Kenya is broke, finally

Kenya is broke, finally

Mapato yanakusanywa ila wanatumia zaidi ya 60% kulipa madeni ya nje na ndani. Kiuchumi ni bora ukose kulipa mishahara kuliko madeni kama bonds yafikie maturity alafu uingie mitini. Hapo unakuwa defaulted na unafeli vibaya mno na sarafu yako inashuka thamani haraka sana. Pia ni bora usilipe mishahara kuliko nchi ikose huduma za kijamii na kukosa kuagiza bidhaa muhimu. Nchi zetu za kimaskini hizi unakuta waajiriwa wa serikali ni kama 15% ya wananchi, na sio wote hawajalipwa. Sijui idadi ila utakuta wasiolipwa hawafiki 10% ya raia, sasa huwezi kufanya ukichaa kuacha hospitali hazina dawa eti ulipe mishahara yote. Hapo unatafuta priorities kama hela haitoshi.

Kenya tangu wapate uhuru hawakuwahi kosa kulipa mshahara, na watalipa mishahara hii kwa makusanyo ya kodi yanayofuata. Ila wanatakiwa wapunguze matumizi, Kenya ina matumizi makubwa sana ya serikali. Na wapambane na ufisadi.

Tatizo lingine ni miradi isiyozalisha na mikopo mikubwa mikubwa inayofuatana. Haya mambo ya kukopa kwa pamoja ujenge SGR, barabara, ndege na vitu visivyozalisha direct itatufikisha uko. Mfano trilioni za SGR tutazilipa kwa hela hii hii tunayomkamua muuza mkaa. Wakati nchi zenye akili zinakopa zijenge viwanda zizalishe bidhaa faida ndio ilipe mkopo na riba yake. Au basi tukope hela tuanzishe miradi mikubwa ya kilimo. Kwani trilioni ngapi zinahitajika kufunga mifumo ya umwagiliaji watu wakalima mwaka mzima, tena hii inagusa almost kila Mtanzania na faida yake inaanza kurudi mwaka uleule mfumo umeanza.

Tunatumia trilioni 14 kujenga SGR ambayo inabeba watu zaidi kuliko mizigo. Hii sio India au China ya watu zaidi ya bilioni moja. Tumenunua ndege kwa hela nyingi ambavyo Air Tanzania haitokaa ipate faida. Baada ya hapo tubangaize na makusanyo ya PAYE na VAT kulipa mikopo.
Very brainy inputs...
 
it was just a speculation but yesterday finally the DP Rigathi Gashagua aka Right G ...declared bankruptcy to his government.

The so called EA giant has officially declared unable to pay salaries to an indefinite period of time and asking well wishers to intervene the situation.

Right G blamed the handshake government which stole everything in the stoke causing problems and shame to the current administration.

Recently top Kenyan officials visited the neighbors Tanzania for foreign currency to help cover some of the outstanding debts.

Droughts, political and social unrest, are some of the many other things causing the shame to cover the Nation of Kenya.

Kenya on her Kneels
Recently top Kenyan officials visited the neighbors Tanzania for foreign currency to help cover some of the outstanding debts.[emoji3064]
 
Mapato yanakusanywa ila wanatumia zaidi ya 60% kulipa madeni ya nje na ndani. Kiuchumi ni bora ukose kulipa mishahara kuliko madeni kama bonds yafikie maturity alafu uingie mitini. Hapo unakuwa defaulted na unafeli vibaya mno na sarafu yako inashuka thamani haraka sana. Pia ni bora usilipe mishahara kuliko nchi ikose huduma za kijamii na kukosa kuagiza bidhaa muhimu. Nchi zetu za kimaskini hizi unakuta waajiriwa wa serikali ni kama 15% ya wananchi, na sio wote hawajalipwa. Sijui idadi ila utakuta wasiolipwa hawafiki 10% ya raia, sasa huwezi kufanya ukichaa kuacha hospitali hazina dawa eti ulipe mishahara yote. Hapo unatafuta priorities kama hela haitoshi.

