Kelele masikioni naombeni tiba hata ya kienyeji

Kelele masikioni naombeni tiba hata ya kienyeji

huna tatizo la sikio, una tatizo la mishipa ya neva inayopeleka sauti kwenye akili ili ilete maana, mishipa haifanyi kazi vizuri ndio maana unasikia makelele, unaweza kusikia sauti ya mtu anaongea kwamba ni bezi au sauti laini ila akili inapata shida kutafsiri sauti kuleta maana, hapa muhanga atasema ana nafuu ya kusikia sauti lakini anapata wakati mgumu kuyaelewa maneno.

mafuta ya kuku, mafuta ya kenge, mafuta ya kondoo, maji ya bangi mbichi, kitunguu swaumu, n.k. hizo ni dawa za kutibu sikio linalotoa usaha, kuuma, kuyeyusha wax, n.k. sio dawa ya mishipa ya neva.

hilo tatizo linaitwa tinnitus, kelele zinazosikika kichwani kama mawimbi, filimbi, mivumo, mkwanguo, n.k. hali hii inapelekea na mtu kupungua uwezo wa kusikia.

AINA ZA TINNITUS

1. PRESHA

dalili mojawapo ya presha, mishipa ya sikioni ikifinywa unasikia hizo kelele na kupungua usikivu, nenda hospitalini upime presha, kama unayo watakupa dawa ya kuipunguza, zingatio la muhimu ni kuacha kutumia vilevi kwasababu huwa vinafinya mishipa, kaa mbali na pombe, sigara, bangi, kahawa, n.k. kama huwezi ni kazi bure.

2. KUTUMIA QUININE KUTIBU MALERIA

Wengi ni viziwi tangu wakiwa watoto sababu ya hii dawa, wengine huwa viziwi pamoja na shida ya macho kwa mpigo, quinine huwa inaenda moja kwa moja kufubaza mishipa ya neva ya sikio na hata kwa wengine mishipa ya macho, ndio maana zamani mtu akitumia dawa hii masikio yanaweza kuziba siku 2 mfululizo, tatizo huwa ni pale mtu anavyochomwa sindano ya quinine au kupewa vidonge kuliko kipimo cha kawaida inakuwa ni overdose, huwa wanaanza kupata matatizo ya masikio na wengine macho hata baada ya miaka sita, hawa kutibika inakuwa changamoto kidogo maana muda mrefu umepita, lakini dawa za mishipa ya neva kama neuroton huwa zinasaidia. kaa mbali na vilevi.

3. UPUNGUFU WA VITAMIN B

Wengine ni wale wana upungufu wa vitamin B kana b6 na b12 ambazo ni muhimu kwa afya ya mishipa ya neva, ili kutambua kama upo hili kundi nenda maabatra ya afya kapime viwango vyako vya vitamin b aidha kwa damu au mkojo, ripoti utayopewa itaonesha kama una upungufu wa vitamin b makundi mbali mbali, cheki kama vitamin b6 na b12 zipo chini, kama zipo chini inabidi uiongeze kwa kupigwa sindano, utumie vidonge vya vitamin au kula vyakula vyenye hizo vitamin. kaa mbali na vilevi.

KUFANYA KAZI SEHEMU ZENYE KELELE

Kelele kubwa zikizoeleka kwa muda mrefu, akili inajenga mazoea ya kukaa nazo hata kama haupo eneo la tukio, ndio maana inashauriwa uwe una vaa vifaa vya kupunguza sauti kama upo mazingira ya kelele nzito kwa muda mrefu. kama tatizo limesababishwa hivi inabidi uondoe mazoea yaliyojengwa kwenye akili, unapokuwa sehemu tulivu hasa usiku vaa earphone ama iache redio inacheza muziki laini kwa sauti ya kati tu, hii itasaidia kukandamiza na kuisahaulisha akili yale makelele iliyozoea.
 
Wakubwa nina tatizo la kusikia nakuwa kama kiziwi.

Nimeenda hospital ekanywa nikapewa dawa za miezi miwili lakini sijapata nafuu.

Msaada hata dawa ya kienyeji anayejua ya kutoa kelele masikioni.
 

