Kenya vs Tanzania: Mbona Kuna Chuki?


Umeandika andika hata sijui kama umesoma na kuhariri au ulibonyeza send tu.
Islamic bank kwani ya Wapwani?? Hiyo ni biashara na waloanzisha wana malengo yao, binafsi sijaifuata wala kuwa na haja nayo maana nimejitosheleza kwenye benki ninazotumia, ila zaidi ya yote nategemea kwa wao kuwapa Wakenya mikopo sio favor, ila ni biashara kama nyingine.

Hayo unayozungumzia ya EPA mara mitumba bado ni maamuzi ya kibiashara yasiyohusiana na undugu, wanaokubali au kukataa wanafanya hivyo kwa kuzingatia mahesabu yao na maslahi wala hamna chochote cha undugu hapo. Biashara haina undugu, haina urafiki ila maslahi, ukija kwangu ofisini muda wa kazi aisei tuongee mambo ya deals, matangazo ya zabuni/tenders, fursa za uwekezaji, mahesabu ya hisa n.k. Usije kuniletea hadithi sijui za undugu wala udada, hayo subiri tukikutana nje kwenye vilabu.

Kuna baadhi yetu hata nje huko, maongezi yetu mengi huwa yanahusu sayansi ya biashara, utakuta tumekusanyika kwenye mgahawa sehemu kila mmoja ana kikokotozi na daftari na kalamu.......
 
Wakenya bana kama watoto, kila kukicha kulialia. Punguzeni ujinfa kichwani mwenu.
mimi mwenyewe nilidhani nitakuta wanajadili masuala ya maana, kumbe ni kulialia tu na kulalamika kama watoto wakiwa.

nakuhakikishia hii thread itakufa kifo cha mende very soon. hakuna cha kujadili hapa.labda porojo.

acha turudi kwenye ile thread yetu ya battle.
 
Kila siku tunawaambia hamjuwi nini maana ya muungano, huu ni ugonjwa mlioachiwa na wakoloni na mmashidwa kuutibu. Ikiwa rasilimali za Kenya zimeshikikiwa na wachache na hawataki kugawana na walio wengi, mnategemea mtaweza kugawana na nchi majirani?. (Achana na hizi ahadi fake za visa free za Kenyatta).

EAC waliweka mpango madhubuti wa kugawana kazi ndani ya EAC, mmojawapo ni Kenya kuunganisha magari na nchi zingine watoe hata 30% ya vifaa vitakavyo tumika kuunganiaha hayo magari, batteries, tyres, wiring nk. Je, Kenya wametimiza hiyo ahadi? Jibu ni hapana,, Kenya wanakumbatia fursa zote huku mkitegemea kuuza hayo magari kwenye soko la EAC. Hapo hakuna undugu wala nini, ni akili ya kiungwana inayojenga muungano. Sasa mtashangaa Waganda, Wanyarwanda na nchi zingine wakiangalia maslai yao mahali pengine? Sijaona EU wakinyimana fursa kama Kenya inavyo fanya EAC. Hata South Africa hawabani fursa kwa nchi zote zilizokaribu nao hata Kenya mnanufaika na South Africa.
 

Huko sijui wapi umekwenda kutafuta kwa kutokea, sasa hayo ya mkataba wa kuunganisha magari halafu wengine nyie mtoe vipuri au vifaa vinavyohusiana na uunganishaji wa magari, na eti Kenya waligomea, hayo unayajua wewe na kama una chanzo lete humu tukisome na kuchambua.

Bado narudia, biashara haina undugu, waulize hata maelfu ya Wachagga wanaofanya biashara Kenya, wengi wako huku wanapiga biashara zao na kunufaika pasipokuingiza undugu. Labda wakirudi huko msimu wa Krisimasi kwenye kula mbuzi na 'mbus katolik' na kunywa mbege ndio mnaitana ndugu.
 
Hapo ndio unaniacha hoi, mimi naongelea biashara za nchi kwa nchi, kikanda, na mabara mengine wewe unaongelea biashara za maduka ya Wakamba na Wachagaa. Duh, mbona kazi?

