Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Leo Mahakama ya juu kabisa nchini Kenya inatarajiwa kutoa hukumu ya kesi ya uchaguzi wa urais.
Kesi hii imekuwa ikisikilizwa tangu mwanzoni mwa wiki na jopo la majaji 7.
Kesi hii ilifunguliwa na wanasiasa wa Muungano wa Upinzani NASA, wakidai kuwa ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta ulitokana na hila zilizofanywa kupitia mfumo wa Computer wa Tume huru ya uchaguzi IEBC na wanataka matokeo hayo yafutwe na uchaguzi kuitishwa upya ndani ya siku 60.
Kwa upande wa pili tume ya uchaguzi IEBC na mawakili wa chama cha Jubilee wanasisitiza hakuna ushahidi wa kuyafutilia mbali matokeo ya uchaguzi yaliyompa Rais Uhuru Kenyatta ushindi.
======== ======== =========
Update;
==>Ulinzi mkali nje ya Mahakama ya Juu Nairobi, huku kukutarajiwa kutoa uamuzi kuhusu kesi ya uchaguzi wa urais muda mfupi kuanzia sasa
==>Odinga awasili mahakamani akiambatana viongozi wenzako wa NASA
Kesi hii imekuwa ikisikilizwa tangu mwanzoni mwa wiki na jopo la majaji 7.
Kesi hii ilifunguliwa na wanasiasa wa Muungano wa Upinzani NASA, wakidai kuwa ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta ulitokana na hila zilizofanywa kupitia mfumo wa Computer wa Tume huru ya uchaguzi IEBC na wanataka matokeo hayo yafutwe na uchaguzi kuitishwa upya ndani ya siku 60.
Kwa upande wa pili tume ya uchaguzi IEBC na mawakili wa chama cha Jubilee wanasisitiza hakuna ushahidi wa kuyafutilia mbali matokeo ya uchaguzi yaliyompa Rais Uhuru Kenyatta ushindi.
======== ======== =========
Update;
==>Ulinzi mkali nje ya Mahakama ya Juu Nairobi, huku kukutarajiwa kutoa uamuzi kuhusu kesi ya uchaguzi wa urais muda mfupi kuanzia sasa
==>Odinga awasili mahakamani akiambatana viongozi wenzako wa NASA