Kauli ya Benchikha kuhusu usajili Simba

Kauli ya Benchikha kuhusu usajili Simba

Metronidazole 400mg

JF-Expert Member
Joined
Aug 25, 2016
Posts
941
Reaction score
2,062
Kocha Mkuu wa Simba SC, Abdelhak Benchikha ametoa onyo kwa mastaa wa klabu hiyo, ambao wamepewa nafasi nyingi kupitia michuano ya Mapinduzi ambao walikuwa hawapati nafasi ya kucheza kuitumia vyema ili kumshawishi kuweza kuingia katika kikosi chake akiwemo nyota Moses Phiri.

Phiri tangu kuanza kwa msimu huu amekuwa hapati nafasi ya kutosha huku kwenye michuano ya Mapinduzi inayoendelea kutimua vumbi visiwani Zanzibar amekuwa akipewa nafasi mara kwa mara na amefanikiwa kufunga bao moja.

Kocha Benchikha amesema: “Kwa wale wachezaji wote ambao walikuwa hawapati nafasi ya kucheza mara kwa mara, tumejaribu kuwapa nafasi ya kutosha ili waweze kuonyesha mabadiliko na kulishawishi benchi la ufundi.

“Kwa hali nyingine, hii ni kawaida lakini kwa wachezaji wanatakiwa kupambana ili kuleta ushindani wa namba na hapo itakuwa ni faida ya timu kwa kuwa maendeleo yatakuwa yanapatikana kupitia wachezaji kujituma, ili walinde nafasi zao.

“Sisi kama Simba SC na ukubwa wa hii timu, hatutaki kuona mchezaji anajihajikishia namba kwani tunataka ushindani na ndio maana wamepewa nafasi kupitia hii michuano ili waweze kulishawishi benchi la ufundi” amesema kocha huyo.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari yako inahusiana Nini sasa na usajili??
 
20231231_220832.jpg
 
Kocha Mkuu wa Simba SC, Abdelhak Benchikha ametoa onyo kwa mastaa wa klabu hiyo, ambao wamepewa nafasi nyingi kupitia michuano ya Mapinduzi ambao walikuwa hawapati nafasi ya kucheza kuitumia vyema ili kumshawishi kuweza kuingia katika kikosi chake akiwemo nyota Moses Phiri.

Phiri tangu kuanza kwa msimu huu amekuwa hapati nafasi ya kutosha huku kwenye michuano ya Mapinduzi inayoendelea kutimua vumbi visiwani Zanzibar amekuwa akipewa nafasi mara kwa mara na amefanikiwa kufunga bao moja.

Kocha Benchikha amesema: “Kwa wale wachezaji wote ambao walikuwa hawapati nafasi ya kucheza mara kwa mara, tumejaribu kuwapa nafasi ya kutosha ili waweze kuonyesha mabadiliko na kulishawishi benchi la ufundi.

“Kwa hali nyingine, hii ni kawaida lakini kwa wachezaji wanatakiwa kupambana ili kuleta ushindani wa namba na hapo itakuwa ni faida ya timu kwa kuwa maendeleo yatakuwa yanapatikana kupitia wachezaji kujituma, ili walinde nafasi zao.

“Sisi kama Simba SC na ukubwa wa hii timu, hatutaki kuona mchezaji anajihajikishia namba kwani tunataka ushindani na ndio maana wamepewa nafasi kupitia hii michuano ili waweze kulishawishi benchi la ufundi” amesema kocha huyo.


Sent using Jamii Forums mobile app
sawa ila tunacho know,hafiki easter...
 
Back
Top Bottom