Kenya Airways kutaifishwa

Wewe huelewi chochote heri ungenyamaza tu, Kwa taarifa yako KQ haiuzwi,pili serikali ya Kenya ndio mmiliki mkuu wa KQ ,kinachofanyika hapa ni kuwaondoa wamiliki binafsi kama KLM na wengine ili KQ iwe [emoji817]% shirika la serikali ndio liweze kumiliki na kuuendesha uwanja wa kimataifa wa jomo Kenyatta.
Sent from my CPH1803 using JamiiForums mobile app
 
Mwaka jana KQ ilitumia $120m ya kipato chake kulipa madeni.... Baada ya hapo ndo wakabaki na loss ya $7m... Hiiinamaanisha madeni yanachangia pakubwa kwa loss, lakini kinacho changia pakubwa zaidi ni KQ kulipa serekali kutumia JKIA manake kila mwaka karibia $400m hutumika na KQ kulipa kodi na utumizi wa JKIA, wakiondolewa hili jukumu KQ itakuana uwezo wa kupata faida kubwa sana.....

Kitakacho fanyika ni kwamba serekali itanunua shares zote kama forcefull takeover, alafu madeni ya KQ yataenda kwa serekali na KQ itabaki bila madeni....


----------------------------------------------------------
Kenya is seeking to emulate countries like Ethiopia which run air transport assets from airports to fueling operations under a single company, using funds from the more profitable parts to support others, such as national airlines.

"The government is keen to take a consolidated view of aviation assets of the country in order to make sure they work in a coherent and efficient way to support the (Nairobi aviation) hub," Koimett said.

The committee's report proposes that Kenya set up an aviation holding company with four subsidiaries, one of which would run Kenya Airways. Another arm of the holding company would operate Nairobi's main international airport.
The committee's report also recommended the holding company be given tax concessions for a period to be determined and that it be exempted from paying excise duty on all goods, including jet fuel.
 
Sasa KQ itajazwa election losers kwa bodi na wafanyakazi zazwa wa kabila mbili😂😂😂
 
Alaumiwe rubani aliyetua chato airport akimpakia Uhuru Kenyata
 
Uwanja wa Jomo unamilikiwa na kusimamiwa/kuendeshwa na nani?
 
Mm nilikuwa na hisa 4000 KQ nilinunua hapa tz nitalipwa chuma ngapi hapa naombea mambo yaende kinyang'au nyang'au tulipwe mifedha mingiminvi Kwa sababu familia ya Kenyatta nayo inamiliki pakubwa KQ nisipokuwa tajiri mwaka huu basi tena maana hii ni bahati ya kutembelea nyota ya mafisadi ya kenya
 
Sasa KQ itajazwa election losers kwa bodi na wafanyakazi zazwa wa kabila mbili😂😂😂
Hio campuni itakua semi-autonomous kutokana na bunge kama vile zile independent commissions kama vile SRC,KHRC.. etc same public process iliotumika ku appoint watu wa nguvu kama DPP Haji au Chief Justice Maraga ndo itatumika.
 
Haa uliziuza !!! Kumbe ulikuwa unatukubali watz tulivyokuwa tunachambua kufilisika Kwa KQ ungeniuliza ning'ekushauri vizuri maana wenzako tutatembelea nyota ya fisadi Kenyatta na familia yake lazima atajilipa mabilioni ya fedha za walipa kodi wa Kenya Kwa hisa moja isiyo endana na uhalisi wa bei hivyo wanahisa wote tutanufaika
 
Hio campuni itakua semi-autonomous kutokana na bunge kama vile zile independent commissions kama vile SRC,KHRC.. etc same public process iliotumika ku appoint watu wa nguvu kama DPP Haji au Chief Justice Maraga ndo itatumika.
Hehe unajifariji tuu..Angalia hali ilivyo KPLC,KPA na KPC
unaongea watu wa nguvu eti DPP na juzi walipendekeza Justice Chunga awe prosecutor, yaani jitu ambalo lilishuhudia mauwaji ezi za Moi. Ilibidi tu tupige kelele mitandaoni hadi jitu lenyewe lika kataa hiyo kazi.
You are placing your hopes on thieves
 
Majigambo mengi kwamba tuna route ya Marekani sasa hayana faida maana shirika liko taaban! Tuna ndege nyingi kuliko nyie kumbe mwendo ni wa hasara tu.... Jifunzeni kumeza viburi vyenu
 
We msukuma...unajua nn zaidi ya kujifanya mkenya[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Ni vema serikali ya Kenya imeshtuka mapema. Ni ngumu sana kuendesha public airline isiyomilikiwa na serikali kwa asilimia 100 hapa Africa.

Hakuna aviation business kubwa kihivyo kuendana na gharama za biashara hiyo hususani bei za ndege zenyewe.

Hivyo basi, malengo makubwa ya mashirika haya yapaswa kuwa kukuza sekta zingine kama utalii, biashara, kilimo, viwanda, nk.

Si sahihi kulenga kupata faida kwenye financial statements za haya mashirika.

Hapa sasa ndipo private sector anatupwa nje kwani yeye lengo lake kubwa ni kupata faida. Nakumbuka baada ya anguko la kiuchumi la 2009 Japan ililazimika kulisaidia shirika lake usd 27bln ili kulilinda lisianguke.

Ila ikumbukwe kuwa serikali inapomiliki airline kwa 100% kuna mgogoro wa kibajeti utatokea. Baadhi ya pesa ambazo kawaida zilienda maeneo mengine zitaelekezwa "nje ya nchi" kununua ndege.

Hapo taratibu vyuma vitaanza kukaza katika kipindi kifupi. Hapa ndipo serikali hugeuka adui wa wananchi hata kama inafanya hivyo kwa faida yao wenyewe.

Ikiwa uwepo wa shirika hilo una tija kiuchumi, taratibu hali inapaswa kuanza kuimarika kwenye kipindi cha kati (medium term) kuelekea kirefu (long run).





H
 
Uwanja wa Jomo unamilikiwa na kusimamiwa/kuendeshwa na nani?
Unaendeshwa na shirika la viwanja vya ndege la KAA ambalo ni la serikali , lakini serikali inampango wa kuutoa uwanja wa JKIA chini ya hilo shirika na kuuweka chini ya KQ ila hilo haliwezekani kama KQ itakua na wamiliki binafsi na ndio maana serikali inanunua hisa zote zinazo milikiwa na KLM royal na mashirika mengine kama KCB ,CBA, Co-op bank etc,itaundwa kampuni maalumu itakayo endesha KQ na JKIA kama kampuni moja.
 
Tumeaminishwa kwa muda mrefu kuwa GoK aslani haifanyi biashara. Huu uzi sijauelewa au?
 
Tumeaminishwa kwa muda mrefu kuwa GoK aslani haifanyi biashara. Huu uzi sijauelewa au?
Serikali ya Kenya ndio inamiliki hisa nyingi za KQ, aliyewaaminisha vingine aliwahadaa. Ila naelewa kwamba nyinyi watz mna ushabiki mwingi sana kuhusu siasa na masuala ya Kenya. Ndio maana mlimtwika rais Uhuru Kenyatta taji la baba wa demokrasia, wakati sisi wakenya tunamuona wa kawaida sana.
 
Hapa target ni kupata uwanja ndo mtumie kupata faida
Na acha kupotosha watu kwamba kq inalipa 400mil kwa government
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…