Kenya is broke, finally

Kenya is broke, finally

Madeni na mikopo yamekuwa siyo himilivu kwani makusanyo ya kodi yapo level ile ile enzi za utawala wa Uhuru Kenyatta tofauti ni kuwa madeni yamewiva na lazima yalipwe hivyo serikali ya Mh. William Ruto hawana jinsi bali kuyapa malipo ya madeni / mikopo kipaumbele na kukuta hela ya kulipa mishahara haipo ktk hazina .

Tanzania nasi tujifunze kuhusu kukopa sana na kudai kuwa madeni na mikopo ni Himilivu tujiulize wenzetu wamekwama wapi.

Wakubwa walisema ukiona mwenzio ananyolewa nywele kwa lazima inabidi nasi tutie kichwa maji maana tunaweza kuangukia ktk hali Kenya inayopitia kuzidiwa na dhamana ya kulipa mikopo, madeni na riba iliyoiva
Kwahiyo Unakubariana na Ndugai?
 
Kweli maisha yanaenda kasi sana, kutoka kuwa Taifa kubwa Afrika Mashariki lililoongoza ile movement ya kujitenga kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki hadi kupelekea kuvunjika miaka ile hadi kuwa Taifa la kushindwa kulipa watumishi Mishahara🤔

Waswahili wanasema mwenzio akinyolewa zako tia maji.

Ni wakati wa Sisi Watanzania kujipanga, kama hakutakuwa na udhibiti wa fedha za Umma na watu kupiga cha Juu kama ile tenda ya SGR badala ya 660 Bilioni hadi 1.1Trilioni nasi tutafika huko.

Wananchi tuna nafasi ya Kuamua viongozi wa Adilifu 2025 kabla mambo hayajawa magumu zaidi.

Mungu awasaidie Wakenya kipindi hiki cha Ukata wanachopitia
 
Mkuu matumizi ya serikali zetu ni makubwa mno.
Pia nimeona jamaa wa video ya chini anasema Kuna bond zinamature mwaka kesho ambazo zinahitaji pesa nyingi zaidi ya hizi walizolipa nikajiuliza huku kwetu sisi zinamature lini? Hivi upewe mkopo toka 2014 unajua miaka nane ijayo unapaswa kulipa hata huanzi kudunduliza kidogo kidogo unasubiri mpk siku ya kulipa ndio ukombe hazia yote kweli!!!
Tatizo lingine naloliona kwenye hiyo mikopo ni wazungu kuja tu na project kupresent na sisi kuingia kichwa kichwa bila kufanya utafiti wetu kuangalia kwa mapana kama zitarudisha hela.
Ila nimependa mjadala wao angalau walishajadili wakategemea haya kutokea tofauti na sisi ambao bado hata hatujui lini tunatumbukia.
Mkuu, tofauti kati ya Kenya na Tanzania ni kwamba, Tanzania tunajaribu Sana kuishi kulingana na uwezo wetu, hatujikwezi.

Kenya ni watu wa kujikweza na kuonekana wanauchumi mzuri. Serikali ya Kenya haina vipaumbele vya nchi, wao siasa, ukabila na "prestige" ndivyo vinavyoongoza maamuzi ya kiuchumi.

Hivi nchi masikini Kama Kenya itawezaje kulipa "salaries" hadi madiwani?, yaani karibia Kila mbunge anapewa ulinzi na serikali, nchi kuwa na wabunge wa kitaifa na bunge la "senate", gharama ya kuendesha serikali ya Kenya pekee ni zaidi ya pesa zote za maendeleo Kenya.
 
Hapo nimekupata mkuu lakini unaonaje unakuwa na reli ambayo inafanya kazi zaidi ya miaka hamsini halafu inachakaa kabisa bila hata kuweza kurekebishika. Ninachomaanisha ni kwamba kama hizo reli zilitumika mpk kuchakaa namna hii na mpk Sasa tukawa hatuna cash ya kujenga nyingine mpk tukope je hii tunayojenga tunahakikisha vipi kwamba haitaangukia huko huko. Mashirika yetu yamekuwa yakiliwa na watendaji na bila serikali kubana hata hii miradi itafanya kazi miaka mia na bado ikichakaa tusiw ena cash ya kujenga mingine.
Swali zuri Sana kaka. Sijui sababu zilizosababisha reli Yao kushindwa kuendelea, lakini huku Tanzania sababu kubwa ni mabadiliko ya sera za uchumi na mabadiliko ya malengo.

