Uchaguzi 2020 Kauli ya Membe leo imedhihirisha kuwa Tundu Lissu hatunaye tena kwenye uchaguzi ujao

Kwani sheria inasemaje? Kuna sheria kweli inayomtaka mtia nia kwenda kimya kimya kutafuta wadhamini? Mara nyingi nimemsikia TAL akilizungumzia hili kwamba kabla ya mtia nia hajapitishwa na NEC yale anayoyatamka haiwezi kutafsirika (kisheria) kuwa ni kufanya kampeni kabla ya wakati!

Kuhusu Membe kuna mambo ya kuangaliwa na yananifanya nikitilie mashaka ACT-Wazalen na shaka yangu huenda ipo kwa Chadema
siku Membe anachukua fomu NEC yule mwanadada wa publicity wa ACT alizungumza kwa namna ya kumwonyeha TAL hafai apo hakumtaja (Tafuta taarifa ya habari ya ITV iku hiyo)

Kwa kuwa Zito amewahi kutumiwa na akina Jack Zoka na Membe amefanya na akina Jack Zoka ni rahisi kuhitimisha kwamba ACT-Wazalen ni chombo kinachotumiwa tu na kitengo, na ili kutaka kuJua fuatilia mahuiano ya Zitto na
 
Kampeni ni kampeni na kutafuta wadhamini ni kutafuta wadhamini. Hivyo viwili ni tofauti.

Lissu alikuwa mfu aliyefufuka. Kila anapokwenda watu wana nia ya kumwona na kusalimiana naye.

Hiyo ndiyo tofauti kuu kati ya Lissu na wagombea wengine.

Membe anajizungumzia yeye kama mtu ambaye hakuwa mfu.

Suala la Lissu ni tofauti hayupo asiiyeijua tofauti hiyo.
 
Watanzania tuache kukumbatia ujinga. Hivi yule mkurugenzi aliyempa fomu mtu ambaye hata yeye mwenyewe hamjui sababu ilikuwa CDM wameanza kampeni mapema? Au sugu alivyokamatwa akiwa anajukua fomu sababu ilikuwa ameanza kampeni mapema au alimtukana Tulia Akson?? Tuache ujinga badala ya kupinga udhalimu tunashabikia. Shule za kata zina madhara makubwa sana. Heading "kauli ya membe leo imedhihirisha kuwa TL hatunaye tena." Ndani unaanza kuuliza maswali hizi aakili au matope!!
 
Si tunaambiwa ni mwanasheria mbobezi ina maana sheria,taratibu na kanuni za uchaguzi hazifahamu?
 
Kwaiyo mfu wake ndio asifuate sheria,taratibu na kanuni za uchaguzi?
 
Mapingamizi halali kisheria dhidi ya mgombea nafasi ya Urais
 
TUME ILISHATANGAZA KUANZA KWA KAMPENI KWANI? Kama ni kupokelewa na watu si hoja.Mbona mla mahindi barabarani amekuwa akifanya kampeni tangu 2015 ???Hofu itawaua ccm.
 
TUME ILISHATANGAZA KUANZA KWA KAMPENI KWANI? Kama ni kupokelewa na watu si hoja.Mbona mla mahindi barabarani amekuwa akifanya kampeni tangu 2015 ???Hofu itawaua ccm.
Tatizo mnapenda kushindana na mtu anae washinda kwanza mwenzenu ni Rais mjue nyie wahun wa chadema kuwen na Adabu

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Lissu hawezi kukatwa hata kama amevunja sheria izo mnazosema

Na ikitokea ikawa ivyo,basi amini kwamba Tanzania itaenda kuweka rekodi mpya ya umwagaji damu kipindi chote cha kampeni.
Nchi imwage damu kw watu wachache wapuuzi wenye uchu wa madaraka ?? Acheni nyimbo za ndotoni .....hii nchi tupo pia tusiokuwa na vyama ila tunaangalia nani ana nia na uthubutu kwa nchi yake,


Wengi wenu mna mahaba tu na vyama.
 
Tatizo mnapenda kushindana na mtu anae washinda kwanza mwenzenu ni Rais mjue nyie wahun wa chadema kuwen na Adabu

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
Watu aina yako ndiyo mnarudisha nyuma juhudi chanya za kuleta uhuru wa kweli,haki na usawa. Kama ni rais ndiyo afanye chochote? Mungu angeweza kuifutilia mbali dunia hii kwa "maudhi" tufanyayo wanadamu lakini anatuacha.Sembuse huyo jamaa yule???
 