Kenya tangu wapate uhuru hawakuwahi kosa kulipa mshahara, na watalipa mishahara hii kwa makusanyo ya kodi yanayofuata. Ila wanatakiwa wapunguze matumizi, Kenya ina matumizi makubwa sana ya serikali. Na wapambane na ufisadi.

Tatizo lingine ni miradi isiyozalisha na mikopo mikubwa mikubwa inayofuatana. Haya mambo ya kukopa kwa pamoja ujenge SGR, barabara, ndege na vitu visivyozalisha direct itatufikisha uko. Mfano trilioni za SGR tutazilipa kwa hela hii hii tunayomkamua muuza mkaa. Wakati nchi zenye akili zinakopa zijenge viwanda zizalishe bidhaa faida ndio ilipe mkopo na riba yake. Au basi tukope hela tuanzishe miradi mikubwa ya kilimo. Kwani trilioni ngapi zinahitajika kufunga mifumo ya umwagiliaji watu wakalima mwaka mzima, tena hii inagusa almost kila Mtanzania na faida yake inaanza kurudi mwaka uleule mfumo umeanza.

Tunatumia trilioni 14 kujenga SGR ambayo inabeba watu zaidi kuliko mizigo. Hii sio India au China ya watu zaidi ya bilioni moja. Tumenunua ndege kwa hela nyingi ambavyo Air Tanzania haitokaa ipate faida. Baada ya hapo tubangaize na makusanyo ya PAYE na VAT kulipa mikopo.
Inaonekana upo vizuri Sana kichwani, ila hapo kwenye SGR kidogo umefikiria juu juu sana
 
Inaonekana upo vizuri Sana kichwani, ila hapo kwenye SGR kidogo umefikiria juu juu sana
Yuko sahihi mkuu SGR itabeba mazao gani tunayozalisha ili tupate faida? Kuna mizigo gani itabeba iweze kufikai kuleta return? Ule mradi sidhani tuliuhitaji kwa wakati huu.
 
Hivi wakati Marais wanakabidhiana nchi huwa haufanyiki ukaguzi wa Mali? Unakubali vipi kuuziwa mbuzi ndani ya gunia? Sasa si raisi aliyepo apeleke muswada bungeji kuondoa Kinga ya Uhuru kushitakiwa wamburuze mahakamani kujibu kuiibia serikali? Sikuwahi kumuamini Ruto hata kidogo kama anaweza kuendesha nchi ni basi tu demokrasia zetu hizi yeyote anakuwa rais.
 
it was just a speculation but yesterday finally the DP Rigathi Gashagua aka Right G ...declared bankruptcy to his government.

The so called EA giant has officially declared unable to pay salaries to an indefinite period of time and asking well wishers to intervene the situation.

Right G blamed the handshake government which stole everything in the stoke causing problems and shame to the current administration.

Recently top Kenyan officials visited the neighbors Tanzania for foreign currency to help cover some of the outstanding debts.

Droughts, political and social unrest, are some of the many other things causing the shame to cover the Nation of Kenya.

Kenya on her Kneels


We, as a country, needs to take the lesson seriously on how Kenya have reached such condition, today is Kenya tomorrow is us, God forbids.
 
Yuko sahihi mkuu SGR itabeba mazao gani tunayozalisha ili tupate faida? Kuna mizigo gani itabeba iweze kufikai kuleta return? Ule mradi sidhani tuliuhitaji kwa wakati huu.
Mkuu, Kuna huu ushoroba wa kati unaufuatilia vizuri?. SGR itaongeza ufanisi wa bandari ya Dar na Tanga by 100%.

