Kenya Vs Tanzania

Mimi nafkiri watanzania tuache ligi ya mabishano na Kenya, tujikite na ishu zetu za ndani, wale jamaa wapo hatua kadhaa mbele kuliko sisi.

  • Sekta ya elimu wametuacha.
  • Sekta ya siasa wametuacha, sisi upinzani ulifutwa kabisa bungeni na bado tukaweka matako chini. Mtu akaamua kufuta matokeo ya uchaguzi zanzibar na bado tukampa heshima.
  • Maisha yanapanda kasi sana bila ya sababu za msingi, mfumuko wa bei ktk mahitaji yetu ya msingi unaendelea kupaa, wakulima bado wana hali ngumu.
  • Nishati ambayo ingekuza viwanda kwetu imekuwa ni shida.
  • Tumeshindwa kuendesha bandari n.k

Muda wa kubishana na Wakenya ni heri tuwekeze mitandaoni ili kuonesha serikali hatufurahishwi na utendaji wake.
 

Toa mambo ya siasa afu tuendelee na mjadala!!!
Huwezi ongelea uchaguzi afu ukaringanisha na maendeleo!!

siasa si kipmo cha maendeleo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…