YAFAHAMU MAPINGAMIZI HALALI YA KISHERIA AMBAYO ANAWEZA AKAWEKEWA MGOMBEA WA NAFASI YA URAIS NCHINI TANZANIA.

Wiki ijayo tarehe 26 August, 2020 itakuwa ni siku ya wagombea kuwasilisha mapingamizi dhidi ya wagombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mapingamizi halali kisheria anayoweza kuwekewa mgombea wa nafasi ya Urais kwa mujibu wa masharti ya ya Kifungu cha 35 D na 40 (1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura 343 yakisomeka kwa pamoja na (read in tendem with) masharti ya Kanuni ya 39 (4) ya Kanuni za Uchaguzi wa Rais na Wabunge, 2020 (Tangazo la Serikali Na. 402 la 2020) ni haya yafuatayo;

(1) Mgombea Urais sio raia wa Tanzania.

(2) Mgombea Urais hajafikisha umri wa miaka 40.

(3) Mgombea Urais hajui kusoma na kuandika Kiswahili au Kiingereza.

(4) Mgombea Urais sio mwanachama wa chama cha siasa.

(5) Mgombea Urais hajadhaminiwa na chama cha siasa kugombea.

(6) Mgombea Urais amekutwa na hatia ya kosa la jinai la kukwepa kodi katika kipindi cha miaka 5 kabla ya siku ya Uchaguzi.

(7) Mgombea Urais hajadhaminiwa na wapiga kura 200 kutoka mikoa 10 ya Tanzania ikiwemo mikoa 2 kutoka Zanzibar.

(8) Mgombea Urais hajadhaminiwa na idadi ya kutosha ya wapiga kura.

(9) Mgombea Urais hakulipa dhamana ya Tshs 1, 000, 000/=

(10) Mgombea Urais hakuwasilisha au hakuambatinisha picha kwenye Fomu ya Uteuzi.

(11) Mgombea Urais ameshindwa kuambatanisha Tangazo la Kisheria (statutory declaration) kwenye Fomu ya uteuzi ambalo limesainiwa na mgombea na limefanywa mbele ya Jaji kudhibitisha kuwa mgombea anayo nia na anazo sifa za kugombea Urais.

(12) Mgombea Urais ameshindwa kuweka wazi pesa ambazo atazitumia katika uchaguzi.

(13) Mgombea Urais hakusaini kukubali kutii Maadili ya Uchaguzi.

(14) Mgombea Urais hakujaza au hakurudisha Fomu ya Uteuzi kwa Tume ya Taifa Uchaguzi kwa mujibu wa matakwa ya sheria.

(15) Mgombea Urais amefanya makosa ambayo yamezuiliwa na Sheria ya Gharama za Uchaguzi, 2010.

(16) Kutokana na taarifa ambazo ziko kwenye Fomu yake ya Uteuzi, mgombea hana sifa za kuwa mgombea wa nafasi ya Ubunge au mjumbe wa baraza la wawakilishi la Zanzibar zilizoainishwa na Katiba husika.

(17) Taarifa ambazo mgombea Urais amewasilisha kwa Tume ya Taifa uchaguzi hazijitoshelezi kumtambua mgombea.

(18) Kutokana na taarifa ambazo ziko kwenye Fomu yake ya Uteuzi, hana sifa za kuwa mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zilizoainishwa na Katiba.

Haya ndo mapingamizi 18 pekee ambayo anaweza kuwekewa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sio vinginevyo.
 
Watu aina yako ndiyo mnarudisha nyuma juhudi chanya za kuleta uhuru wa kweli,haki na usawa. Kama ni rais ndiyo afanye chochote? Mungu angeweza kuifutilia mbali dunia hii kwa "maudhi" tufanyayo wanadamu lakini anatuacha.Sembuse huyo jamaa yule???
Kuna mipaka kila sehem ukitaka kushindana na mtu mwenye kukushinda jua utaangukia pua lisu angefanya siasa zake bila kumtukana mtu unafikir haya yangekuwepo

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Zitto, Membe, na ACT ni wachezaji wa kutegemewa wa CCM, tofauti ni rangi tu.
 
Wamwache agombee,,sheria haisemi kuongozana na watu au kuwahutubia ni kampeni,,ile ni mikutano tu
Unaonekana una busara sana mkuu hata katika uhalisia wako. Mbona kuna wengine wamevaa ngozi ya kijani hadi busara zimewatoka?
 
1.Umesahau wale wasanii wanamuziki 200 waliotumbuiza na kumpigia kampeni magufuli pale DSM,au CCM ndio wanaruhusiwa tu kufanya kampeni.kama ishu ni kuanza kampeni mapema.
2.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…