuzi wowote.

Alipoingia madarakani alisema atapambana na rushwa na ufisadi lakini hali nalo halijafanyiwa kazi maana rushwa badi imekithiri nchini na mafisadi wote waliohusika na EPA, Richmond, Kiwira, Ununuzi wa rada, Ununuzi wa ndege ya Rais na heli za jeshi n.k.

Alipoingia madarakani nchi ilikuwa na matatizo mengi ya umeme na upatikanaji maji safi kwa matumizi ya binadamu. Hadi hii leo baada ya kukaa madaraki kwa miaka mitano bado matatizo haya ni sugu na kero kubwa kwa Watanzania.

Sasa Rais anaposema "mmetutuma tumetekeleza" hivi ni kipi walichotekeleza ikiwa matatizo yote ambayo aliingia madaraka na kutakuta baada ya miaka mitano yako vile vile na hakuna ahueni yeyote?

Kama huu siyo usanii ndugu Watanzania sijui tuite nini!!! Kwanini CCM hawataki kuwa wakweli hata pale ambapo ukweli umedhihiri?
 
What???? naota au ni kweli!! Hivi tujiite ni wajinga tumekosa akili tumekosa uelewa au ni vipi? kazi ipo wajameni...
 
Hapo tayari Komba keshaitungia nyimbo!...na wabongo wataiandika hadi kwenye magari yao!...Ni kauli za kupitisha muda na kuhalalisha uwizi wa mchana kweupe!
 


Hivi ndani ya Sekretarieti ya Propaganda ya CCM kuna waimbaji wa taarabu wangapi? To hii kauli mbiu inanikumbusha nyimbo za Bi Hadija Kopa na Nasma Hamis!
 
Nani tumlaumu ? Ata angekuja na slogan mbaya kuliko tulizowahi kusikia lakini bado atachukua hiyo nafasi. Upinzani upinzani...upizani my a**
 
Katika WANASIASA HALISI wa Tanzania JK ni mmoja wao. Kila analolitamka ni GUMZO humu ndani na kwingineko!! Hii inanikumbusha enzi zile za Mwalimu kuanzia mwaka 1967 Azimio la Arusha lilipoanzishwa.

Tuliimba sana, tukatembea sana. Ikaja Mwongozo Mpya wa TANU, vijiji vya ujamaa, siasa ni kilimo, ambayo yoote aliondoka nayo madarakani hatimaye akafa nayo.
 

"Mvinyo wa Zamani Ndani Ya Chupa Mpya" Hakuna dodose hapo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…