Kenya Election 2007: Outcomes

Kenya Election 2007: Outcomes

Mkuu please clarify, agakhan anaingiaje? nifungue macho hapa

Agakhan Owns the Nation media group ambayo pia ni inamiliki Mwananchi na the Citizen. lakini aliifanya hii nation iwe independent for his other investment portfolios.
 
Halafu unadiriki kweli kukubaliana na Kibaki kwamba hili ni tatizo la ndani ya Kenya, na wewe unakubali kweli?

..bado hajaona jinsi wakenya wanavyohamia tanzania kwa makumi. na bado wengi wako njiani!

..hajui kama hali yao ikiendelea hivyo,dar port will be a mess,infact even our roads,as miundombinu yetu haiwezi support vya kutosha influx ya cargo to uganda,rwanda,burundi na drc.

Nimejaribu kukutafutia article iliyopo kwenye The Economics ya leo naona nimeshindwa kui-access online; nakushauri sana popote ulipo utafuta nakala ya The Economics ya leo: soma uk 9 na 45 utaelimika sana kuhusu kilichotokea Kenya.

..seconded!
 
..bado hajaona jinsi wakenya wanavyohamia tanzania kwa makumi. na bado wengi wako njiani!

Mbaya zaidi ni kwamba hao wakenya wanazuiwa mpakani, sasa sijui wanataka wafie ndani ya Kenya? Kibaki anazuia wakenya wasitoke nje ili tatizo liendelee kuonekana ni la ndani ya Kenya na hivyo halihitaji attention ya mataifa mengine.
 
Mbaya zaidi ni kwamba hao wakenya wanazuiwa mpakani, sasa sijui wanataka wafie ndani ya Kenya? Kibaki anazuia wakenya wasitoke nje ili tatizo liendelee kuonekana ni la ndani ya Kenya na hivyo halihitaji attention ya mataifa mengine.

..kweli mbuzi wa masikini hazai!

..kwahiyo wenye pass za kusafiria pekee ndio wanahama?!
 
Africa World News | Home
Kampala, Uganda - Uganda's military was on high alert Thursday as the violent conflict that has rocked neighbouring Kenya has sparked fears of a cross-border spillover. Uganda has already felt the effect from unrest in Kenya, with oil prices hiked up and shortages across the country. Uganda depends on Kenya's Indian Ocean port for petrol and the violence has halted transport.
 
Mkuu Kiltime:

Yaani wewe bado unataka watu wameze maneno kuhusu huu wizi wa urais huko Kenya? Kama diplomatic missions wenyewe wanasema Kibaki kaiba urais unataka CHADEMA watumie maneno gani? Kumbe wewe bado unakubaliana na falsafa ya kuwa neutral? Hujui kuwa neutrality ni adui mkubwa wa conscience na ni silaha ya binadamu wote waoga na wazembe wa kutafakari? Halafu unadiriki kweli kukubaliana na Kibaki kwamba hili ni tatizo la ndani ya Kenya, na wewe unakubali kweli? Ina maana wewe huna kabisa kamshipa ka-pan africanism? Na kwa nini unakubaliana na Kibaki (serikali) na hutaki kuwasikiliza wengine wanaongea au nawe unaamini kwamba ni serikali pekee inayohodhi ukweli?

Nimejaribu kukutafutia article iliyopo kwenye The Economics ya leo naona nimeshindwa kui-access online; nakushauri sana popote ulipo utafuta nakala ya The Economics ya leo: soma uk 9 na 45 utaelimika sana kuhusu kilichotokea Kenya na naamini baada ya kusoma hizo article unaweza kubadilisha kidogo mtazamo wako.

Kitila Mkumbo,

Heshima mbele!

Mimi (Kilitime) nimechukizwa sana na Kibaki alichofanya na wewe Kitila the same na wengine wengi! na Huenda na Kikwete, huenda na Mbowe, huenda na Lipumba!!! okay no problem.

Tanzania kama taifa huenda haikufurahishwa pia, lakini Tanzania kama taifa haiwezi kusema Kibaki toka! ila yaweza kusema kaeni muyamalize Kibaki na Raila muyamalize!!! na hili ndilo UK/USA wameendelea kulisema, hawajasema Kibaki toka!!! NO!!!... kwa maana nyingine kama taasisi mbali mbali hii ndio inakua misimamo!!! lakini individual hakuna shaka mkuu!!!

