Kenya: Nyumba ya Makamu wa Rais William Ruto yashambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267

Watu wasiojulikana wameshambulia nyumbani ya mashambani ya Makamu wa Rais wa Kenya William Ruto Magharibi mwa Uasin Gishu Kaunti, ripoti zinasema.

Ripoti katika eneo hilo zinasema kuwa washambuliaji hao waliwashinda nguvu polisi mmoja katika lango la nyumba hiyo na kuingia ndani.

Ufyatulianaji wa risasi uliendelea katika nyumba hiyo ambayo imezungukwa na maafisa wa polisi.

Bwana Ruto hakuwepo wakati huo.

Kisa hicho kinajiri siku 10 kabla ya Kenya kufanya uchaguzi wa Rais, Ubunge na ule wa Kijimbo.

Makamu wa Rais alikuwa alikuwa ameondoka saa chache kabla ya uvamizi huo ili kuhudhuria mkutano wa kampeni katika mji wa Kitale, ambapo alijiunga na Rais Uhuru Kenyatta.

Kenyatta anatetea kiti chake cha urais mwezi ujao.

Huku uchaguzi wa 2013 ukifanyika kwa njia ya amani kulikuwa na ghasia mbaya za baada ya uchaguzi 2007 ambazo zilisababisha vifo vya watu 1000 huku wengine 600,000 wakiwanchwa bila makao

Hata hivyo wataalamu wanasema hawatarajii kuona kiwango cha ghasia kama hicho kufuatia uchaguzi wa Agosti 8.

Chanzo: BBC

PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana

~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 

Hivi yale ' masalia ' ya Umafia wa aliyekuwa ' Mafia ' Mkuu nchini Kenya Marehemu Nicholas Biwott ( anayesifika kwa mauaji ya Wanasiasa wengi nchini Kenya ) yamemalizwa?
 
Hivi yale ' masalia ' ya Umafia wa aliyekuwa ' Mafia ' Mkuu nchini Kenya Marehemu Nicholas Biwott ( anayesifika kwa mauaji ya Wanasiasa wengi nchini Kenya ) yamemalizwa?
Mkuu.. Kwa namna siasa za Kenya kwa sasa na nikipima kifo cha Waziri Nkaissery

Nashidwa kuelewa uelekeo wake.!

Tuwaombee amani itawale jirani zetu
 
Huo ni mpango wa kuleta tension kwenye uchaguzi ili watumie jeshi. Hii ni movie part 1
 
Wakenya poleni sana, umakini unatakiwa.

Usinisahau kwenye Baraza Jipya.
 
Siasa na madaraka ni kitu kibaya sana hawa jamaa walianza na kipindupindu sasa mashambulizi this time Kenya mambo magumu
 
Mkuu.. Kwa namna siasa za Kenya kwa sasa na nikipima kifo cha Waziri Nkaissery

Nashidwa kuelewa uelekeo wake.!

Tuwaombee amani itawale jirani zetu

Na watauwana sana tu Mkuu. Taarifa za chini kabisa kutoka kwa ' wafuatiliaji ' wa Siasa waliopo huko nchini Kenya wanasema kwamba kuna uwezekano Raila Odinga na mwenzake Kalonzo Musyoka safari hii wakaibuka washindi kutokana na kwamba sasa wamejipanga kwa hila / hujuma / ngendembwe zote na kuna mahala nasikia wameshamshika pabaya Kenyata na Ruto hivyo kupelekea wao kuwa na hali mbaya.

Kuanzia sasa na hadi siku moja kabla ya upigwaji Kura hizo tutegemee makubwa kwani kama akina Uhuru na William walisababisha yale ' mauaji ' makubwa yaliyopelekea kuwa na post election violence nina uhakika hata safari hii tena baada ya kuona wanaelekea kushindwa basi ndiyo wakasababisha ' mauaji ' makubwa mno.
 
He is enforcer of the president. The guy who do all the dirty jobs. Sometimes shit hit the fan, and you reap what you saw. Ukitumia nguvu pia watu watakufuata kwa nguvu. Action and reaction are equal and opposite.
 
Breaking news inaonekana washambulizi ni wasomali
 
If you hear the gunmen have been neutralized, killed and no bodies seen just know Osama mission like executed.
Anyway let's watch.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…