Kauli ya Waziri Mkuu kutilia shaka barakoa za kisasa na kutaka watu wajishonee matambara na kuyavaa usoni haiwezi kuachwa bila kujadiliwa

Hivi Tanzania inapambana na Wazungu au na Corona? Mbona mnatuchanganya?
 
Hapa ndio napata taabu sana kuona tangu lini maskini hakawa na adui
 
Kwa kutapatapa boss alionyesha mashaka, ni kawaida yao kusisitiza, asionekane yuko tofuti nae,
Dawa zote aidha vifaa vya kutengeneza vinatoka nje, iwe leo barakoa hatari.
Ni tatizo kutoa kauli ukimchungulia boss ili kumjenga mbele ya umma! Huko hata mwenyewe kauli za boss uziamini ila unazisisitiza!
 
Hii ngumu kumeza lakini ndiyo ukweli wenyewe
 
Acha ujinga wewe!
Kutumia barakoa kutoka nje ya nchi kuna hasara nyingi. Moja ni kwamba barakoa zaweza kutumika kuleta corona. Pili hasara ya capital flight. Tutengeneze barakoa zetu.
 
Hapo anatumia busara kuhakikisha anatembea na biti za wabuza Jiwe.
 
Acha ujinga wewe!
Kutumia barakoa kutoka nje ya nchi kuna hasara nyingi. Moja ni kwamba barakoa zaweza kutumika kuleta corona. Pili hasara ya capital flight. Tutengeneze barakoa zetu.
Sawa basi tungeanza na
1. Condomu
2. Miswaki
3. Tooth pick
4. Dawa za malaria
5. Dawa za Ukimwi
6. Dawa za magonjwa yote yanayosababishwa na kujamiana
7. Dawa za aina za cancer kama iliyoumuondoa Rais wetu Kambarage Nyerere
.






.

Ongezea mwenyewe

Bila kusahau kurudi kwenye tiba asilia.
Tuokoe hela sio kwenye barakoa tu.
Ipi muhimu condom au barakoa.
 
Kazi ya TBS Ni nini Sasa.

Pili, nijuavyo mimi kiongozi mkubwa Kama Waziri Mkuu kutoa kauli Kama hiyo Ni lazima kuna taarifa nyeti anazo kuhusu hiyo bidhaa. Sidhani km aliropoka

Tatu, inaweza kuwa ni kauli iliyojaa wasiwasi ya kutilia mashaka hizo barakoa kutokana na msimamo wa serikali yetu unaopingana na mabeberu. Hivyo PM akaona wanaweza kupitia barakoa wakasambaza hao virusi kuhakikisha maambukizi yanakuwa juu ili kuonyesha dunia jinsi Serikali ya Tanzania ilivyofeli ktk suala la korona.

Ikumbukwe kwamba walitengeneza tatizo na tatizo limekuwa kubwa, na tumerudi kwao kuomba suluhisho. Suluhisho Ni kukuuwa na pia kutengeneza chanjo na kuuzia na kutengeneza mapato makubwa.

Unalipa mabilioni kununua chanjo iliyobeba mauti yako mwenyewe .
 
Hii haitufanyi kuacha kuchukua tahadhari.
 
Jiwe amemfanya kila msaidizi wake kuwa juha
Kama Kuna ambazo huziamini si jenga kiwanda chako haraka haraka kwa kutumia Suma JKT kama ulivyofanya Mirerani au ofisi za Dodoma?
Pia unaweza kuziagiza na kupimwa TBS toka nchi unayona haina hicho anachokiita Vita uchumi na sisi?
Amefeli vibaya sana.
 
Hii nchi ipo mikononi kwa wahuni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…