Kenya: Polisi washutumiwa kuwaua watu 15 kiholela

Kenya: Polisi washutumiwa kuwaua watu 15 kiholela

Masi Lambo

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2020
Posts
532
Reaction score
360
Kenya: Polisi washutumiwa kuwaua watu 15 kiholela

Mamlaka inayoangazia utendakazi wa polisi nchini Kenya IPOA, Jumatano ilisema kwamba Wakenya wapatao 15 wameuawa na polisi katika taifa hilo la Afrika Mashariki katika kipindi hiki ambacho kumewekwa marufuku ya kutoka nje usiku, kati ya masharti mengine, kama hatua za kudhibiti kasi ya ongezeko la maambukizi ya virusi vya Corona.

Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa mjini Nairobi na mamlaka hiyo, maafisa sita wa polisi watashtakiwa kwa makosa ya mauaji na unyanyasaji, baadhi wakituhumiwa kuhusika kwa vitendo vya kufyatua risasi kiholela dhidi ya raia wakati wakitekeleza masharti ya marufuku hiyo.

Polisi pia wanatuhumiwa kwa kutumia nguvu kupita kiasi badala ya kutii sheria wakati wakitekeleza majukumu yao.
Nalo shirika la umoja wa mataifa la kutetea haki za binadamu, pia linawashutumu polisi wa Kenya kwa makosa mbalimbali, ikiwa ni pamoja na mauaji na unyanayasaji wa kingono kwa baadhi ya raia.

Mtu ajisalimisha kwa polisi wa Kenya.

1591880278636.png
 
Back
Top Bottom