Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hata kama ikirekebishwa Matokeo ni Kilio na Msiba wa Taiffa..
Hata kama ungekuwa ni ww lazma uchanganyikiwe......hari mbaya
Waliofanya mtihani walikuwa 399,000 kwa hesabu za haraka...
Nilikuwa najaribu kupata takwimu kwenye website ya NECTa lakini haifunguki.
Kwa haraka haraka nilihisi kuwa huenda hiyo 456,137 ni registered candidates, na kwa kuwa huwa wanakuwapo some absent students, huenda waliofanya mtihani ni less than registered students, so kama denominator itakuwa less than 456,137 basi hata percentage itapanda juu kidogo na kufikia hiyo 60.6%. Ni hisia tu, ningepata figure zote ningejiridhisha, ila sasa website ya matokeo haifunguki
napita tuu wakuu
Itasaidia?
Kehasema wasichana wamefeli sababu ya wanamme!
Pity shame, Hapa ndo tunamkumbuka Mbatia, yaani kaja na mswaada wa kuboresha Elimu magamba wa kaupiga chini, Watanzania tuwe makini hakuna nchi inaweza kufelisha hivi yaani waliofaulu ambao wanaweza kwenda kidato cha tanoi ni 5.9% na hii yote 94% ieende mtaani hili ni bomu tumelitengeneza. Waziri wa Elimu hatakiwi kukaa pale ! Aibu aibu aibu
WanaJF!Napenda kufahamu hivi jina la kabila hapa JF ni matusi;
Hapo kwenye vidashi niliandika kabla la mhe Waziri wa elimu:
Naomba kufahamishwa nisije nikala BAN kwa kuandika makabila ya watu.Je ni makabila yote au ni kwa kabila la KWE.RE tu ndio ambalo linakuwa censored.
Nawasilisha;Bazazi!
hebu nijaribu;mchagga (Kilimanjaro), mhaya (bukoba), mkurya (mara), ------ (bagamoyo), mzaramo (kisarawe)
Hiyo 456,137 ni yale waliostahili kufanya mtihani yaani registered ila waliofanya ni 1641+6495+15,426+103,327+240,903Nanukuu kutoka kwenye gazeti ka mwananchi
"...MATOKEO ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika mwaka jana yametangazwa. Watahiniwa 240,903 sawa na asilimia 60.6 wamepata sifuri, ...
Akitangaza matokeo hayo jana, Waziri wa Elimu Dk Shukuru Kawambwa alisema watahiniwa walikuwa 456,137..."
Hii 60.6% inatoka wapi?
Maana 240903/456137 x 100% = 52.8%
Nimeona hata baadhi ya vyombo vingine vya habari vimeripoti namba hizo hizo...
Someone to clarify?...
Hiyo 456,137 ni yale waliostahili kufanya mtihani yaani registered ila waliofanya ni 1641+6495+15,426+103,327+240,903
Huyu jamaa ni kimeo, nakumbuka swala la mitaala, akakanusha, lakini cha kushangaza mkurugenzi wa taasisi ya elimu akajiuzulu, sasa kwanin alijiuzulu , kama kweli ile mitaala ilikuwa halali?
Ukisoma hilo hilo mwanachi chini baada ya hiyo uliyo quote utakutana na hiiHapana...
Soma hii sehemu ya habari ya mwananchi hapa chini...
[Dk Kawambwa alisema watahiniwa wote kwa ujumla waliosajiliwa walikuwa 480,036 kati yao wasichana 217,583 sawa na asilimia 45.33 na wavulana 262,453 sawa na asilimia 54.67 lakini waliofanya mtihani huo ni 456,137 sawa na asilimia 95.44, wengine 21,820 (asilimia 4.55) hawakufanya mtihani.]
Alafu, ukichukua hao 456,137 waliofanya ukajumlisha na 21,820 waliofanya, unapata 477, 957. Sasa hao 2079 ambao hawapo kwenye hiyo hesabu, sijui wako wapi!!!
