Nilikuwa najaribu kupata takwimu kwenye website ya NECTa lakini haifunguki.Nanukuu kutoka kwenye gazeti ka mwananchi
"...MATOKEO ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika mwaka jana yametangazwa. Watahiniwa 240,903 sawa na asilimia 60.6 wamepata sifuri, ...
Akitangaza matokeo hayo jana, Waziri wa Elimu Dk Shukuru Kawambwa alisema watahiniwa walikuwa 456,137..."
....
Tuko!Nanukuu kutoka kwenye gazeti ka mwananchi
"...MATOKEO ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika mwaka jana yametangazwa. Watahiniwa 240,903 sawa na asilimia 60.6 wamepata sifuri, ...
Akitangaza matokeo hayo jana, Waziri wa Elimu Dk Shukuru Kawambwa alisema watahiniwa walikuwa 456,137..."
Hii 60.6% inatoka wapi?
Maana 240903/456137 x 100% = 52.8%
Nimeona hata baadhi ya vyombo vingine vya habari vimeripoti namba hizo hizo...
Someone to clarify?...
Yaani hii kitu sio ya kuchekelea hata kidogo ulivyojichanganya hapo kwenye RED ndo hivyo hivyo Kawambwa nae kajichanganya usipime yaani 94% wamefeli? kudagadeki mwakaa jana ilikua 91% tutegemee mwakani kuwa 97% baada ya hapo 2015 watakaofeli watakua 100% hii ndo nchi Kikwete anatuachia, na hii EAC kudagdeki watotot wetu watakua manamba tu kwenye Ardhi yao !Mkuu usishanagae kwani ingekuwa 52% wamefeli unafikiri haya ni matokeo mazuri. Kwa mtazamo wangu wote waliopata DIV 0 na IV wote wamefeli ukitafuta wastani utakuta waliofeli ni 94% na waliofaulu ni kama 0.43% aibu kubwa ndugu zangu. Hili ni janga lingine la kitaifa. Haya pia ni matokeo ya serikali kupuuza matakwa ya waalimu. Bila CCM kutoka madarakani hakika tutaendelea kuumia milele. Wote tukatae hili 2015 tufanye mabadiliko maana kila sehemu tunaumizwa na hii serikali ya CCM.
mkuu uko sahihi vijana wamefail sana ni aibu sana kwa taifa letu siasa ni adui wa elimu yetu. Na cha ajabu sana hakuja hata na solution ya nini klifanyike. nilitegemea ameona wananfunzi wamefail sana sasa kama waziri mwenye PhD holder angekuja na nini kifanyike na sikutangaza tu na kualalamika kuwa shule hazikuwa na walimu, maabara, na pengine bila kujua kiini hasa cha tatizo.Masahihisho: Waliopata ZERO ni 68.1% na sio 60%. Calculation zinatokana na school candidates waliofanya mtihani na sio waliojiandikisha kufanya mtihani.
Toka Gazeti la Mwananchi.
Alisema watahiniwa wa shule (school candidates) walikuwa 397,136 sawa na asilimia 96.57, miongoni mwao, 14,090 sawa na asilimia 3.43 hawakufanya mtihani huo kutokana na sababu mbalimbali zikiwamo utoro, ugonjwa na vifo.
Ufaulu kwa madaraja
Kwa mujibu wa matokeo hayo, watahiniwa waliopata daraja la kwanza ni 1,641, wavulana wakiwa 1,073 na wasichana 568, daraja la pili ni 6,453, wavulana wakiwa 4,456 na wasichana 1,997.
Waliopata daraja la tatu ni 15,426, wavulana 10,813 na wasichana 4,613, waliopata wa daraja la nne 103,327, wavulana 64,344 na wasichana 38,983 huku waliopata sifuri wakiwa 240,903, wavulana 120,664 na wasichana 120,239.
Kwa watahiniwa wa shule(school candidates) waliofanya exams walikuwa 397,136, I=1,641, II=6,453, III=15,426, IV=103,327. Jumla ya I-IV=126,847; Hivyo basi Zero ni 397,136 - 126,847=270,289. Hivyo asilimia ya ZERO ni 68.1. Ukichanganya ZERO na IV ni asilimia 94.1, ikiwa na maana kuwa waliopata I-III ni 5.9%.
Unaamua kumdhalilisha ------ wa Bagamoyo [/INDENT]
WanaJF!Napenda kufahamu hivi jina la kabila hapa JF ni matusi;
Hapo kwenye vidashi niliandika kabla la mhe Waziri wa elimu:
Naomba kufahamishwa nisije nikala BAN kwa kuandika makabila ya watu.Je ni makabila yote au ni kwa kabila la KWE.RE tu ndio ambalo linakuwa censored.
Nawasilisha;Bazazi!