Kenya: IEBC yatiliwa shaka baada ya sanduku la kura kupatikana kichakani

Kenya: IEBC yatiliwa shaka baada ya sanduku la kura kupatikana kichakani

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
23e7c5045565c57581bfda524ea806f7.jpg
Kasoro zaidi za Uchaguzi Mkuu wa Agosti 8 zilijitokeza Jumatano baada ya sanduku la kura za ugavana katika Kaunti ya Turkana lilipopatikana na wafugaji kichakani.

Sanduku hilo lilipatikana karibu na makutano ya Napeililim katika barabara ya Lodwar kuelekea Kakuma, lilikuwa limefungwa lakini lilikuwa na shimo chini.

Maafisa wa Chama cha Jubilee walikuwa wa kwanza kuwasili eneo hilo baada ya kuarifiwa na wafugaji walithibitisha kuwa sanduku hilo halikuwa na karatasi za kura ndani.

Mwenyekiti wa Chama hicho katika kaunti hiyo, Bw James Kuya alisema shimo katika sanduku hilo ni kubwa, ishara kwamba karatasi za kura zilizokuwepo zilitolewa.

"Masanduku yote ya uchaguzi na vifaa vingine vinavyotumiwa ni lazima viwe mikononi mwa Serikali. Kwa nini sanduku hili liko hapa siku saba baada ya uchaguzi?", aliuliza

Alisema viongozi wa Jubilee katika kaunti hiyo walikuwa wamelalamika kuhusu jinsi Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka IEBC ilivyosimamia uchaguzi eneo hilo.
 
Swali nyeti niiii, na najua wenzangu mnajiuliza swali hili piaaa! Aliyepata sanduku hilooo alikuwa anafanya nini kichakaniiii? Nikiripotia JFtv mi ni wenuu...........! 😀
 
Swali nyeti ni, na najua wenzangu mnajiuliza swali hili piaaa! Aliyepata sanduku hilooo alikuwa anafanya nini kichakaniiii? Nikiripotia JFtv mi ni wenuu.......! 😀
Kama waliolipata ni wafugaji haina haja kujiuliza maswali mengi, kwa vile kazi ya mfugaji iko wazi

Akina nani waliliweka huko kichakani ilhali vifaa hivyo vya uchaguzi Tume ndo mdhibiti? Gumzo hapo ndipo
 
Leteni plastic huku, tunahitaji kutengeneza mifuko na chupa za maji.
 
Swali nyeti niiii, na najua wenzangu mnajiuliza swali hili piaaa! Aliyepata sanduku hilooo alikuwa anafanya nini kichakaniiii? Nikiripotia JFtv mi ni wenuu...........! 😀


Kisumu tidim, Kisumu tialala!
 
Sidhani kama IEBC wanahusika
Pengine ni NASA wanajaribu kutoka kuthibitisha kuwa wizi ulifanyika. Na hilo ni sanduku wametengeneza wakalitupa na kuita watu

Najiuliza IEBC ni wajinga kiasi gani mpk wakalitupe porini!? Kwann wasingelichoma moto!?
 
Kama waliolipata ni wafugaji haina haja kujiuliza maswali mengi, kwa vile kazi ya mfugaji iko wazi

Akina nani waliliweka huko kichakani ilhali vifaa hivyo vya uchaguzi Tume ndo mdhibiti? Gumzo hapo ndipo
Ata wacha tume kando ,wale representatives wa vyama na reps wa candidates wote walikuwa wapi sanduku likipotea vile?
 
Sidhani kama IEBC wanahusika
Pengine ni NASA wanajaribu kutoka kuthibitisha kuwa wizi ulifanyika. Na hilo ni sanduku wametengeneza wakalitupa na kuita watu

Najiuliza IEBC ni wajinga kiasi gani mpk wakalitupe porini!? Kwann wasingelichoma moto!?
Ndio swali nililojiuliza ata mimi. Kuna vitu logically doesnt make sense. Ata mtoto mdogo angelichoma moto seuze mtu mzima mhalifu
 
Back
Top Bottom