Anyway, hayo maswala ya magari habari zimo huomo mitandaoni. Tokea vikao vya mawaziri na wakuu wa nchi 2016, wamekuwa wanaongelea automotive industry in EAC. Mwaka jana wameongelea swala la uwingizaji wa nguo za mitumba kwenye soko la EAC au hilo nalo utasema hulijuwi? Kifupi Kenya mnapenda kuvutia kila kitu kwenu, halafu mnategemea kufanya biashara na majirani zenu, hiyo biashara itatoka wapi kama majirani zenu na wao hawatengenezi hela. Tumeanza kuzalisha bidhaa zaidi ya Kenya na kupunguza utegemezi wa bidhaa za Kenya, roho zina wadunda. Ndio maana nasema hamjuwi nini maana ya muungano, kwenu kila kitu ni mashindano. Jumuiya zingine hazina michezo kama hii, sio SADC, EU wala ASEAN.
 
Mimi sioni kama kuna chuki kati ya Tz na Ke,,ninachokiona hapa ni UBISHANI na USHINDANI,,tena ushindani wenyewe ni wa KIMAENDELEO

Mathalani,,chukulia uzi unaotrend wa DAR vs NRBI ambao kwa azaidi ya 90% unaongelea maendeleo ya miundombinu ktk majiji haya na wakati mwingine hata kwenye Mikoa.Sema tu kuna kipindi wanaweza toka nje ya mada wakapigana na vijembe kidogo,,na hii sioni kama ni chuki (ni kupata pumziko"kazi na dawa")
 
Inawezekana wewe mgeni humu Jf
au umetumia makusudi tu kutumia Id Mpya ili ulete mada hii,
Waanzilishi wa Haya ni Wakenya wenzie
Na baadhi yao hawapo humu kwa sasa
Ilikuwa shida humu
Watanzania tulipewa Dharau ya kila aina
kejeli yahali ya juu

Ilibidi watu tuunde Id mpya kupambana na madharau hayo
Sasa baada ya kuuona moto mnaanza kulialia
 
Imekuwa too much, I have gone through the treads here and I was shocked. It's like Tanzanians don't want anything do with Kenya. USA and China have rivalry but they still trade with each other.
Hakuna chuki kati ya Mtu Mweusi wa Tanzania na Mtu Mweusi wa Kenya. Amini, nachokuambia Wananchi wa Tanzania na Kenya tunapendana sana kwasababu sisi ni ndugu wa Kiafrika hata Mungu wetu analitambua hilo. Ukweli mchungu ni kwamba kuna mishenzi/mipumbavu mikubwa yenye maslahi binafsi ndiyo inasababisha huo upumbavu. Unachokisema kuhusu threads za kufananisha/kulinganisha kati ya hizi nchi mbili(Tanzania & Kenya) ni kweli kabisa zipo humu JamiiForums na huwa inashishangaza sana.

1:Kwa nini Tanzania na Kenya?
2:Kwa nini isiwe Afrika Kusini na Nigeria au Tanzania na Uganda au Kenya na Kongo?
3:Kwa nini Dar es Salaam na Nairobi na isiwe Nairobi na Maputo au Dar es Salaam na Ouagadougou au Bamako?
4:Ipo siku nitakuwa kiongozi wa Taifa(Raisi) afu nitaifanya Afrika kuwa moja kimabavu iwe kwa damu au chuma, yeyote atakae leta fyokofyoko ataenda kupuliza moto wa Jehanamu.
 
ukute huyu muanzisha mada ni kolo, kaamua kurudi na ID ya dharula....maana kachezea ban huku addiction yake ya jf ikiwa bado juu.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Ndugu yangu samahani sana kama nitakukwaza, ukweli ni kwamba wewe na huyo rafiki yangu mtabishana sana na hamtapata muafaka. Kwasababu unaweza ukawa unabishana na Bepali Kuu "Biashara Haina Undugu " na wewe kumbe ni Mjamaa mwenye msimamo mkali(Mkomunisti), au inaweza ikawa wewe ni Bepali Kuu na yeye ndiye Mkomunisti mwenye msimamo mkali. Naomba mjiweke wazi ili na sisi tujue kama ni Ubepali au Ujamaa.
 

Biashara haina undugu iwe kwa kiwango cha mama nitilie au baina ya nchi. Na pia biashara haiendeshwi kwa chuki, wewe hapo utakaa ukifikiria chuki zako dhidi ya Wakenya zitazingatiwa ikulu wakati wa maamuzi lakini hilo halipo, na nikuhakikishie, biashara baina ya Wakenya na Watanzania inazidi kuongezeka kila siku, hivyo utabaki hapo ukilalamika na kulea chuki wakati wenzako wanachangamkia fursa zinazozidi kuongezeka.