Nawatakia maandamano mema!!! lakini kumbukeni hawa ni majirani na kumbukeni narudia tena tofauti ni kati ya Wananchi wa Kenya, Kibaki ni Mwananchi wa Kenya na Raila ni Mwananchi wa Kenya, ODM ni chama cha Kenya, na PNU ni chama cha Kenya. Hata kama source ni Uchaguzi au Ukabila au namna yoyote ile. Let them deal with it first!!! Kabla pili pili ya shamba haijawawasha!!!

Kama ingekuwa Kenya na Ethiopia,,, well tungekuwa na nguvu zaidi ya sisi kusimama kama chama na kama Taifa kusema lolote kwa urahisi zaidi!

Zimbabwe tuko nao, sio kwa kusema Shangarai ni Mbaya au Mugabe ni Mzuri,,, ni kwa kusema Uingereza acheni/mpeni basi nafasi Mugabe afanyie kazi mambo ya Ndani ya nchi yake!!! Nadhani huo ndio msimamo wa Tanzania.

Hiyo article nitafutie niendelee kujielimisha lakini itakuwa imeandikwa na binadamu kama wewe na mimi sio malaika!!! anaweza lalia upande wowote!!!

Ndio maana nawapongeza sana viongozi wa dini kuombea amani, sio kuombe Raila au Kibaki adumu Madarakani?

Swali:
Ukishajibu Maraisi wa Maswali haya matatu utajua kwanini nimesema hivyo!!! regardless walichukua je madaraka!!! hata M7 awamu yake ya Kwanza haikuwa kachaguliwa but he was the president of republic of Uganda.

Raisi wa Jamhuri ya Kenya ni nani?______________________

Raisi wa Visiwa vya Zanzibar ni nani?___________________

Raisi wa Jamhuri ya Zimbabwe ni nani?__________________

Hawa wote walikuwa na issues lakini kuna marais wao ambao wako madarakani mpaka sasa pamoja na issues zinazoendelea sasa za miafaka na kadhalika!!!
 
1. Kibaki na Raila wakutane waongee kama Viongozi na Wanakenya


2. Mahakama- Kama ODM wana wasiwasi over Mahakama ya Kenya- ile ya EA ya Arusha itumike- kwani tuliona walivyokabili upendeleo wa Wale Wbunge wa Kenya- ktk AELA- as hao wabunge wanatoka Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Tz- basi kuna haki zaidi!
Jurdicial Process should be fast tracked in 3 months- rulling iwe tayari!
 
Kilitime, nakubaliana na wewe na reaction yangu ya kwanza kuhusu maandamano hayo ni kuwa "unnecessary". Hasa kutokana na subject yenyewe na jinsi ilivyodokezwa kwangu.

Endapo maandamano haya yatachukua sura ya kumuunga mkono Raila na kumlaani Kibaki siyo tu yatakuwa ni ya uchochezi bali hayatasaidia kutafuta usuluhishi kule Kenya. Endapo mzigo wa uvunjaji wa haki za binadamu na mauaji yaliyofanyika utabebeshwa kwenye mabega ya Kibaki tu sidhani kama hilo litasaidia katika kuleta uponyaji wa Kenya.

Binafsi naamini kabisa kuwa Raila ana sehemu kubwa ya kulaumiwa kutoka na machafuko ya kisiasa nchini Kenya kama vile Kibaki anavyolaumiwa. Yawezekana wengi wetu kutokana na kutaka "Raila ashinde" na baada ya kuona upuuzi na uhalifu uliofanyika katika kutangaza kura tumekuwa vipofu wa kufuata haki na hivyo kuchukua upande wa "anti-kibaki" ilimradi na sisi tuoneshe kuwa haki haikutendeka.

Hilo laweza kuwa sawa. Hata hivyo kwenye moto na cheche za Ukabila na mauaji yanayoshabihiana na yale ya kimbari rafiki kuchagua upande au kuonekana wamechagua upande haisaidii kitu zaidi ya kupulizia moto!

Kenya wako katika moto, na sisi Watanzania na hasa wapinzani wasitumike kama wapuliziaji moto kwa kisingizio "cha mshikamano" na "wale wote wenye kutetea utawala wa demokrasia".