Yaani hii kitu sio ya kuchekelea hata kidogo ulivyojichanganya hapo kwenye RED ndo hivyo hivyo Kawambwa nae kajichanganya usipime yaani 94% wamefeli? kudagadeki mwakaa jana ilikua 91% tutegemee mwakani kuwa 97% baada ya hapo 2015 watakaofeli watakua 100% hii ndo nchi Kikwete anatuachia, na hii EAC kudagdeki watotot wetu watakua manamba tu kwenye Ardhi yao !
Pity shame, Hapa ndo tunamkumbuka Mbatia, yaani kaja na mswaada wa kuboresha Elimu magamba wa kaupiga chini, Watanzania tuwe makini hakuna nchi inaweza kufelisha hivi yaani waliofaulu ambao wanaweza kwenda kidato cha tanoi ni 5.9% na hii yote 94% ieende mtaani hili ni bomu tumelitengeneza. Waziri wa Elimu hatakiwi kukaa pale ! Aibu aibu aibu
tatu nibora wanafunzi walio fail wapelekwe vyuo vya ufundi agalau wanaweza pata kitu cha kusaidia katika maisha yake
Masahihisho: Waliopata ZERO ni 68.1% na sio 60%. Calculation zinatokana na school candidates waliofanya mtihani na sio waliojiandikisha kufanya mtihani.
Toka Gazeti la Mwananchi.
Alisema watahiniwa wa shule (school candidates) walikuwa 397,136 sawa na asilimia 96.57, miongoni mwao, 14,090 sawa na asilimia 3.43 hawakufanya mtihani huo kutokana na sababu mbalimbali zikiwamo utoro, ugonjwa na vifo.
Ufaulu kwa madaraja
Kwa mujibu wa matokeo hayo, watahiniwa waliopata daraja la kwanza ni 1,641, wavulana wakiwa 1,073 na wasichana 568, daraja la pili ni 6,453, wavulana wakiwa 4,456 na wasichana 1,997.
Waliopata daraja la tatu ni 15,426, wavulana 10,813 na wasichana 4,613, waliopata wa daraja la nne 103,327, wavulana 64,344 na wasichana 38,983 huku waliopata sifuri wakiwa 240,903, wavulana 120,664 na wasichana 120,239.
Kwa watahiniwa wa shule(school candidates) waliofanya exams walikuwa 397,136, I=1,641, II=6,453, III=15,426, IV=103,327. Jumla ya I-IV=126,847; Hivyo basi Zero ni 397,136 - 126,847=270,289. Hivyo asilimia ya ZERO ni 68.1. Ukichanganya ZERO na IV ni asilimia 94.1, ikiwa na maana kuwa waliopata I-III ni 5.9%.
Siyo mjadala. Hapa bunge lijiuzuru lote, baraza la mawaziri livunjwe, uchaguze uitishwe wa haraka. tupate serikali mpya then ndiyo tufanye mjadala wa kitaifa wa kujadili ustakabali wa elimu ya nchi yetu. Hii sasa hivi siyo serikali sikivu.Mkuu naunga mkono hoja 100%. Sasa hili sii tatizo la wizara ya elimu peke yake tena. Ni tatizo la kila mwananchi mwenye mapenzi mema na hii nchi. Tungetakiwa tuliwajibishe bunge na serikali kwa kushindwa kutetea maslahi ya mtanzania. Mbaya zaidi, zaidi ya asilimia 20 ya bajeti ya Tanzania kwa sasa imeelekezwa kwenye elimu. Hivyo ni kusema kwamba, karibu asimia 20 ya bajeti ya Tanzania inatumika kuzalisha sifuri!!! Hii ni hatari kwa ustawi wa Taifa. Mjadala wa kitaifa kuhusu ubora wa elimu yetu haukwepeki!
Nanukuu kutoka kwenye gazeti ka mwananchi
"...MATOKEO ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika mwaka jana yametangazwa. Watahiniwa 240,903 sawa na asilimia 60.6 wamepata sifuri, ...
Akitangaza matokeo hayo jana, Waziri wa Elimu Dk Shukuru Kawambwa alisema watahiniwa walikuwa 456,137..."
Hii 60.6% inatoka wapi?
Maana 240903/456137 x 100% = 52.8%
Nimeona hata baadhi ya vyombo vingine vya habari vimeripoti namba hizo hizo...
Someone to clarify?...