Ngongo
Platinum Member
- Sep 20, 2008
- 20,654
- 35,887
Heshima sana,
Tanzania ya Mwl. ilikuwa juu sana katika siasa za kimataifa. Tanzania ilikuwa kinara katika siasa za ukombozi Kusini mwa Afrika. Mwl. alikuwa Mwenyekiti wa nchi zilizo mstari wa mbele kupigania uhuru wa nchi za Kiafrika hasa Kusini mwa bara la Afrika.
Tanzania ya Mzee Ruksa ilifuta nyayo za Mwl Nyerere ingawa taratibu tulianza kupoteza heshima yetu katika siasa za kimataifa. Tanzania ya Mzee Mkapa na Kikwete ilijaribu kurejea katika nafasi yake ingawa si kwa kiwango cha juu.
Tanzania ya Mzee Magufuli iliacha kabisa masuala yote ya mahusiano ya diplomasia. Mahusiano yetu na majirani zetu yalikuwa hovyo sana.
Kifupi Mzee Magufuli siasa zake zilituacha hoi bin taabani lilipokuja suala mahusiano mazuri na majirani, wafadhili. Tanzania ya Mama inajitahidi kurejea katika nafasi yake ya uongozi hasa wafadhili na majirani.
Vurugu zilizojitokeza huko Msumbiji tuliona nchi ya Rwanda ikipeleka wanajeshi kusaidia kurejesha amani. Ikumbukwe Rwanda si mwanachama wa SADC.
Vurugu zilinazoendelea huko Congo DRC nchi ya Kenya imechukua uongozi kwa kutuma wanajeshi na Rais Mstaafu wa Kenya ni msuluhishi Mkuu.
Tanzania ipo kando ikisubiri Rwanda watuzalishie wakimbizi na kuharibu usalama eneo lote la mikoa ya mipakani.
Tanzania ya Mwl. ilikuwa juu sana katika siasa za kimataifa. Tanzania ilikuwa kinara katika siasa za ukombozi Kusini mwa Afrika. Mwl. alikuwa Mwenyekiti wa nchi zilizo mstari wa mbele kupigania uhuru wa nchi za Kiafrika hasa Kusini mwa bara la Afrika.
Tanzania ya Mzee Ruksa ilifuta nyayo za Mwl Nyerere ingawa taratibu tulianza kupoteza heshima yetu katika siasa za kimataifa. Tanzania ya Mzee Mkapa na Kikwete ilijaribu kurejea katika nafasi yake ingawa si kwa kiwango cha juu.
Tanzania ya Mzee Magufuli iliacha kabisa masuala yote ya mahusiano ya diplomasia. Mahusiano yetu na majirani zetu yalikuwa hovyo sana.
Kifupi Mzee Magufuli siasa zake zilituacha hoi bin taabani lilipokuja suala mahusiano mazuri na majirani, wafadhili. Tanzania ya Mama inajitahidi kurejea katika nafasi yake ya uongozi hasa wafadhili na majirani.
Vurugu zilizojitokeza huko Msumbiji tuliona nchi ya Rwanda ikipeleka wanajeshi kusaidia kurejesha amani. Ikumbukwe Rwanda si mwanachama wa SADC.
Vurugu zilinazoendelea huko Congo DRC nchi ya Kenya imechukua uongozi kwa kutuma wanajeshi na Rais Mstaafu wa Kenya ni msuluhishi Mkuu.
Tanzania ipo kando ikisubiri Rwanda watuzalishie wakimbizi na kuharibu usalama eneo lote la mikoa ya mipakani.