TAZARA lengo la kujengwa kwake ilikua ni kuzisaidia nchi za kusini mwa Afrika kutotegemea bandari za Makaburu katika kuisafirisha mizigo yao, wengi walikua wanategemea bandari za Afrika kusini, kwahiyo kabla ya 1994, TAZARA ilikua ikipata mzigo mkubwa Sana, baada ya uhuru wa Afrika kusini, nchi nyingi ziliamua kupirishia mizigo yao huko, kwahiyo TAZARA ikaanza kuyumba Sana.

Reli ya kati tuliirithi kutoka kwa wakoloni, hatukua na utaalamu wowote wa kuiendesha, Kama utakumbuka viwanda na mashirika ya serikali karibu yote yalifilisika.

Hivi Sasa serikali inajaribu Sana kushirikisha "private sector" katika kuiendesha haya mashirika ya Imma Kama ilivyo "UDART", ni matumaini yangu hata hii SGR pia itakua hivyo.
 
Mkuu, tofauti kati ya Kenya na Tanzania ni kwamba, Tanzania tunajaribu Sana kuishi kulingana na uwezo wetu, hatujikwezi.

Kenya ni watu wa kujikweza na kuonekana wanauchumi mzuri. Serikali ya Kenya haina vipaumbele vya nchi, wao siasa, ukabila na "prestige" ndivyo vinavyoongoza maamuzi ya kiuchumi.

Hivi nchi masikini Kama Kenya itawezaje kulipa "salaries" hadi madiwani?, yaani karibia Kila mbunge anapewa ulinzi na serikali, nchi kuwa na wabunge wa kitaifa na bunge la "senate", gharama ya kuendesha serikali ya Kenya pekee ni zaidi ya pesa zote za maendeleo Kenya.
Mkuu happy sawa ila hata hivyo wanajitahidi sana kumbuka wao hawana rasilimali vitu kama sisi na karibu nusu ya ardhi yao ni kame balaa lakini bado wamefurukuta imagine wangekuwa sisi wangekuwa wapi
 
Mkuu happy sawa ila hata hivyo wanajitahidi sana kumbuka wao hawana rasilimali vitu kama sisi na karibu nusu ya ardhi yao ni kame balaa lakini bado wamefurukuta imagine wangekuwa sisi wangekuwa wapi
Bado ni kama kamari kutabiri kuwa wangekua njema kutokana na ukabila. Kenya hata hivyo walivyo leo wangeachana na ukabila toka zamani wangekua mbali. Wana ukabila wa kipumbavu moja ya element kuu ya akili mbovu ya mtu mweusi licha ya kuchapwa bakora na mzungu na kuletewa shule.
 
Sio kwamba serikali imeshindwa kulipa mishahara ya wafanyikazi wa umma Bali Ni imecheleweshwa tu,bt everything shall be sorted out within a short period of time.

And don't forget that Kenya will continue to be the economical giant of EA despy all these financial constraints in the country.
Only if EAC was Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, DRC
 
It was just a speculation but yesterday finally the DP Rigathi Gashagua aka Right G declared bankruptcy to his government.

The so called EA giant has officially declared unable to pay salaries to an indefinite period of time and asking well wishers to intervene the situation.

Right G blamed the handshake government which stole everything in the stoke causing problems and shame to the current administration.

Recently top Kenyan officials visited the neighbors Tanzania for foreign currency to help cover some of the outstanding debts.

Droughts, political and social unrest, are some of the many other things causing the shame to cover the Nation of Kenya.

Kenya on her Kneels
Meanwhile riggy G, rutto and mudavadi each drew 1B KSH for private cars
 
Yawezekana ikawa hivyo ila kama kweli jamaa hawana hela za kulipa basi Ruto ana safari ngumu.

Na mzee RAO atacheza na hii issue hadi handshake au wafungue server!.

...
Anapenda mambo ya umbea eti Russia hii vita akifikisha mwaka anafilisika. Wao vurugu zimetokea wiki tu hawana pesa.
 
Swali zuri Sana kaka. Sijui sababu zilizosababisha reli Yao kushindwa kuendelea, lakini huku Tanzania sababu kubwa ni mabadiliko ya sera za uchumi na mabadiliko ya malengo.