Mkuu, hivi huoni jinsi Burundi, DRC na Uganda wanavyohangaika kuhusu hii reli?. Tukiachilia mbali mizigo mengine ya ndani, bandari ya Dar pekee ikitumiwa na hizi nchi tatu by 80% na Uganda na South Sudan by 50% ya mizigo yao ya hivi Sasa tu, tunauwezo wa kupata mapato ya nchi nzima by 50%.

Lengo la hizi nchi kukimbilia Sana hii SGR ni kutaka kuanza kichimba madini yao mazito ambayo kwa Sasa hawawezi kuyachimba kwasababu hawawezi kuyasafirisha nje ya nchi. Kwahiyo usiangalie miaka 5 ijayo, huu ni mradi utakaodumu miaka 100 ijayo. Huu mradi "stimulating effect on the economy" ni mkubwa Sana mkuu, hasa kwa DRC, Burundi na Uganda.
 
Hivi wakati Marais wanakabidhiana nchi huwa haufanyiki ukaguzi wa Mali? Unakubali vipi kuuziwa mbuzi ndani ya gunia? Sasa si raisi aliyepo apeleke muswada bungeji kuondoa Kinga ya Uhuru kushitakiwa wamburuze mahakamani kujibu kuiibia serikali? Sikuwahi kumuamini Ruto hata kidogo kama anaweza kuendesha nchi ni basi tu demokrasia zetu hizi yeyote anakuwa rais.
Mkuu, wanajaribu kutafuta visingizio tu, tatizo la Kenya ni hili hapa


 
Mkuu, Kuna huu ushoroba wa kati unaufuatilia vizuri?. SGR itaongeza ufanisi wa bandari ya Dar na Tanga by 100%.

Mkuu, hivi huoni jinsi Burundi, DRC na Uganda wanavyohangaika kuhusu hii reli?. Tukiachilia mbali mizigo mengine ya ndani, bandari ya Dar pekee ikitumiwa na hizi nchi tatu by 80% na Uganda na South Sudan by 50% ya mizigo yao ya hivi Sasa tu, tunauwezo wa kupata mapato ya nchi nzima by 50%.

Lengo la hizi nchi kukimbilia Sana hii SGR ni kutaka kuanza kichimba madini yao mazito ambayo kwa Sasa hawawezi kuyachimba kwasababu hawawezi kuyasafirisha nje ya nchi. Kwahiyo usiangalie miaka 5 ijayo, huu ni mradi utakaodumu miaka 100 ijayo. Huu mradi "stimulating effect on the economy" ni mkubwa Sana mkuu, hasa kwa DRC, Burundi na Uganda.
Labda kwa kuitegemea hiyo mizigo ya nje sawa...
Una maana kwa sasa hii reli iliyopo imezidiwa mizigo? Tatizo naliona liko bandarini zaidi kuliko kusafirisha mizigo yenyewe...
Waendelee kuijengea hiyo bandari ya Dar uwezo wa kutoa mizigo sababu hata hiyo SGR ikikamilika kwa utendaji huo wa bandari bado itakuwa haisaidii kitu
 
Labda kwa kuitegemea hiyo mizigo ya nje sawa...
Una maana kwa sasa hii reli iliyopo imezidiwa mizigo? Tatizo naliona liko bandarini zaidi kuliko kusafirisha mizigo yenyewe...
Waendelee kuijengea hiyo bandari ya Dar uwezo wa kutoa mizigo sababu hata hiyo SGR ikikamilika kwa utendaji huo wa bandari bado itakuwa haisaidii kitu
Mkuu, reli zote za zamani, yaani TAZARA, reli ya kati na Ile reli ya Kenya RVR, zote ziliharibika kiasi kikubwa Sana zikawa ufanisi wake ni chini, ukipakia mzigo wako, uhakika wa kufika ni mdogo, zilikua zikichukua hadi wiki kufikisha mzigo kutokana na uchakavu wa reli na trains zenyewe, kipindi Cha mvua nyingi, ndio haziendi kabisa, ndio sababu wafanyabiashara wakakimbilia usafiri wa barabara.