Attachments

  • Screenshot_2024-05-16-09-54-09-861_com.facebook.katana.jpg
    Screenshot_2024-05-16-09-54-09-861_com.facebook.katana.jpg
    245.1 KB · Views: 10
huna tatizo la sikio, una tatizo la mishipa ya neva inayopeleka sauti kwenye akili ili ilete maana, mishipa haifanyi kazi vizuri ndio maana unasikia makelele, unaweza kusikia sauti ya mtu anaongea kwamba ni bezi au sauti laini ila akili inapata shida kutafsiri sauti kuleta maana, hapa muhanga atasema ana nafuu ya kusikia sauti lakini anapata wakati mgumu kuyaelewa maneno.

mafuta ya kuku, mafuta ya kenge, mafuta ya kondoo, maji ya bangi mbichi, kitunguu swaumu, n.k. hizo ni dawa za kutibu sikio linalotoa usaha, kuuma, kuyeyusha wax, n.k. sio dawa ya mishipa ya neva.

hilo tatizo linaitwa tinnitus, kelele zinazosikika kichwani kama mawimbi, filimbi, mivumo, mkwanguo, n.k. hali hii inapelekea na mtu kupungua uwezo wa kusikia.

AINA ZA TINNITUS

1. PRESHA

dalili mojawapo ya presha, mishipa ya sikioni ikifinywa unasikia hizo kelele na kupungua usikivu, nenda hospitalini upime presha, kama unayo watakupa dawa ya kuipunguza, zingatio la muhimu ni kuacha kutumia vilevi kwasababu huwa vinafinya mishipa, kaa mbali na pombe, sigara, bangi, kahawa, n.k. kama huwezi ni kazi bure.

2. KUTUMIA QUININE KUTIBU MALERIA

Wengi ni viziwi tangu wakiwa watoto sababu ya hii dawa, wengine huwa viziwi pamoja na shida ya macho kwa mpigo, quinine huwa inaenda moja kwa moja kufubaza mishipa ya neva ya sikio na hata kwa wengine mishipa ya macho, ndio maana zamani mtu akitumia dawa hii masikio yanaweza kuziba siku 2 mfululizo, tatizo huwa ni pale mtu anavyochomwa sindano ya quinine au kupewa vidonge kuliko kipimo cha kawaida inakuwa ni overdose, huwa wanaanza kupata matatizo ya masikio na wengine macho hata baada ya miaka sita, hawa kutibika inakuwa changamoto kidogo maana muda mrefu umepita, lakini dawa za mishipa ya neva kama neuroton huwa zinasaidia. kaa mbali na vilevi.

3. UPUNGUFU WA VITAMIN B

Wengine ni wale wana upungufu wa vitamin B kana b6 na b12 ambazo ni muhimu kwa afya ya mishipa ya neva, ili kutambua kama upo hili kundi nenda maabatra ya afya kapime viwango vyako vya vitamin b aidha kwa damu au mkojo, ripoti utayopewa itaonesha kama una upungufu wa vitamin b makundi mbali mbali, cheki kama vitamin b6 na b12 zipo chini, kama zipo chini inabidi uiongeze kwa kupigwa sindano, utumie vidonge vya vitamin au kula vyakula vyenye hizo vitamin. kaa mbali na vilevi.

KUFANYA KAZI SEHEMU ZENYE KELELE

Kelele kubwa zikizoeleka kwa muda mrefu, akili inajenga mazoea ya kukaa nazo hata kama haupo eneo la tukio, ndio maana inashauriwa uwe una vaa vifaa vya kupunguza sauti kama upo mazingira ya kelele nzito kwa muda mrefu. kama tatizo limesababishwa hivi inabidi uondoe mazoea yaliyojengwa kwenye akili, unapokuwa sehemu tulivu hasa usiku vaa earphone ama iache redio inacheza muziki laini kwa sauti ya kati tu, hii itasaidia kukandamiza na kuisahaulisha akili yale makelele iliyozoea.
Naomba tuongee kuhusu hili plzzz, mm ni muhanga na naona umeelezea vizur kabisa. Please
 
Back
Top Bottom