Kelele za wizi wa mali za umma zimezidi sasa, ni wizi wizi wizi kila mahala

Kelele za wizi wa mali za umma zimezidi sasa, ni wizi wizi wizi kila mahala

The Evil Genius

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2014
Posts
6,017
Reaction score
19,506
Ndani ya kipindi kifupi tunasikia taarifa ya wizi wizi wizi wa mali za umma kila kona, kila mahala na mbaya zaidi na watu wakubwa kabisa.

Juzi hapa tulisikia mkurugenzi huko Gairo wa halmashauri ameiba Nondo na Simenti na akazirudisha baada ya kuombwa na waziri Mkuu.

Leo hii kelele za wizi wa Tanzanite zinasikika kila kona, serikali ina mgodi/shimo lake la Tanzanite kule Mirerani watu wanachukua Tanzanite ya Serikali kama ya kwao. Rais aliliongelea hilo mwezi sa 4 akasema wizi huo ukomeshwe lakini sasa ndio unashika kasi.

Leo unasikia ubadhilifu mkubwa wa pesa za umma chuo kikuu Udom, wizi uliopindukia tena kutoka kwa watu wa ngazi za juu kabisa.

Hujakaa sawa unasimia ubadhirifu wa pesa za umma TBC wa kiwango cha kufa mtu, ni wizi uliopindukia kutoka kwa watu wa juu kabisa pale TBC. Ndio maana TBC ukiangalia taarifa ya habari inabidi ukae jirani na tv maana ubovu wa picha unashindwa kuelewa vizuri picha ni ya mtu ama mbuzi, kumbe hela za video camera za hd zimeibiwa.

Leo unasimia mgao wa umeme kila kona, na hili joto watu wanalala bila kuoga, sasa hivi Dar karibu 60% ya watu wananuka vikwapa, hakuna maji na hakuna umeme, ni hatari.

Tanzania tutafika kweli?
 
Ndani ya kipindi kifupi tunasikia taarifa ya wizi wizi wizi wa mali za umma kila kona, kila mahala na mbaya zaidi na watu wakubwa kabisa.

Juzi hapa tulisikia mkurugenzi huko Gairo wa halmashauri ameiba Nondo na Simenti na
Kumbe unaongelea vitu vinavyoripotiwa na serikali na vinafanyiwa kazi! Sasa shida iko wapi?

Ningekuelewa Kama unaongelea mambo yanayoripotiwa alafu hayafanyiwi kazi!

Wizi haujawai kuisha au kupotea suala ni kuwa unadhibitiwa na kufanyiwa kazi au la?
 
Bila shaka na semina sasa zimeanza mahotelini, nimeanza kupata mashaka now, kila mahala na magari yetu bar...
 
Ndani ya kipindi kifupi tunasikia taarifa ya wizi wizi wizi wa mali za umma kila kona, kila mahala na mbaya zaidi na watu wakubwa kabisa.

Juzi hapa tulisikia mkurugenzi huko Gairo wa halmashauri ameiba Nondo na Simenti na akazirudisha baada ya kuombwa na waziri Mkuu.

Leo hii kelele za wizi wa Tanzanite zinasikika kila kona, serikali ina mgodi/shimo lake la Tanzanite
Halafu unamlipa Mbunge 12M kwa mwezi akutetee.
 
Zimejengwa ili wafanyakazi wa serikali wakafanyie semina na kulipana posho...
Kwa iyo wewe hoteli za watanzania zikifanya biashara unaona si sawa?

Zimeajiri watanzania na zinalipa kodi TRA shida iko wapi? Acheni roho zenu za kichawi izo! Zikikosa biashara wanaokosa ajira ni watoto wetu watanzania
 
Ndani ya kipindi kifupi tunasikia taarifa ya wizi wizi wizi wa mali za umma kila kona, kila mahala na mbaya zaidi na watu wakubwa kabisa.

Juzi hapa tulisikia mkurugenzi huko Gairo wa halmashauri ameiba Nondo na Simenti na akazirudisha baada ya kuombwa na waziri Mkuu.

6008AA81-70E1-4041-B094-A1C9602DAC90.jpeg
 
Nahisi kunakikundi komeachiwa kuiba ili kulipa walivyokswa wakati wa Magu.
 
Huwezi tokomeza wizi Tanzania.

Wizi wa mali za umma utabaki palepale staili za kuiba ndiyo zinabadilika kulingana na upepo.

Ukihoji mambo sana utaambiwa siyo kila kitu unapaswa kujua, hushawahi kujiuliza unafichwa nini? na kwanini?.

Kila mmoja ni Hustler.
 
Kwa iyo wewe hoteli za watanzania zikifanya biashara unaona si sawa?

Zimeajiri watanzania na zinalipa kodi TRA shida iko wapi? Acheni roho zenu za kichawi izo! Zikikosa biashara wanaokosa ajira ni watoto wetu watanzania

Kwa hiyo wewe unaona ni sawa matumizi ya hela za serikali yakienda hovyo hovyo kwa watu kufanya semina, mikutano mahotelini na kulipana posho lukuki na matumizi makubwa huku serikali ikiwa na kumbi zake zimejengwa kwa gharama kubwa?
 
Zimejengwa ili wafanyakazi wa serikali wakafanyie semina na kulipana posho...
Hiyo ni sehemu ya shughuli zake. Hakuna tatizo. Serikali inakusanya kodi hapo
Kwa hiyo wewe unaona ni sawa matumizi ya hela za serikali yakienda hovyo hovyo kwa watu kufanya semina, mikutano mahotelini na kulipana posho lukuki na matumizi makubwa huku serikali ikiwa na kumbi zake zimejengwa kwa gharama kubwa?
Hizi fikra zako si sahihi. Serikali ina wajibu wa kuchangamsha private sector pia. Kumbuka sector hii huisaidia serikali kutoa ajira kwa maelfu. Kumbuka pia fedha unazolalamikia hurudi serikalini kupitia kodi.
 
Back
Top Bottom