Mkuu, fikiria zaidi nchi za Burundi, DRC, Rwanda, Uganda na South Sudan, kuliko kufikiria zaidi Tanzania.

Mkuu, akili ya kawaida tu inakujulisha kwamba, huwezi kuboresha uwezo wa bandari kupokea mzigo bila kuwezesha uwezo wa mandarin kuondoa mzigo wanaopokea, lazima vifanyika sambamba
 
Wabongo hivi Kuna nafasi huko kwenu nihamie ama niendelee kuvumilia kuwa mkenya?
Njoo karibu sana....huku hatuandamani eti bei ya unga ishuke....huku hakunaga njaa za kilo 1 ya unga....ni aibu sana kulilia chakula Bora ulilie mke
 
Alafu data za uchumi wa Kenya ni za kupika ( fabricated) na ukweli umedhihirika....siku zote njia ya mwongo ni fupi. Huwezi sema eti una GDP ya 106B USD alafu ushindwe kuwa na food security na normal salary to employees. Acheni swaga zenu nyinyi ni masikini ila mnajificha kwenye kuongea English [emoji23][emoji23]
 
Mkuu, wanajaribu kutafuta visingizio tu, tatizo la Kenya ni hili hapa



Mkuu matumizi ya serikali zetu ni makubwa mno.
Pia nimeona jamaa wa video ya chini anasema Kuna bond zinamature mwaka kesho ambazo zinahitaji pesa nyingi zaidi ya hizi walizolipa nikajiuliza huku kwetu sisi zinamature lini? Hivi upewe mkopo toka 2014 unajua miaka nane ijayo unapaswa kulipa hata huanzi kudunduliza kidogo kidogo unasubiri mpk siku ya kulipa ndio ukombe hazia yote kweli!!!
Tatizo lingine naloliona kwenye hiyo mikopo ni wazungu kuja tu na project kupresent na sisi kuingia kichwa kichwa bila kufanya utafiti wetu kuangalia kwa mapana kama zitarudisha hela.
Ila nimependa mjadala wao angalau walishajadili wakategemea haya kutokea tofauti na sisi ambao bado hata hatujui lini tunatumbukia.
 
Mkuu, reli zote za zamani, yaani TAZARA, reli ya kati na Ile reli ya Kenya RVR, zote ziliharibika kiasi kikubwa Sana zikawa ufanisi wake ni chini, ukipakia mzigo wako, uhakika wa kufika ni mdogo, zilikua zikichukua hadi wiki kufikisha mzigo kutokana na uchakavu wa reli na trains zenyewe, kipindi Cha mvua nyingi, ndio haziendi kabisa, ndio sababu wafanyabiashara wakakbilia usafiri wa barabara.

Mkuu, fikiria zaidi nchi za Burundi, DRC, Rwanda, Uganda na South Sudan, kuliko kufikiria zaidi Tanzania.

Mkuu, akili ya kawaida tu inakujulisha kwamba, huwezi kuboresha uwezo wa bandari kupokea mzigo bila kuwezesha uwezo wa mandarin kuondoa mzigo wanaopokea, lazima vifanyika sambamba
Hapo nimekupata mkuu lakini unaonaje unakuwa na reli ambayo inafanya kazi zaidi ya miaka hamsini halafu inachakaa kabisa bila hata kuweza kurekebishika. Ninachomaanisha ni kwamba kama hizo reli zilitumika mpk kuchakaa namna hii na mpk Sasa tukawa hatuna cash ya kujenga nyingine mpk tukope je hii tunayojenga tunahakikisha vipi kwamba haitaangukia huko huko. Mashirika yetu yamekuwa yakiliwa na watendaji na bila serikali kubana hata hii miradi itafanya kazi miaka mia na bado ikichakaa tusiw ena cash ya kujenga mingine.
 
Back
Top Bottom