Kauli ya Lissu kwamba haki ya kupiga kura sio ya kikatiba inahitaji ufafanuzi zaidi wa kisheria

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Nimemsikia Tundu Lissu katika mahojiano yake na moja ya chombo cha habari akidai kwamba haki ya kuchagua katika katiba iliyo ibara ya 5 sio haki ya kikatiba na haiwezi kudaiwa mahakamani kwa sababu haijawekwa kati ya ibara ya 12 hadi 30 ya katiba!

Hakufafanua zaidi ina maana gani haki kuwepo katika katiba halafu isiwe haki ya kikatiba inayoweza kudaiwa mahakamani. Anasema mtu huwezi kwenda mahakamani kudai umenyimwa haki ya kuandikishwa kupiga kura!

Wataalamu wa sheria, inamaanisha nini Tundu Lissu anaposema haki za kikatiba zipo kuanzia ibara ya 12 hadi 30?
 
Kwamba hili nalo ni la kubishania? Wewe ukinyimwa kujiandikisha sheria gani inakuruhusu kwenda kushitaki serikali?
 
Mbona nawe hujaitolea ufafanuzi umejibu juu juu tu?

Umeona ilivyo ngumu kujibu in details?

Nawewe ungetaka mwenzako ajibu hivi basi ungemuomba mwandishi amuulize kama mimi nilivyofanya kwako.
😂😂😂

Happy New Year
 
Ni haki ya kikatiba provided vigezo na masharti mengine ya Katiba yamezingatiwa. Kwa mfano, Ibara 5(1) lazima itumike sanjari na Ibara 5(2). Soma exceptions zilizobainishwa kwenye Ibara 5(2).
 
Ni haki ya kikatiba provided vigezo na masharti mengine ya Katiba yamezingatiwa. Kwa mfano, Ibara 5(1) lazima itumike sanjari na Ibara 5(2). Soma exceptions zilizobainishwa kwenye Ibara 5(2).

Ibara 5(2)
Kama mtu amenyimwa haki ya kuandikishwa katika daftari la kupiga kura au kupiga kura kabisa anaweza kwenda mahakamani kudai hiyo haki??
 
Kama mtu amenyimwa haki ya kuandikishwa au kupiga kura anaweza kwenda mahakamani kudai hiyo haki??
Anaweza, kama anakidhi masharti mengine yote! Mwenye ugonjwa wa akili au mwenye uraia wa nchi nyingine, kwa mfano, hakidhi vigezo; kwa hiyo, hawezi kuidai hiyo haki mahakamani.
 
Nchi kama Brasil, Australia, Belgium, equador , Argentina na nyinginezo, kupiga kura ni jambo la haki na lazima kwa kila mmoja kwa mujibu wa sheria na katiba zao. Ikitokea uchaguzi umefanyika haafu kuna watu hawakupiga kura watu hao huchukiliwa hatua ikiwemo kupigwa faini.

Tanzania uchaguzi ndiyo haki kikatiba lakini kupiga kura ni maamuzi ya mtu
 
Unachanganya right (haki) na obligation (wajibu). You do not get punished for not exercising your right, lakini unaweza kuadhibiwa kwa kutotimiza wajibu wako!
 
Tundu lissu hapigi kura bongo wala hajajiandikisha!
 
Hii kitu kama tunaanza kufunguliwa macho vileee,mmmmhhh
 
Katiba ya Tanzania ina tabia ya kutoa haki kwa mkono mmoja na kuiondoa kwa mkono mwingine.

So possibly anasema kuna sehemu hiyo haki imekuwa contradicted?

Weka video/audio clip tusikie maneno yake mwenyewe.
 
Wakili msomi Pascal Mayalla au Mr Katiba pitia hapa..
 
Wakili msomi Pascal Mayalla au Mr Katiba pitia hapa..
Sheria ni fani bahari, japo ki umri, TAL ni mdogo wangu, lakini kwenye fani, mimi ni very junior kwa TAL, ila kiukweli kwenye mambo ya kutafsiri vifungu vya katiba, TAL atasubiri!. He is not right at all!.


P
 
Ha ha kwa hili umeingia Chaka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…