Kenya ni taifa lililokomaa katika ubepari. Badala ya kuwapiga vita na kuwachukia tujifunze kutoka kwao na historia yetu

Kenya ni taifa lililokomaa katika ubepari. Badala ya kuwapiga vita na kuwachukia tujifunze kutoka kwao na historia yetu

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Ziara ya Rais Samia Kenya imewaibua wafahidhina makanjanja wasiojua chochote kuhusu umuhimu wa mahusiano mazuri kwa manufaa biashara na uchumi kati ya nchi mbili.

Wameibuka vihiyo wenye mawazo ya kijima wanaofikiri vita vya kibiashara na mahusiano mabovu katika ya Kenya na Tanzania yana faida kwetu Tanzania.

Inashangaza kuona maelfu ya nyuzi za kumpinga Rais Samia zikipanda jukwaani baada ya kuonyesha muelekeo wa kurejesha uhusiano wetu na Kenya uliporomoka vibaya miaka mitano iliyopita na kupelekea kushuka vibaya sana kwa ujazo wa biashara kati ya nchi hizi mbili.

Kuna watu wanalia na kupiga mayowe hata Kenya kuuziwa gesi na Tanzania wakisema haitutoshi, wameacha kelele za Stiglers Gorge sasa wamerudi kwenye gesi tena waliyosema imepewa mabeberu.

Nyie wafahidhina uchwara mnaofikiri Kenya inainyonya tu Tanzania ndio maana imepiga hatua kubwa katika uchumi wa viwanda kutuzidi isomeni historia vizuri muone ni jinsi gani Kenya pamoja na matatizo yake mengi walivyojenga uchumi wao endelevu wa soko wakati sisi tunakomaa na ujamaa wetu na sera kujifungia ndani kwa takribani ya miongo 3, miaka 24 ya Nyerere na 5 ya Magufuli.
 
Kama gesi ni muhimu kwa viwanda na viwanda vyetu vinaihitaji kwanini tuharakishe hivyo kuwapa wao?

Hii gesi ni ya nchi hii. Ilibidi tueleweshwe wenye viwanda wa hapa wamekwama wapi mpaka hawawezi pewa gesi kwanza
 
Ni Kenya iliyokomaa au waingereza waliowekeza mle huku Kenya na wakenya wakiambulia umaskini kuliko hata watanzania ukiachia wachache wenye madaraka? Umaskini wa mwananchi wa kawaida wa Kenya ni mkubwa kuliko wa mwananchi maskini wa Tanzania.
 
Hatuwapi. Wananunua.

Kama gesi ni muhimu sana kwetu tuongeze matumizi ya bomba la mafuta kutoka chini ya asilimia 10 ya sasa.

Kama gesi ni muhimu kwa viwanda Na viwanda vyetu vinaihitaji kwanini tuharakishe hivyo kuwapa wao?

Hii gesi ni ya nchi hii. Ilibidi tueleweshwe wenye viwanda wa hapa wamekwama wapi mpaka hawawezi pewa gesi kwanza
 
Wanashangaza kweli ujamaa wenyewe uliwashinda wakiwa vijana Leo hii wazee watauweza kweli. Namuheshimu sana Tuntemeke Sanga, Kambona, Prof. Baregu nk waliomwambia wazi bila kificho Nyerere wetu ujamaa sio dili, ubeberu ndo maisha yawatu, hatukatai udugu na wajamaa ila tusiufanyie kazi sana kama kuna maeneo ya kuchota tuchote twende mbele.
 
Huku tukiamini kutekana kutaleta maendeleo, na kutumia maguvu mengi Bila akili. Hata ukitizama mawaziri wa Kenya na tz utaona wakenya wapo serious kwenya ajenda zao hata kama nako kuna mafisadi lkn huwezi linganisha na wa kwetu
 
Vilaza wenye mawazo ya utopian hawatakuelewa, lazima mama akaze na msimamo wake wa kiliberali na soko.huria ndio kitu pekee kitaondoa mentality za utegemezi ,ulalamishi na lawama vichwani mwa Watzn.

Nawafahamu vizuri wakenya nimefanya nao Kazi kwenye kampuni zao ni kuchapa Kazi sio utoto wa excuses nyingi za Watzn wajinga wajinga
 
Kama gesi ni muhimu kwa viwanda Na viwanda vyetu vinaihitaji kwanini tuharakishe hivyo kuwapa wao?

Hii gesi ni ya nchi hii. Ilibidi tueleweshwe wenye viwanda wa hapa wamekwama wapi mpaka hawawezi pewa gesi kwanza
Usiwe mpumbavu kama Jiwe
 
Back
Top Bottom