Etugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 6,514
- 15,247
Bila Shaka baadhi yetu tumeshawahi kusikia msemo huu huko mtaani, naam msemo huu ninaweza kuutumia kama ushauri Kwa vijana wenzangu ambao wanafunga ndoa na hasa hasa katika msimu huu WA mfungo mtukufu ambao tunatarajia hivi karibuni.
Kwanza Kwa wale ambao hawajui Dela ni nini? Ni nguo ambayo imeshonwa mfano WA kanzu hivi na mara nyingi huwa ni ndefu Sana kiasi kwamba mvaaji hulazimika kulishikilia ili apate kutembea vizuri maana Bila hivyo anaweza kulikanyaga na kuanguka au anaweza asiwe huru pale atembeapo. Aina hii ya vazi kuivaa sio tabu Kwani unalivaa kirahisi Tu, kazi au shughuli ipo kwenye kulishikilia na hapo ndo kibarua kizito
Napenda kuongea na waoaji kwamba Kama ilivyo rahisi kuvaa Dela basi hata kuoa ni Jambo rahisi pia,lakini shughuli inakuja kwenye kuyaishi Maisha ya ndoa kama ambavyo shughuli inakuja pale unapolazimika kulishikilia Dela Mda wote.
Wanaume ambao mnatarajia kuoa niwaambie wanawake ni viumbe muhimu Sana lakini vina changomoto nyingi Sana katika sayari hii ya dunia, kwahiyo msitarajie kila siku mtakuwa na good time na wake zenu laa! Itafika kipindi mtakuwa na nyakati ngumu Sana ambazo kama hujajizatiti vizuri basi si ajabu ndani ya miezi mitatu ukajikuta unajilaumu kwanini uliamua kuoa au kumuoa huyo baby mama.
Na wana maneno makali mithili ya Kisu kikali na maumivu yake ni Makubwa mno Kwa mwanaume ambaye hajajitayarisha kisaikolojia kudili nayo, hayo maumivu haya poni Kwa kumpiga au kumtolea lugha chafu Bali yahitaji hekima kubwa na Busara kudili nayo,na kubwa zaidi inahitajika kuwa na Subira kubwa kuweza kusavaivi.
Mwanamke ameumbwa na ubavu uliopinda kwahiyo ukijaribu kuunyosha utakatika na ukiuacha hivyo basi unapinda, umeona eeh Yani hapo kama ule msemo WA ndugu zetu wamakonde " ukisimama nchale na ukikaa nchale" nadhani unajua nazungumzia nini hapa,Kwa wale ambao bado hamjanipata ni kwamba tarajia na tambua kuwa always utapata changamoto nyingi toka Kwa wake zenu lakini kubwa ni kuendelea kulishikilia Dela Kwa nguvu zote.
Ni hayo Tu!
Kwanza Kwa wale ambao hawajui Dela ni nini? Ni nguo ambayo imeshonwa mfano WA kanzu hivi na mara nyingi huwa ni ndefu Sana kiasi kwamba mvaaji hulazimika kulishikilia ili apate kutembea vizuri maana Bila hivyo anaweza kulikanyaga na kuanguka au anaweza asiwe huru pale atembeapo. Aina hii ya vazi kuivaa sio tabu Kwani unalivaa kirahisi Tu, kazi au shughuli ipo kwenye kulishikilia na hapo ndo kibarua kizito
Napenda kuongea na waoaji kwamba Kama ilivyo rahisi kuvaa Dela basi hata kuoa ni Jambo rahisi pia,lakini shughuli inakuja kwenye kuyaishi Maisha ya ndoa kama ambavyo shughuli inakuja pale unapolazimika kulishikilia Dela Mda wote.
Wanaume ambao mnatarajia kuoa niwaambie wanawake ni viumbe muhimu Sana lakini vina changomoto nyingi Sana katika sayari hii ya dunia, kwahiyo msitarajie kila siku mtakuwa na good time na wake zenu laa! Itafika kipindi mtakuwa na nyakati ngumu Sana ambazo kama hujajizatiti vizuri basi si ajabu ndani ya miezi mitatu ukajikuta unajilaumu kwanini uliamua kuoa au kumuoa huyo baby mama.
Na wana maneno makali mithili ya Kisu kikali na maumivu yake ni Makubwa mno Kwa mwanaume ambaye hajajitayarisha kisaikolojia kudili nayo, hayo maumivu haya poni Kwa kumpiga au kumtolea lugha chafu Bali yahitaji hekima kubwa na Busara kudili nayo,na kubwa zaidi inahitajika kuwa na Subira kubwa kuweza kusavaivi.
Mwanamke ameumbwa na ubavu uliopinda kwahiyo ukijaribu kuunyosha utakatika na ukiuacha hivyo basi unapinda, umeona eeh Yani hapo kama ule msemo WA ndugu zetu wamakonde " ukisimama nchale na ukikaa nchale" nadhani unajua nazungumzia nini hapa,Kwa wale ambao bado hamjanipata ni kwamba tarajia na tambua kuwa always utapata changamoto nyingi toka Kwa wake zenu lakini kubwa ni kuendelea kulishikilia Dela Kwa nguvu zote.
Ni hayo Tu!