TAZARA lengo la kujengwa kwake ilikua ni kuzisaidia nchi za kusini mwa Afrika kutotegemea bandari za Makaburu katika kuisafirisha mizigo yao, wengi walikua wanategemea bandari za Afrika kusini, kwahiyo kabla ya 1994, TAZARA ilikua ikipata mzigo mkubwa Sana, baada ya uhuru wa Afrika kusini, nchi nyingi ziliamua kupirishia mizigo yao huko, kwahiyo TAZARA ikaanza kuyumba Sana.

Reli ya kati tuliirithi kutoka kwa wakoloni, hatukua na utaalamu wowote wa kuiendesha, Kama utakumbuka viwanda na mashirika ya serikali karibu yote yalifilisika.

Hivi Sasa serikali inajaribu Sana kushirikisha "private sector" katika kuiendesha haya mashirika ya Imma Kama ilivyo "UDART", ni matumaini yangu hata hii SGR pia itakua hivyo.
Naona tatizo mahali yaani ujenge reli kwa matrilioni halafu umuite mwekezaji kwa ajili ya kuisimamia tu ale hela...kwamba tumeshindwa kweli kuisimamia miradi yetu ikaleta faida? Kama ni hivyo hao wawekezaji nao ingepaswa wahusishwe kwenye ujenzi watie mzigo na sio kuja tushapigwa tozo mpk basi wao waanze kuuza tiketi.
Hivi ni kweli hatukuwa na utaalamu wa kuisimamia miradi yetu au watu waliinywa na kulindana kwingi?
 
Yaani huyo Gachagua ndio bure kabisa badala kutafuta solution anasingizia uhuru ..nchi za kiafrika tu a safari ndefu Sana wao posho za mabilioni na wake zao wanajipa ila wafanyakazi wengine hawajalipwa ...hii ni second time nchi Iko broke wanaelekea kubaya eti hawataki kukopa wanategemea makusanyo Hadi next week
 
Mkuu happy sawa ila hata hivyo wanajitahidi sana kumbuka wao hawana rasilimali vitu kama sisi na karibu nusu ya ardhi yao ni kame balaa lakini bado wamefurukuta imagine wangekuwa sisi wangekuwa wapi
Mkuu, wao hujisifia kuwa na "hard working and educated citizens, pia wanasema nchi yao Iko na uchumi mkubwa.

Siku hizi mambo muhimu yanayoitajika Ili nchi iweze kupata maendeleo kwa haraka ni
1)Educated human resource
2)Capital
3)Technology
Kenya huwa wanajisifu kuwa navyo vyote hivi, kwanini hawaendelei wanatoa kisingizio Cha kukosa Ardhi na rasilimali?.
Israel, Taiwan, Singapore, South Korea na Sychelles, wote hawana Ardhi Wala rasilimali yoyote, mbona wanaendelea kwa Kasi?
 
Naona tatizo mahali yaani ujenge reli kwa matrilioni halafu umuite mwekezaji kwa ajili ya kuisimamia tu ale hela...kwamba tumeshindwa kweli kuisimamia miradi yetu ikaleta faida? Kama ni hivyo hao wawekezaji nao ingepaswa wahusishwe kwenye ujenzi watie mzigo na sio kuja tushapigwa tozo mpk basi wao waanze kuuza tiketi.
Hivi ni kweli hatukuwa na utaalamu wa kuisimamia miradi yetu au watu waliinywa na kulindana kwingi?
Mkuu, wakati tunapata uhuru kulikua na madaktari 3 na Engineer mmoja nchi nzima, tuliirithi bandari tatu, reli mbili ya Tanga - Moshi na Central corridor, kweli tungeweza kuiendesha wenyewe?.

Kuhusu kuendesha, itakua Kama "UDART", sio lazima kuendeshwa na wageni, inaendeshwa na watanzania lakini sio serikali. Kwa kufanya hivyo tunawapa watanzania ajira na uwezo wa kuendesha uchumi wao.

Mkuu, serikali haipaswi kufanya biashara, inapaswa ijenge miundombinu Ili wananchi wafanye biashara, serikali imejenga Barbara lakini raia ndio wenye magari yanayotumia hizo Barbara, hata reli ni hivyo hivyo.
 
Back
Top Bottom