Kazi au mume......ushauri

Kazi au mume......ushauri

Mi naona kazi yake ni bora zaidi,kumbuka kabisa kuwa mume anaweza kumuacha lakini kazi haiwezi kumuacha.wengi wamejuta kwakuacha kazi kwa ajili ya mwanaume.
 
nina best yangu ameolewa mwaka sasa, recently amepata kazi nje ya tz (un) kwa mkataba wa miaka 2,yupo kwenye maandalizi kuondoka nchini amepewa miezi 2 ya kujiandaaa. Ameongea na mumewe kuhusiana na suala hili mumewe ameridhia.


Best yangu anatamani sana angeondoka na mumewe, na mpango wake ulikuwa wakati yeye yupo huko kikazi mumewe angekuwa anasoma degree ya pili. Mume amegoma amesema yeye hawezi kuacha kazi, na kama ni kusoma yeye atasoma hapa hapa tz. Hii issue inamsumbua sana best yangu na anasema kama vipi anaweza akaachia hiyo opportunity.

Mimi nimemshauri asiache hiyoo nafasi aliyopata, na aendelee kumshawishi mumewe waende wote kwani sioni sababu ya huyo mume kutokwenda na mkewe. Siamini kama kazi ni kisingizio coz ni mwajiriwa serikalini,na mishahara ya serikali inajulikana kwa hiyo sio kusema akiacha hiyo kazi atakuwa amepoteza big opportunity.

Naombeni tips zaidi juu mtazamo wenu kwenye hili labda naweza kupata idea za kumpa best yangu akaweza kumshawishi mumewe akubali waondoke wote, coz naamini itaimarisha ndoa yao.
kazi ni bora zaidi,simshauri kuacha kazi,wengi imewaghalimu.
 
Miaka miwili mbona michache tu. Mke anabana hadi penati. Duh!
 
Hapo bana Mume ni mpango wa kando Kazi ni mpango mzima. Unamuwaza kumuacha Mama/Baba yako huyo? Ukirudi ukakuta kavuta kifaa unasonga mbele kha?!
 
Huyo dada asiachie nafasi ya kazi, ye aende tu. Akimhofia sana mumewe atashindwa kufanya maamuzi, ye akapige kazi mume watakutana baadae!
 
Hapo bana Mume ni mpango wa kando Kazi ni mpango mzima. Unamuwaza kumuacha Mama/Baba yako huyo? Ukirudi ukakuta kavuta kifaa unasonga mbele kha?!

Dena umenichekesha sana..,kazi ndio mpango mzima copy that!
 
Miaka miwili mbona michache tu. Mke anabana hadi penati. Duh!

KIPIPI ....Huyo dada asiachie nafasi ya kazi, ye aende tu. Akimhofia sana mumewe atashindwa kufanya maamuzi, ye akapige kazi mume watakutana baadae!


nimesoma wapendwa asante
 
nimesoma wapendwa asante

Huyo dada apunguze ubinafsi na pia ajue kuwa anaongea na mwanume...wa Mtanzania na Mwafrika!!

1..Aende majuu kumtegemea mwanamke, 100%. Kula, kulala na msalani bure kama mwanamuziki wa Kongo!
2. Aaache kazi yake inayomfanya aonekane kijogoo wa mujini!! (Kama walau ingewezekana kupewa sabbatical leave ningemshauri alitazame vizuri wazo la mkewe!
3. Aende kupigwa pamba na kupewa shule bure na mkewe...pia na pocket money!

Pamoja na watu kuwe kwenye ndoa, ila ukweli ni kwamba wanabaki kuwa watu 2 ambao ni independent!!!
 
Kweli miaka miwili si lazima waongozane. Na kama unasema hana hofu ya ndoa kuota majani kwa wao kuwa distant sioni kwa nini jamaa a sacrifice kazi yake.

Nadhani huo ni muda wa kujipa break kwani distance ina strenghten love. Na kazi kama inalipa wanaweza kuwa pamoja miezi miwili ya likizo zao za mwaka. Sioni tofauti na mtu ambaye mkewe anasoma Mwanza yeye yuko Dsm. Ulaya ni karibu saaana kuliko mwanza kama una pesa.
 
Nimeipenda hiyo ya mume mpango wa kando, kazi mpango mzima. Teh teh.

Na unadhani Dena kuna mwanaume atathubutu kukuacha wakati una kazi yenye mshiko wa kueleweka?? Very rare. Atamkuta anamsubili.

Hapo bana Mume ni mpango wa kando Kazi ni mpango mzima. Unamuwaza kumuacha Mama/Baba yako huyo? Ukirudi ukakuta kavuta kifaa unasonga mbele kha?!
 
Nimeipenda hiyo ya mume mpango wa kando, kazi mpango mzima. Teh teh.

Na unadhani Dena kuna mwanaume atathubutu kukuacha wakati una kazi yenye mshiko wa kueleweka?? Very rare. Atamkuta anamsubili.

Una uhakika na hilo????