Tufanye vitu vya kwanza kwanza; Raila na timu yake na Kibaki na timu yake wasiweke preconditions zozote na wakae meza ya mazungumzo and nothing should be taken off the table and everything should be open for discussion!
 
Raila na timu yake na Kibaki na timu yake wasiweke preconditions zozote na wakae meza ya mazungumzo and nothing should be taken off the table and everything should be open for discussion!

Unaleta utani. Bahati nzuri najua utakuwa na namba ya Raila. Talk to him and you'll know what's his stand regarding such talks to Kibaki. The guy's firm; he's not ready to do so. Maybe you can convince him and then remember to tell Kibaki to accept what Tutu is [SIZE=-1]trying to mediate to end turmoil that has killed more than 500 people.

[/SIZE]
[SIZE=-1]
ALeqM5gAl-zU3B_I84cqcAwUrftX6vaNmQ

[/SIZE]Mwai Kibaki walks alongside South African Archbishop Desmond Tutu
 
Kilitime, nakubaliana na wewe na reaction yangu ya kwanza kuhusu maandamano hayo ni kuwa "unnecessary". Hasa kutokana na subject yenyewe na jinsi ilivyodokezwa kwangu.

Endapo maandamano haya yatachukua sura ya kumuunga mkono Raila na kumlaani Kibaki siyo tu yatakuwa ni ya uchochezi bali hayatasaidia kutafuta usuluhishi kule Kenya. Endapo mzigo wa uvunjaji wa haki za binadamu na mauaji yaliyofanyika utabebeshwa kwenye mabega ya Kibaki tu sidhani kama hilo litasaidia katika kuleta uponyaji wa Kenya.

Binafsi naamini kabisa kuwa Raila ana sehemu kubwa ya kulaumiwa kutoka na machafuko ya kisiasa nchini Kenya kama vile Kibaki anavyolaumiwa. Yawezekana wengi wetu kutokana na kutaka "Raila ashinde" na baada ya kuona upuuzi na uhalifu uliofanyika katika kutangaza kura tumekuwa vipofu wa kufuata haki na hivyo kuchukua upande wa "anti-kibaki" ilimradi na sisi tuoneshe kuwa haki haikutendeka.

Hilo laweza kuwa sawa. Hata hivyo kwenye moto na cheche za Ukabila na mauaji yanayoshabihiana na yale ya kimbari rafiki kuchagua upande au kuonekana wamechagua upande haisaidii kitu zaidi ya kupulizia moto!

Kenya wako katika moto, na sisi Watanzania na hasa wapinzani wasitumike kama wapuliziaji moto kwa kisingizio "cha mshikamano" na "wale wote wenye kutetea utawala wa demokrasia".

Tufanye vitu vya kwanza kwanza; Raila na timu yake na Kibaki na timu yake wasiweke preconditions zozote na wakae meza ya mazungumzo and nothing should be taken off the table and everything should be open for discussion!
Mwanakijiji, nimekuwa nasoma sana thread zako na nyingi huwa zimesimama imara ila hii ya kusema kuwa Raila pia anapaswa kulaumiwa sijaelewa, alaumiwe kwa lipi? Tunachokiona kenya kwa sasa ni matokeo ya wananchi waliompigia kura Raila wa react baada ya haki yao kupotea, hatujasikia hata mara moja Raila akiwahamasisha wafuasi wake wafanye fujo, sasa utamlaumu Raila kwa lipi?
 
Way foward,

1. Kabaki na Raila wakutane kama viongozi na kuongea- hata kama iatabidi kuwe na uchaguzi tena- ila waache ubabe na ubinafsi waongee kama Wanakenya!

2. ODM waende mahakama ya EA. Kwa kuwa Kenya ni signatory wa EA na hii mahakama ina mahakimu wa nchi za Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda na Tz- maamuzi yao yatakuwa fair! Je do you recall ile case ya members wa Kenya EALA na ruling ya EA mahakama? Kulikuwa na fairness!

3. EA as a region we need institution zaidi ya mahakama za member states so as to resolve crisis of this nature- in the future!
 
Kilitime, nakubaliana na wewe na reaction yangu ya kwanza kuhusu maandamano hayo ni kuwa "unnecessary". Hasa kutokana na subject yenyewe na jinsi ilivyodokezwa kwangu.