Kila nchi huvutia kwake, ndivyo ilivyo dunia yote nakushangaa hukulijua hilo, mimi nilifikiria kwa utawala wa Magufuli mtaamka na kubadilisha mitazamo ya kizembe ya kiujamaa lakini bado mumelemazwa kiakili. Huyo rais wenu anayo kazi sio haba maana nyie ni shughuli kweli kweli, kabla muamke itachukua muda.
Kuzalisha bidhaa ndani ndio mojawapo wa mfano wa kuvutia kwako, hiyo ni hatua nzuri maana inadhihirisha maendeleo ya nchi, lakini kama mnazalisha ili muikomoe Kenya, basi hapo naona mtachelewa sana maana Kenya tupo kimikakati zaidi, hatuendeshwi na mihemko ya chuki kama nyie. Leo hii tumeanza mikakati ya kumfuata mwarabu wa Sudan na Libya, nia yetu ni kutanua Afrika yote Kenya to open tea warehouses in Sudan with eye on new markets
 
Karibu kwenye forum ndugu yetu Elly Owange. Pia nakukaribisha Tanzania na nikuhakikishie tu kuwa ukifika TZ utaona tofauti kubwa ya ukarimu uliotukuka wa watanzania. Huku kwenye mtando tunasukuma muda tu "don't take the comments seriously".
 
Kenya si tumeijua kupitia Ngugi wathing'o "this time tomorrow"
 
1.Wakenya wengi ni viherehere mbele ya Mzungu

2.Walikuwa ni wa kwanza kuzijua social network kuliko Tanzania hivyo kila zuri la Tanzania wakawa wanawadanganya wazungu kuwa ni ya kwao na hivyo kufanikiwa kupata watalii wengi kiujanjaujanja mfano mlima kilimanjaro, mbuga ya serengeti na Madini ya Tanzanite na hata wasanii maarufu wa gospel na bongoflavour waliitwa wakenya

3. Wakenya wengi wanajua kucheka "kijinopembe" na ni rahisi kukuingiza mkenge hasa mikataba yao mikubwa ya kinchi lazima uirudie mara nne nne maana wapo ki maslahiya kwao zaidi kumbuka wakati wa bomba la mafuta la uganda walikuwa wanatuma mashushushu kuja kuingilia kuna nini kinaongelewa

4. Wakenya wengi wananchi wa kawaika hawana ardhi kwani sheria ya ardhi ya kenya ni tofauti na ya Tanzania huko mabepari wanamiliki for life maeneo makubwa hivyo ni kuishi nao kimachale hasa kwenye mikataba inayohusu ardhi

5.Wakenya wamepotosha kabisa kiswahili na ndio wanahusika kwa kiasi kikubwa kuweka msamiati wa maneno mapya kidigit na kufanya upotoshwaji mkubwa wa lugha adhimu ya kiswahili. Ukitaka kucheka tafuta google translator ama manue ya simu ya kiswahili
 
Mkuu usiwaze still Kenya ni strong katika kila kitu ku compare na Tanzania. Waswahili husema kelele za chura hazimzuii ngombe kunywa maji.
Kenya ni sawa sawa na mtoto anayetembea na Tanzania ni sawa sawa na mtoto anayetambaa
 
Sitaki kuamini kama hapa ndio umemaliza, hapa ndio mwisho wa uwezo wako wa kulewa biashara za kinchi na kikanda. Kinacho nishangaza ni hili neno Ushindani, mnashindana na nani, wateja wenu? Nani mnunuzi wa bidhaa za Kenya na nani mnunuzi wa bidhaa za Tanzania, nani mnunuzi wa bidhaa za Uganda au Rwanda? Hivi kama Marekani ingeamuwa kushindana na bara la Ulaya baada ya vita ya pili ya Dunia, wangeweza kufanya biashara kama wanayoifanya hii leo? Badala ya kukaa meza moja na wateja au washiriki wenu wa kibiashara, nyinyi mnaazisha ushidani kama ule wa CoW. Hizo mbio mnazokimbia kusikojulikana mnategemea kupata nini mwisho wake?
 
Itachukua muda sana kushirikiana na wakenya.
Ni wanafiki sana na wapenda maslahi hata kama wataathiri wengine hawajali....
When you do businesses with wakaenya kuwa makini sana siyo wa kweli......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…