Kaze arudi Yanga haraka iwezekanavyo!

netein

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2019
Posts
281
Reaction score
480
Kuna tetesi nimesikia huyu mtaalam viongozi wa Yanga wanataka kumrudisha kama kocha msaidizi.

Naunga mkono hili sababu moja kuu Kaze anajua lugha nyingi kifaransa, kiingereza, kiswahili, Kirundi, kijeruman nk. Hii itawasaidia hata wachezaji wetu wa kibongo kwenye mawasiliano na kuimarisha viwango vyao.
 
fact mkuu
 
Si alikuwepo hapo Yanga. Ilikuwaje mkamtimua huku mkijua anaongea Lugha zote hizo?.

Tatizo ni Lugha, Kushindana na Simba au Uwezo wa kufundisha?

Halafu hapo Yanga si kuna kocha Profesa? Nyie si mlishaachana na Makocha wenye Diploma
 
Bhoo,,baada ya Nabi kutimuliwa tegemea Papa Zahera kupewa mikoba,Bhoo unajua Yanga ni watu wa kukurupuka miaka yote.
 
Kwa hiyo mnaanza kula matapishi mkuu
 
Timu imecheza mechi na friends rangers eti ndio mnajiandaa kucheza klabu bingwa Afrika, kocha wenu akalalamika, mmeenda kutolewa huko ndio mnataka kumfukuza kocha ili kuwadanganya mashabiki mandazi wa utopolo wasiojielewa, nikuulize tu, alivyofukuzwa Kaze kosa lake lilikuwa ni lipi?

GSM wanawapelekesha kama mbuzi mnadani.
 
Ni kweli anakuja kuwa kocha msaidizi wa nabi,pia mwinyi zahera,naye kwa pamoja watasaidiana,hadi pale ambapo nabi akimaliza mkataba ataondoka,kinachomponza nabi ni lugha na pia matamshi yake wachezaji hawamwelewi kabisa

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Hata aje Tuchel utopolo itabaki kuwa utopolo
 
Akirudi kama kocha msaidizi atakuwa ni zezeta!! Kama kocha mkuu sawa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…