Endapo maandamano haya yatachukua sura ya kumuunga mkono Raila na kumlaani Kibaki siyo tu yatakuwa ni ya uchochezi bali hayatasaidia kutafuta usuluhishi kule Kenya. Endapo mzigo wa uvunjaji wa haki za binadamu na mauaji yaliyofanyika utabebeshwa kwenye mabega ya Kibaki tu sidhani kama hilo litasaidia katika kuleta uponyaji wa Kenya.

Binafsi naamini kabisa kuwa Raila ana sehemu kubwa ya kulaumiwa kutoka na machafuko ya kisiasa nchini Kenya kama vile Kibaki anavyolaumiwa. Yawezekana wengi wetu kutokana na kutaka "Raila ashinde" na baada ya kuona upuuzi na uhalifu uliofanyika katika kutangaza kura tumekuwa vipofu wa kufuata haki na hivyo kuchukua upande wa "anti-kibaki" ilimradi na sisi tuoneshe kuwa haki haikutendeka.

Hilo laweza kuwa sawa. Hata hivyo kwenye moto na cheche za Ukabila na mauaji yanayoshabihiana na yale ya kimbari rafiki kuchagua upande au kuonekana wamechagua upande haisaidii kitu zaidi ya kupulizia moto!

Kenya wako katika moto, na sisi Watanzania na hasa wapinzani wasitumike kama wapuliziaji moto kwa kisingizio "cha mshikamano" na "wale wote wenye kutetea utawala wa demokrasia".

Tufanye vitu vya kwanza kwanza; Raila na timu yake na Kibaki na timu yake wasiweke preconditions zozote na wakae meza ya mazungumzo and nothing should be taken off the table and everything should be open for discussion!

Mwanakijiji,

Je wewe ungelikuwa Raila, ungefanyeje?

Hata ungewaambia wafuasi wako, nani angekusikiliza?

Kuna haja ya kurudi nyuma na kuchunguza migogoro ya dunia. Raila alikuwa hana uwezo wa kuwaamuru wale vijana waache kufanya walichokuwa wanafanya. Ila tu alikuwa na uwezo wa kukaa na wenzake na kupata suluhu ambayo baadaye angeweza kwenda kuiuza kwa wafuasi wake. Vinginevyo asingefanikiwa na angeishia kudharauliwa na hata wafuasi wake.
 
Ssebo na Mtanzania, niwajibu kwa pamoja.

Katika hali ambayo kuna moto wa hasira, kero, hisia za kisasi na uchungu, matumizi ya maneno ni muhimu sana. Hakuna kitu kinachochoea zaidi hasira na maumivu ya kihisia kama matumizi mabaya ya maneno.

Wakati Kibaki anapaswa kulaumiwa na kuwajibishwa kwa vitendo na ukimya wake baada ya kuanza kwa vurugu, Raila anapaswa kulaumiwa na kuwajibishwa kutokana na maneno na vitendo vyake.

Pindi vurugu zilipoanza tu Raila alipaswa kusimama na kujiengua moja kwa moja na mambo hayo badala ya kudai "wananchi wanadai haki yao ya Kikatiba" n.k Raila kama kiongozi alishindwa kabisa kutumia ushawishi wake wa kupanga mkakati uliotulia badala ya kuonekana hajali kinachotokea huku akiendelea kumbebesha lawala Kibaki na kufikia kumuita Mwizi (kitu ambacho chaweza kuwa kweli).

Nitarudisha mfano wa mauaji mengine ili nisikike vizuri; Wakati wa mauaji ya Rwanda kilichoumiza zaidi ni ukimya wa baadhi ya watu na upande wa pili maneno ya upande mwingine kwa kisingizio cha kudai haki! Kama kweli Raila alitaka kuongoza mapambano haya na kuwa tayari kumwaga damu yeye ndiye angekuwa wa kwanza kutembea kwenda kule na apigwe Mabomu kama Mrema, na achapwe viboko kama kina Lewis wa Georgia..

Kama lengo lilikuwa ni kujaribu kutatua mambo haya kwa amani na kuonesha brutality ya serikali alikuwa na uamuzi wa kufanya mikakati ya maandamano ya amani (siyo kusema maandamano ya amani) kama walivyofanya Martin Luther na Gandhi! Raila ameshindwa hivyo.

