Kenya: Wakati NASA wakiwa mahakamani, Kenyatta ajiliwaza mbugani

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Wakati Muungano wa Upinzani NASA nchini Kenya, chini ya kinara wao Raila Odinga wakiwa mahakamani kudai haki yao ya kupinga ushindi katika uchaguzi wa Agosti 8.

Rais mteule wa Kenya Uhuru Kenyatta, ameamua kujiliwaza katika mbuga za nchi hiyo huku akisubiri hatma ya kesi.

Picha hizi za Rais mteule Uhuru Kenyatta zimepakiwa katika akaunti zake za Twitter, Instagram akiwatazama tembo na kumeandika kama ifuatavyo;

"Tukijiliwaza katika urithi maridhawa wa taifa letu huku tukisubiri hatma ya mchakato wa mahakama, itunze amani". Ameandika Kenyatta

Mahakama ya juu katika kesi hiyo iliyowasilishwa na Raila Odinga ambaye alikuwa mgombea urais kupitia Muungano wa Upinzani NASA, inatarajiwa kutoa uamuzi kufikia Ijumaa.
 
Uhuru ni kichwa sana aisee. Kuondoa ubishi na malalamiko yasiyo na msingi; kuongeza trust na transparency; ku-improve democracy tenda haki ambayo ni msingi muhimu sana wa amani katika taifa. Katika mazingira kama haya ya Uchaguzi Mkuu wa Kenya atakayelalamika kila mtu atamshangaa. Hongera Rais Uhuru Kenyatta; hakika wewe ni shujaa na mdemokrasia namba moja wa siasa za Afrika zilizojaa upuuzi mwingi.
 
Hon. Uhuru Kenyatta try to remember a meeting conference in 20 / 09 / 2017 in Pretoria, south Africa in grand lodge of father Ian whitternburg Freemasonry.
 
Hao tembo kweli wa msituni au wa kufugwa
Huwezi kumsogelea tembo wa porini namna hii utakuwa hujipendi
 
Hao tembo kweli wa msituni au wa kufugwa
Huwezi kumsogelea tembo wa porini namna hii utakuwa hujipendi
Ni mbugani mkuu. Tembo ukijifanya ujuaji mwingi anakuzingua kuna post hapo #7

Irejee kuisoma utapata kufahamu tabia ya tembo
 


Usikute hapo hao Tembo ni wake yaani mali yake hapo yupo Shambani kwake tu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…