"Kazi Iendelee" ni msemo unaokwepa majukumu huko tuendapo, umekaa kijumlajumla

"Kazi Iendelee" ni msemo unaokwepa majukumu huko tuendapo, umekaa kijumlajumla

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,487
Reaction score
13,611
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wote waliopo huitikia kwa nguvu kazi iendeleee. Nimekaa na kuutafakari huu msemo nimeona kama ni wa kisiasa zaidi.

Unakwepa kuwa na commitment kwenye maisha ya Watanzania milioni 60, ni kama vile ikifika wakati wa Rais kuulizwa kafanya nini aweze kujitetea kirahisi tu kwa kusema niliwaambia kazi iendelee, nilitumia msemo wa jumla!

Ingawa Rais anajaribu kuendana na hiyo kaulimbiu kwa vitendo kwa kutembea Marekani na kuwa na utayari wa kushirikiana na taasisi za kimataifa lipo jambo ambalo naliona kama vile ni deni kwake. Akiweza kulitimiza kwa vitendo ataliweka jina lake miongoni mwa majina yatakayokumbukwa daima.

Ulikuwepo mpango wa Kilimo Kwanza lakini umekufa kifo cha kawaida kabisa, uliondoka na awamu ya nne ya JK. Ulikuwa ni mpango mzuri uliokosa watendaji na ukakosa kule kujitoa kwa wataalam waliopewa kazi ya kuusimamia kikamilifu.

Huwa ninasikitika sana nikiona hii mito tuliyopewa na Mungu inatitirisha maji kuelekea baharini ufikapo mwezi wa April. Inasikitisha mno na kuona hazina hiyo ya maji mengi yakipotea bure. Ushauri wangu ili nguvu ya awamu ya sita isipotee bure ni kutenga pesa nyingi za kujenga visima vya kisasa vya maji, ili wakati wa mvua nyingi tuweke akiba ya kutumia mwaka mzima.

Tutambue kuwa mahitaji ya chakula ya Ulaya ni ya mwaka mzima. Lakini uzalishaji wetu ni wa misimu bado ni ule wa kusuasua. Tukitaka kwenda sambamba na soko kubwa na la uhakika la Ulaya basi tufufue mradi wenye kufanana na kilimo kwanza. Unaweza usiwe unafanana mia kwa mia na ule wa mwanzo, lakini unaweza kuboreshwa na kutusaidia.

Kuliko kuyaona maelfu kwa maelfu ya lita za maji yakitiririka baharini na kupotea bure, Ni wakati wa kuyatumia kwa faida ya kilimo chetu chenye ukame mwingi.

Yangu ni hayo tu kwa jioni hii.
 
2960219_IMG-20211010-WA0032.jpg
 
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wote waliopo huitikia kwa nguvu kazi iendeleee. Nimekaa na kuutafakari huu msemo nimeona kama ni wa kisiasa zaidi.
Unakwepa kuwa na commitment kwenye maisha ya watanzania milioni 60, ni kama vile ikifika wakati wa Rais kuulizwa kafanya nini aweze kujitetea kirahisi tu kwa kusema niliwaambia kazi iendelee, nilitumia msemo wa jumla!.

Ingawa Rais anajaribu kuendana na hiyo kaulimbiu kwa vitendo kwa kutembea Marekani na kuwa na utayari wa kushirikiana na taasisi za kimataifa lipo jambo ambalo naliona kama vile ni deni kwake. Akiweza kulitimiza kwa vitendo ataliweka jina lake miongoni mwa majina yatakayokumbukwa daima.

Ulikuwepo mpango wa Kilimo Kwanza lakini umekufa kifo cha kawaida kabisa, uliondoka na awamu ya nne ya JK. Ulikuwa ni mpango mzuri uliokosa watendaji na ukakosa kule kujitoa kwa wataalam waliopewa kazi ya kuusimamia kikamilifu.

Huwa ninasikitika sana nikiona hii mito tuliyopewa na Mungu inatitirisha maji kuelekea baharini ufikapo mwezi wa April. Inasikitisha mno na kuona hazina hiyo ya maji mengi yakipotea bure. Ushauri wangu ili nguvu ya awamu ya sita isipotee bure ni kutenga pesa nyingi za kujenga visima vya kisasa vya maji, ili wakati wa mvua nyingi tuweke akiba ya kutumia mwaka mzima.

Tutambue kuwa mahitaji ya chakula ya Ulaya ni ya mwaka mzima. Lakini uzalishaji wetu ni wa misimu bado ni ule wa kusuasua. Tukitaka kwenda sambamba na soko kubwa na la uhakika la Ulaya basi tufufue mradi wenye kufanana na kilimo kwanza. Unaweza usiwe unafanana mia kwa mia na ule wa mwanzo, lakini unaweza kuboreshwa na kutusaidia.

Kuliko kuyaona maelfu kwa maelfu ya lita za maji yakitiririka baharini na kupotea bure, Ni wakati wa kuyatumia kwa faida ya kilimo chetu chenye ukame mwingi.