Watu waliompigia kura Raila haiwezekani wote walikuwa watu wa makabila mengine na hakuna Mkikuyu aliyempigia kura. Kuna Wakikuyu wengi (hasa vijana) ambao waliona ndani ya Raila mabadiliko na matumaini ya mwelekeo mpya wa Taifa. Kitendo cha Raila kutojitokeza mara moja, kupinga, na kutojihusisha kwa namna yoyote na mashambulizi dhidi ya Wakikuyu au mali za Wakikuyu ni kitendo cha kushindwa uongozi, yes I said it!

Raila alikuwa na nafasi ya kuonesha umakini, uthubutu, ujasiri na ukomavu wa kisiasa. Badala ya kudai "ni vyombo vya serikali ndiyo vinafanya vurugu" Raila angetumia uwezo wake wote kutuliza moto huo huko akijipanga hatua inayofuata. Wote wawili Raila na Kibaki wanahusika moja kwa moja na mauaji na machafuko ya kisiasa nchini Kenya ni wao na timu zao lazima wakae chini na kutafuta suluhu bila kuweka masharti mapema.

Raila ana ushawishi mkubwa na ameshindwa kutumia ushawishi huo kutuliza Kenya na kwa maneno yake amechochea vurugu zilizotekea nchini Kenya baada ya uchaguzi. Endapo uchaguzi mwingine utaitishwa Kenya, msishangae Wakikuyu wengi waliomuunga mkono Raila wataaamua kubadili msimamo.
 
FIVE HINTS
1.In any revolution loss of life is inevitable because the aggressor is ready to kill to mantain the status quo and the oppressed want liberation

2.The person dying today for libaration,the next generation will honour his/her blood

3.If you flip your tail before the oppresor,you are failing your own generation and future generation

4.You have got to choose,betray yoursef,your generation and be a loser or confront the reality,be honoured as a matyr and be a winner

5.Lets be realistic,peace and justice can never be separated.If you keep one you keep both,if you lose one you lose both.The example is there,dont ask me anything.If you still dont understand,Join us in Kenya.
ALL THOSE WHO HAVE LOST THEIR LIFE TO DEFEND THEIR DEMOCRACY WILL NEVER BE ASHAMED
 
Mkjj na Kilitime kweli mna hoja. your tone sounds so diplomatic and thats what the would be power wilders prefer. Hapa kinachotokea Kenya ni pale wananchi wanapofika peak na kusema NO ENOUGH IS ENOUGH! Wananchi wa Kenya wameamka unlike majority yetu katika bara zima, Africa tumezoea kuwatake wananchi wetu for granted kabisa and this is what Kibaki naively tried to do, thinking kwamba kuweka polisi wakarusha mabomu the game will be over na ataendelea kula nchi for the next five years!

If you think and know that you wouldnt honour the wananchi verdict why then call election? isnt it the waste of money and time?

Hawa wananchi waliambiwa wakapige kura kumchagua wanayemtaka, they faithfully qued kuanzia alfajiri mpaka usiku bila hata kumkwaruza jirani, mpaka polisi Commissioner Ali akawapongeza! sasa leo hiyo serikali kwa nini yenyewe ishindwe kuplay its part of the bargain na wananchi ndo warushiwe mpira? I say No , this dirty game must end in Africa. And the only way to end is through protest, maana diplomatically imeshindikana! Si wamepiga kura, jamaa akakataa kuheshimu maamuzi ya "waajiri" wake? Sasa mwananchi wa Kenya amebaki na silaha gani ya kupambana na Kibaki kama kura yake ndo haina thamani tena??

Diplomacy ni kweli should be given a chance, But I have never seen where it works bila kuwawajibisha hawa vibaka waliokubuhu wanaojiita life presidents especially in third or fourth world countries...... from Ukraine, Georgia, Chile nk! Diplomacy can only work where the defendants and plaintiful are diplomatic! Hizi ziara za Jayndair Frazier, Kufour nk, ni geresha tuu kutudanganya wananchi...hatudanganyiki tena..., wananchi lazima waamke wadae haki yao, hata kama ni kwa ncha ya upanga! After all, kwa Africa the only music our rulers can withstand ni confrontation.