Nadhani shida ya huyo dada siyo kuachwa kwa sababu yoyote ile bali wasi wasi kwamba labda mume wake ataanza kutanua na wanawake wengine!!
 
wakati mwingine ni wivu 2 wa kwamba jamaa ataanza kuchakachua. Mbona wanaume wakienda nje kusoma 4 yrz huwa hawalazimishi kwenda wote? Ni kuvumilia 2,miaka miwili cyo mingi.
 
Ningekuwa mimi ningebaki na mume. Makazi ya UN ushenzi mtupu. Nimekaa field 3 yrs, haizna mpango. Kamani hela bongo zipo tu za kutosha kama ni msakaji. Wengi wakisikia UN wanafikiri kuna cha zaidi ya kujistress kama huna mpango unaishia umaskini tu.

Dada wewe kaa na mume wako!!!!!!!! Endekeza ujinga wa UN tubaki nae sisi tunakuala raha.
 
Ningekuwa mimi ningebaki na mume. Makazi ya UN ushenzi mtupu. Nimekaa field 3 yrs, haizna mpango. Kamani hela bongo zipo tu za kutosha kama ni msakaji. Wengi wakisikia UN wanafikiri kuna cha zaidi ya kujistress kama huna mpango unaishia umaskini tu.

Dada wewe kaa na mume wako!!!!!!!! Endekeza ujinga wa UN tubaki nae sisi tunakuala raha.

Mbona unamrusha roho mwenzio????
 
Tatizo inawezekana ndoa bado ni changa na huwezi jua mdada ali struggle vipi mpaka akaifanikisha hilo la kufunga ndoa. Kingine, pamoja na kuwa jamaa anafanya kazi serikalini sio kigezo cha yeye tu kuamua kuacha kazi bila kuwa na sababu ya msingi, huwezi jua hiyo kazi hata kama ina mshahara mdogo kuna vitu vingine anafanikisha kupitia hiyo position yake ya kuwa katika hiyo kazi.

Kingine inawezekana ni suala la umri, mtu uache kazi halafu baada ya miaka miwili urudi tena uanze kutafuta kazi na umri kila tunasoma kwenye magazeti usizidi miaka fulani, say 37. Kingine huwezi jua huyo jamaa alihangaika vipi mpaka aipate hiyo kazi.

La msingi, kama inawezekana mdada aende kupiga kazi na dollar zi zitakuwepo? awe anamtumia tiketi ya ndege kila baada ya miezi mitatu, si umesema jamaa yupo serikali yeye ni rahisi kuchomoka kuliko kama angekuwa katika private company.

Na pia life ni kama vile kamali, unaweza kusema unaacha kazi kule unafika unakuta mambo siyo, amruhusu mdada aende kwanza akasome mazingira kabla ya jamaa kuamua kumfuata huko.

Kila kheri
 
Ningekuwa mimi ningebaki na mume. Makazi ya UN ushenzi mtupu. Nimekaa field 3 yrs, haizna mpango. Kamani hela bongo zipo tu za kutosha kama ni msakaji. Wengi wakisikia UN wanafikiri kuna cha zaidi ya kujistress kama huna mpango unaishia umaskini tu.

Dada wewe kaa na mume wako!!!!!!!! Endekeza ujinga wa UN tubaki nae sisi tunakuala raha.
Nakubaliana na caro, tatizo la wabongo wengi wakisikia unafanya UN wanadhani ni kila kitu, si kweli, inategemea pia na nchi husika mazingira yakoje, kama ni karzakistani, au Russia hakufai.

Ninachokiona mimi kama sirgeorge alivyosema, ndoa hiyo ni changa, na kwa kweli ni ngumu sana kwa wanandoa kutengana katika kipindi hicho, lakini aende huyo dada kusoma mazingira huko UN, na pakimfaa baada ya miezi kadhaa anaweza kumwita mumewe kuja kumtembelea na dada akamwonyesha hizo opportunity zilizopo huenda akaafiki, maana hata kama ningekuwa mimi huwezi kuacha kazi ati kwa kuwa mkeo anaenda UN wakati hata kuanza bado.
 
kama uchakachuzi kati ya mume na mke unafanyika mnaishi wote sasa hiyo ya kufikiri eti utachakachuliwa haina msingi. Msingi ni ndoa yenu. Ukiruhusu mbio za kukaa mbali kwenye ndoa basi ujue unakaribusha shetani kuwa kiongozi wa maisha yako. Haya ninayosema hakuna wa kuyaelewa mapaka uone.

Muombe mungu akuongoze kwa hilo.
 
kama uchakachuzi kati ya mume na mke unafanyika mnaishi wote sasa hiyo ya kufikiri eti utachakachuliwa haina msingi. Msingi ni ndoa yenu. Ukiruhusu mbio za kukaa mbali kwenye ndoa basi ujue unakaribusha shetani kuwa kiongozi wa maisha yako. Haya ninayosema hakuna wa kuyaelewa mapaka uone.

Muombe mungu akuongoze kwa hilo.
Ubarikiwe sana kwa hii post
 
Nimeipenda hiyo ya mume mpango wa kando, kazi mpango mzima. Teh teh.

Na unadhani Dena kuna mwanaume atathubutu kukuacha wakati una kazi yenye mshiko wa kueleweka?? Very rare. Atamkuta anamsubili.

Noted with thanks
 
Back
Top Bottom