Yangu ni hayo tu kwa jioni hii.
Hata msemo wa Tanzania ya Vwonder nayo ukayeyuka jumla!!
 
Philipo Tanzania ya Viwanda imeishia wapi
Mana hamuoni aibu kusema
Alifeli approach to address
Alifeli strategies
Hakua na right vision whether industrialisation iwe private au government oriented
Hakuna anajua study gani natumia whether China ambao kwa sasa wameshift kwenye privatisation au korea kaskazini
Hatusemi ila tunamengi

Mwacheni Mama Afanye kazi
 
Philipo Tanzania ya Viwanda imeishia wapi
Mana hamuoni aibu kusema
Alifeli approach to address
Alifeli strategies
Hakua na right vision whether industrialisation iwe private au government oriented
Hakuna anajua study gani natumia whether China ambao kwa sasa wameshift kwenye privatisation au korea kaskazini
Hatusemi ila tunamengi

Mwacheni Mama Afanye kazi
Viwanda huchukua muda kusimama. Unaweza kuwa na kiwanda kimesimama ukakosa soko la bidha mfano General Tyre Arusha.
Viwanda huhitaji elimu inayokwenda ikibadilika. Siwezi kusema kama sera nzima imefeli, ilijaribiwa kwenye baadhi ya sekta ikaonyesha mwanga na baadhi ikawa ni failure.

Kwa ujumla tuna safari ndefu.
 
Maza anakwepa kutamka lile jina.... Yesu. Period!

Wakati akiwa Makamu hakuwa hi kulitamka hadharani na kuna uzi humu ulihoji.

Kwa vile serikali haina dini alitakiwa kuwa wazi tu. Hizi salamu za kidini siyo lazima. Wakati wa kina Nyerere na Mwinyi haukuwa nazo. Serikali haina dini. Katikati kuna watu walikuwa wanajaribu kutake advantage ya Waumimini ili kuwafurahisha. Mwendazake aliwakuza sana hawa design ya kina Gwajima mpaka wakadhani hakuna function au kitu kinaweza kuendelea cha kiserikali bila wao. She can reverse this...!!
 
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wote waliopo huitikia kwa nguvu kazi iendeleee. Nimekaa na kuutafakari huu msemo nimeona kama ni wa kisiasa zaidi.
Unakwepa kuwa na commitment kwenye maisha ya watanzania milioni 60, ni kama vile ikifika wakati wa Rais kuulizwa kafanya nini aweze kujitetea kirahisi tu kwa kusema niliwaambia kazi iendelee, nilitumia msemo wa jumla!.

Ingawa Rais anajaribu kuendana na hiyo kaulimbiu kwa vitendo kwa kutembea Marekani na kuwa na utayari wa kushirikiana na taasisi za kimataifa lipo jambo ambalo naliona kama vile ni deni kwake. Akiweza kulitimiza kwa vitendo ataliweka jina lake miongoni mwa majina yatakayokumbukwa daima.

Ulikuwepo mpango wa Kilimo Kwanza lakini umekufa kifo cha kawaida kabisa, uliondoka na awamu ya nne ya JK. Ulikuwa ni mpango mzuri uliokosa watendaji na ukakosa kule kujitoa kwa wataalam waliopewa kazi ya kuusimamia kikamilifu.

Huwa ninasikitika sana nikiona hii mito tuliyopewa na Mungu inatitirisha maji kuelekea baharini ufikapo mwezi wa April. Inasikitisha mno na kuona hazina hiyo ya maji mengi yakipotea bure. Ushauri wangu ili nguvu ya awamu ya sita isipotee bure ni kutenga pesa nyingi za kujenga visima vya kisasa vya maji, ili wakati wa mvua nyingi tuweke akiba ya kutumia mwaka mzima.

Tutambue kuwa mahitaji ya chakula ya Ulaya ni ya mwaka mzima. Lakini uzalishaji wetu ni wa misimu bado ni ule wa kusuasua. Tukitaka kwenda sambamba na soko kubwa na la uhakika la Ulaya basi tufufue mradi wenye kufanana na kilimo kwanza. Unaweza usiwe unafanana mia kwa mia na ule wa mwanzo, lakini unaweza kuboreshwa na kutusaidia.

Kuliko kuyaona maelfu kwa maelfu ya lita za maji yakitiririka baharini na kupotea bure, Ni wakati wa kuyatumia kwa faida ya kilimo chetu chenye ukame mwingi.

Yangu ni hayo tu kwa jioni hii.
Subiri matusi kutoka kwa Chawa wake
 
Uhalisia wa mambo ni kuwa yeye hajachaguliwa kwenye hiko cheo anachotumikia.
Kutochaguliwa sio hoja kakitafuta cheo Tanzania nzima pamoja na hayati JPM, jichanganye tu ufanye ya kipuuzi uone nini kitakukuta.
 
Back
Top Bottom