Kauziwa rice cooker Tsh. 300,000 na Waturuki, kaikuta inauzwa Tsh. 140,000 Mlimani City. Anawaza amalizie hela yao ama?

Kabla ya kufanya manunuzi window shopping muhimu

Ova
Hata Kariakoo ukienda kichwa kichwa unapigwa haswa, unakuja shtuka ushalipa. Madukani siku hizi vishoka wengi sana. Ili usipigwe hakikisha umepitia mitandaoni, kisha zama dukani afu linganisha bei zao
 
Hata karume shati ya kutundikwa juu utauziwa elf 15 posta mpya elf 30,ukienda karume zilizomwagwa chini unapata Kwa elf 2
 
Sasa ulitaka akopeshwe Kwa bei ya kuuza?
Faida itoke wap
 
Mkuu ni makubaliano yako na wao! Kama huna mazoea ya kutembele madukani mara kwa mara wakikuletea nyumbani unajikuta umechukua bidhaa yao kwa mkopo!
 

sema kakopeshwa
 
Daah wabongo mnalalamika mno aisee...ulitaka Mturuki akukopeshe bila hata kuweka maji kidogo hapo umeenda Mlimani City ukienda Shanghai utaanzisha uzi majukwaa yote..
 
Hawa wanaotembeza bidhaa makazini kwa mikopo wanajua kuna watumishi ambao wako busy hawapati muda wa kuingia madukani hivyo wanauza bei za kitapeli hujawahi ona.
Kitu cha elfu 60 unauziwa laki na 40, ni kawaida yao
 
Ila Kuna mambo ya hovyo sana yaan raia wa kigeni anakuja kufanya umachinga ambao sisi wenyewe tunaweza fanya.Nacho jiuliza wao katika nchi za wanaweza kubali sisi tufanye biashara hizo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…