Hivi punde
JF-Expert Member
- Apr 1, 2017
- 2,554
- 8,587
Malkia wa urembo katika gereza kuu la wanawake la Lang'ata jijini Nairobi amehukumiwa kifo baada ya kupatikana na kosa la kumuua mpenzi wake kwa kumchoma kisu mara 22.
Miss huyo aliyefahamika kwa jina la Ruth Wanjiku Kamande amekutwa na kosa la kumuua mpenzi wake Farid Mohammed katika mtaa wa Buruburu, Nairobi Septemba 20,2015.
Jaji Jessie Lessit amesema upande wa mashtaka umedhibitisha kesi hiyo ya mauaji bila shaka yoyote.
Jaji huyo amesema hukumu hiyo inatakiwa kuwa funzo kwa vijana wajue kwamba ββsi vyema kumuua mpenzi wako, ni vyema ukaamua kuondoka zako."
Wakili wake Joyner Okonjo amesema mfungwa huyo alikuwa amejenga uhusiano wa karibu na Mungu tangu kuzuiliwa mwaka 2015 na kwamba alikuwa amesilimu na kuswali mara tano kwa siku.
kwa mujibu wa wakili wake ,wakati wa kukamatwa kwake, mwanamke huyo mwenye miaka 25 sasa alikuwa ndio tu amejiunga na Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta (JKUAT) kusomea masomo ya biashara.
"Mwanamume huyo aliyeuawa alikuwa na miaka 24 wakati huo alikuwa mjane na alikuwa anategemewa na ndugu wengine, haki ilitakiwa kutekelezwa," wakili wa mashtaka amesema
Akijitetea mahakamani hapo mwanamke huyo amesema kwamba mgogoro kati yake na marehemu ulizidi baada yeye kugundua kadi ya hospitali iliyoashiria kwamba Mohammed alikuwa anapokea matibabu ya Ukimwi.
Amesema baada ya kumwuliza alimgombeza huku akimwambia heri wafe wote kuliko hali yake ya Ukimwi itambulike hadharani.
Amesema alimchoma kisu mpenzi wake baada ya kisu cha kutumiwa jikoni kumwangukia wakipigana na hapo akamdunga kisu mara kadhaa.
Miss huyo aliyefahamika kwa jina la Ruth Wanjiku Kamande amekutwa na kosa la kumuua mpenzi wake Farid Mohammed katika mtaa wa Buruburu, Nairobi Septemba 20,2015.
Jaji Jessie Lessit amesema upande wa mashtaka umedhibitisha kesi hiyo ya mauaji bila shaka yoyote.
Jaji huyo amesema hukumu hiyo inatakiwa kuwa funzo kwa vijana wajue kwamba ββsi vyema kumuua mpenzi wako, ni vyema ukaamua kuondoka zako."
Wakili wake Joyner Okonjo amesema mfungwa huyo alikuwa amejenga uhusiano wa karibu na Mungu tangu kuzuiliwa mwaka 2015 na kwamba alikuwa amesilimu na kuswali mara tano kwa siku.
kwa mujibu wa wakili wake ,wakati wa kukamatwa kwake, mwanamke huyo mwenye miaka 25 sasa alikuwa ndio tu amejiunga na Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta (JKUAT) kusomea masomo ya biashara.
"Mwanamume huyo aliyeuawa alikuwa na miaka 24 wakati huo alikuwa mjane na alikuwa anategemewa na ndugu wengine, haki ilitakiwa kutekelezwa," wakili wa mashtaka amesema
Akijitetea mahakamani hapo mwanamke huyo amesema kwamba mgogoro kati yake na marehemu ulizidi baada yeye kugundua kadi ya hospitali iliyoashiria kwamba Mohammed alikuwa anapokea matibabu ya Ukimwi.
Amesema baada ya kumwuliza alimgombeza huku akimwambia heri wafe wote kuliko hali yake ya Ukimwi itambulike hadharani.
Amesema alimchoma kisu mpenzi wake baada ya kisu cha kutumiwa jikoni kumwangukia wakipigana na hapo akamdunga kisu mara kadhaa.