Kazi ya kudhibiti mapaka bar ni ya mmiliki sio mteja

Kazi ya kudhibiti mapaka bar ni ya mmiliki sio mteja

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Kuna hizi bar hasa za daraja la kati na chini paka huwa wametamalaki wanakodolea macho, wanajipitisha kwenye miguu, wanangurumia wateja na wengine wanawarukia hadi kuwaparua wateja ili wawape nyama au samaki.

Sasa paka wenyewe huwa katika hali mbaya sana ya kiafaya, wengine wakiwa na chawa, wamenyonyoka ngozi au hata ngeu za ajabu ajabu.

Kinachokera na kusumbua ni kwamba wamiliki wa Bar au migahawa wamewaachia wateja jukumu la kupambana na hii mifugo yao jambo ambalo sio sahihi kabisa. Inakera sana mtu ananukala huku anapambana na hii mifugo badala ya wahudumu kuwajibika kuwadhibiti.
 
Ndiyo mkuu wewe unataka paka akale wapi wakati hana ajira wala shamba. Mpatie kipande cha nyama naye aenjoy life
Wenye bar wawe wanawatengea share yao ya nyama ili wasikere na kusumbua wateja.
 
Wenye bar wawe wanawatengea share yao ya nyama ili wasikere na kusumbua wateja.
Mwenye baa kashatengeneza mazingira ya paka kuishi na kulala nipale suala la kula ni wateja!

Kama hutaki kere chukua chakula na vinywaji katumie ukiwa kwako
 
Mwenye baa kashatengeneza mazingira ya paka kuishi na kulala nipale suala la kula ni wateja!

Kama hutaki kere chukua chakula na vinywaji katumie ukiwa kwako
Bar zenu hazina supu takeaway.
 
Mwenye baa kashatengeneza mazingira ya paka kuishi na kulala nipale suala la kula ni wateja!

Kama hutaki kere chukua chakula na vinywaji katumie ukiwa kwako
Umewatetea paka mpaka nimefurahi, kiukweli paka huwa hawana shida kubwaa kiivyo mpaka wawe kero.

Tunaishi nao kwenye hizo bar.
 
Kwa macho ya kawaida unawaona ni Paka lakini ni zaidi ya Paka, na mwenye Bar anajua fika kwanini wapo hqpo.
 
Ndiyo mkuu wewe unataka paka akale wapi wakati hana ajira wala shamba. Mpatie kipande cha nyama naye aenjoy life
Sasa paka akila nyama ya.kupikwa na binaadamu, hao panya wataliwa na nani sasa!?
 
Back
Top Bottom