Everybody knows the election was stolen..ok lets use diplomatic language..the elction had irregularities..kwa nini hao diplomats wasimwambie Kibaki ukweli?? We are tired of this diplomatic charade my comrades!!

Kuhusu Raila, mi nadhani we are missing a point and unfair to him! Jamaa aliuza manifesto yake, watu wakamchagua enmasse sasa leo iweje yeye ndo alaumiwe. Mi it doesnt matter kama yeye ndo angekuwa ameina kama incumbent ningemcondemn kama Kibaki.. na kumbuka mwenye hasira siyo yeye tuu, lakini kwa kila mkenya anayeona kwamba ana haki ya kutetea taifa lake hata kama ni kwa kumwaga DAMU!! Ooooh nooo I dont agree, when the worst comes to the worst these dictators must be confronted even if it means shedding blood!

And I tell you, after this unfortunate event, Kenya will raise as stable democracy! Maana watawala watajua kwamba Kenya belongs to ALL KENYANS AND NOT FEW HUNGRY AND WEALTH CLIQUE.

Tumeziona hizi diplomacy za Mbeki Zimbabwe, zimafanya nini? zaidi ya kuwaumiza wananchi mpaka leo wanakufa na kuumia bila sababu..Kisa?? mazungumzo yanaendelea.. kisa diplomacy. I WOULD SUPPORT DIPLOMACY EVEN IN KENYA IF IT WAS GENUINE!! But its not, ni ule ule unafiki wa viongozi wa kiafrika. rub my back I will rub yours tommorrow..

Certainly we cant condon violence, and whats happening is unfortunate, but where Africa is now I can surely say thats the best language our dictators can understand! we cant afford any more ujinga wa Kibaki type..we have enough problems on our continent!!!

Africa tumenyonywa na Mkoloni, tumeteseka kwa majanga ya kila aina, sasa hata waafrica wenzetu wanataka kuwa wakoloni? surely we can now understand why people/suicide bombers blow up their lives!!

Iam sorry guys, to sound harsh, but what Kibaki did is so disguisting for any African to be proud of being an African. And it should be a lesson to all these dictators Mugabe,Zenawi and Mbeki who has joined the group of recently!
 
Ssebo na Mtanzania, niwajibu kwa pamoja.



Kama lengo lilikuwa ni kujaribu kutatua mambo haya kwa amani na kuonesha brutality ya serikali alikuwa na uamuzi wa kufanya mikakati ya maandamano ya amani (siyo kusema maandamano ya amani) kama walivyofanya Martin Luther na Gandhi! Raila ameshindwa hivyo.

.

Jamani afanye maandamano yepi wakati ameitisha rally serikali ikawakataza? kifupi how do you want Raila to adress his supporters? wakati wamekatazwa kukutana? Hata vyombo vya habari vilikuwa blacked out! Lets be fair..kama maandamano yangeruhusiwa na yakazua balaa baada ya Raila kuhutubia, Iam sure tungekuwa tunaongea mengine kuhusu culpability ya Raila.

Polisi kazi yao ni kulinda usalama wa raia, sasa ni usalama gani wamelinda zaidi ya kuwa tear gas wananchi? Polisi ingebidi wajae uhuru park kuchunga amani, lakini walienda barabarani kugombana na wananchi wasifike uhuru park!!! Jamani.. we have solid experience....hizi siasa za CCM eti hamruhusiwi kuandamana kwa sababu "tunahisi" kutatokea fujo! tumezizoea sana Tanzania na kwingineko. Ndo nasema watawala wetu wa Kiafrika they should better wake up! Time is running out kwa wao kuzidi kutudanganya.

Iam sure Kibaki hakutaka maandamano ya ODM kwa sababu aliogopa wananchi watajua from their leaders what happened...and as a result we are seeing what we see..
 
kumlaumu Raila ni kupoteza muda kwa sasa kwa sababu wapiga kura walikuwa na matarajio yao,ambayo walidhani yanaweza kutimizwa kupitia kwa Raila,hii point of no return ikifikiwa kumzuia mhusika ni ngumu,watu wamedhurumiwa kiasi cha kutosha kwao maisha hayana maana kwa kuwa tumaini limeondoka
 
Back
Top Bottom